Ukubwa wa Mpaka wa Mkoa wa Kigoma chanzo Njia za Panya nyingi na kuingiza Wageni haramu

 


















Toyi Silvesta Diwani Kata ya Gwanumpu Kakonko Kigoma akiongea na Wananchi kwenye Mkutano wa Hadhala

Ukubwa wa Mpaka wa Mkoa wa Kigoma chanzo Njia za Panya nyingi na kuingiza Wageni haramu

Kigoma;Kutokana na Mkoa wa  Kigoma  kuwa na  Mpaka mrefu sana kuliko Mikoa yote ya pembezoni huku vituo rasmi vya uhamiaji vikiwa mbali mkubwa  toka kituo kimoja hadi kingine  hatua inayodaiw a kupelekea  uwepo wa  njia za panya nyingi na wahamiaji haramu kupata ulaisi wa kuingia nchini jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa Tanzania

Mkoa huo unapakana na  Nchi za Burundi na Congo DRC upande wa Magharibi na nchi hizo zimekuwa zikikumbwa na matatizo ya usalama na kupelekea Raia wa  nchi  hizo kukimbia kutafuta sehemu salama

Raia wa Nchi jirani wanadaia kuingia Tanzania kwa Vigezo vya kutafuta vibarua kupata Mkate katika maeneo vya Vijiji vya Mpakani Mkoani Kigoma na baadae ulazimika kuendelea kukaa Vijijini humo kinyume cha sheria za Tanzania  na wengine uingia nchini kufanyabiashara katika Masoko ya ujirani mwema yaliyoko Mipakani kasha kuingia Vijijini

Wenyeji hudaiwa kuwapangisha katika Nyumba za Makazi na baadae kununua ardhi na kuishi kama wenyeji kinyume na taratibu huku vitendo visivyofaa vikiendelea kutendeka

Kutokana na hali hiyo Kata ya Gwanumpu iliyoko Wilayani Kako Mkoani Kigoma imeanza udhibiti wa wahamiaji haramu kuendelea kuingia nchini  na kuishi kinyume cha sheria ambapo Viongozi wenyewe kuanzia ngazi za Vijiji wameanza kudhibitiana ambapo katika Kikao cha Viongozi wa Kata hiyo Kikiongozwa na Diwani wa Kata hiyo Toy Silvesta,,Afisa Mtendaji wa Kata hiyo Rashid Ahnmed amewaeleza Viongozi kuanzia ngazi za Vitongoji wanaowapangisha wahamiaji kuwaondoa mara moja kabla hatua hazijaanza kuchukuliwa

‘’Hatuwezi kuanza kuwaandama wananchi wakati wapo Viongozi wanaosadikiwa kuwahifadhi wahamiaji haramu na hicho ndicho chanzo cha kuanza upotevu wa amani’’ amesema Shadi

Akiwa kwenye Mkutano wa hadhala akiongea na Wananchi Diwani wa Kata hiyo Toyi Silvesta amewashauri wananchi kuacha Tabia ya kuwakumbatia wahamiaji haramu maana ni kinyume na sheria za Nchi na atakaekutwa anawaifadhi watu hao atachukuliwa hatua na Masoko yote ya Mpakani lazima mwisho iwe saa kumi na mbili jion  

Toyi ameongeza kuwa kumekuwepo na tabia ya kuoleana kiholaholela hatua inayochangia kuongezeka wageni hao huku wengine wakiingia naa Mifugo na kusababisha magomvi kati yao na wageni hao

Baadhi ya Wananchi wameeleza kuwa ni vema serikali kupitia Idara ya uhamiaji  ingeweka Doria za Mara kwa mara  kwenye Vijiji ili kudhibiti hali hiyo kwani wapo wageni hao ambao wamekuwakijificha vijijini na wengine walishapewa uongozi kwenye serikali za Vijiji na kwenye vyama vya siasa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

40 CHADEMA KIBONDO WAJIONDOA