Ukubwa wa Mpaka wa Mkoa wa Kigoma chanzo Njia za Panya nyingi na kuingiza Wageni haramu
Toyi Silvesta Diwani Kata ya Gwanumpu Kakonko Kigoma akiongea na Wananchi kwenye Mkutano wa Hadhala Ukubwa wa Mpaka wa Mkoa wa Kigoma chanzo Njia za Panya nyingi na kuingiza Wageni haramu Kigoma;Kutokana na Mkoa wa Kigoma kuwa na Mpaka mrefu sana kuliko Mikoa yote ya pembezoni huku vituo rasmi vya uhamiaji vikiwa mbali mkubwa toka kituo kimoja hadi kingine hatua inayodaiw a kupelekea uwepo wa njia za panya nyingi na wahamiaji haramu kupata ulaisi wa kuingia nchini jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa Tanzania Mkoa huo unapakana na Nchi za Burundi na Congo DRC upande wa Magharibi na nchi hizo zimekuwa zikikumbwa na matatizo ya usalama na kupelekea Raia wa nchi hizo kukimbia kutafuta sehemu salama Raia wa Nchi jirani wanadaia kuingia Tanzania kwa Vigezo vya kutafuta vibarua kupata Mkate katika maeneo vya Vijiji vya Mpakani Mkoani Kigoma na baadae ulazimika kuendelea kukaa Vijijini humo kinyume cha sheria z...