Israel yaishambulia Iran kwa makombora, yenyewe yaahidi kulipiza kisasi


 Taharuki imetanda mashariki ya kati kufuatia mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Israel katika mji mkuu wa Iran, Tehran, Ijumaa asubuhi. Milipuko mikubwa ilisikika kote Tehran, huku Israel ikitangaza kuwa imelenga maeneo ya nyuklia na vituo vya kijeshi.

Mashambulizi haya yanakuja wakati mvutano kati ya nchi hizo mbili umefikia kiwango cha juu kabisa kufuatia maendeleo ya haraka ya mpango wa nyuklia wa Tehran.

Mashambulizi hayo pia yalipiga mji wa Kermanshah magharibi mwa Iran, ambapo wakazi walisema walisikia milipuko na kuona moshi mweusi ukipanda juu ya jiji. Haikubainika mara moja ni nini hasa kililengwa. Milipuko pia ilisikika karibu na mji wa Tabriz nchini Iran, ingawa hali halisi huko bado haijawa wazi.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu