HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE
Muhingo Mwemezi Kibondo
Baraza la
Halmashauri ya Kibondo na Kikao cha ushauri cha Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma
vimepitisha mapendekezo ya kuligawa jimbo la Muhambwe kuwa majimbo mawili kwa
kile kinachotajwa kuwa ni kusogeza huduma karibu na wananchi
Daniel
Ndalangavye ni Afisa uchaguzi halmashauri ya kibondo yeye katika taarifa yake
anasema mapendekezo hayo yamezingatia vigezo vilivyotolewa na Tume huru ya
uchaguzi Tanzania ikiwa baadhi yake ni Idadi ya Watu, Ukubwa wa Eneona
ukusanyaji wa ushuru na kodi huku akieleza kuwa kulingana na Jiografia ya
eneo wananchi wengi wamekuwa wakipata
usumbufu kuifikia ofisi ya Mbunge kwa sasa kutokana na umbali hivyo Jimbo
likigawanywa Wabunge wa Majimbo hayo
wataweza kuwahudumia wananchi kwa ufasaha zaidi
Awali Jimbo
la Muhambwe liliitwa Kibondo na mwaka 2010 likagwaanywa Majimbo mawili Buyungu
Kakonko baadae kuitwa Muhambwe na sasa inapendekezwa Muhambwe kugawanywa tenda
ambapo wajumbe wajumbe wa Baraza na Kikao cha ushauri wanapendekeza majina
mapya yanayotakiwa kutumika baada ya Mgawanyo
Insert Paul Ngomagi
Katika Kikao cha Baraza la
MadiwaniPaul Ngomagi alipendekeza liwepo Jimbo la Kibondo Mashariki na Kibondo
Maghari huku baadae kwenye Kikao cha ushauri wilaya Mjumbe wa Kikao hicho
Philbath Misuzi alipendekeza Jimbo Jipya
liitwe Muhambwe Magharibi na Jimbo la zamani liitwe Muhambwe Mashariki
Vikao vyote viwili kwa nyakati
tofauti viliridhia kugawanywa kwa jimbo la Muhambwe huku Mkuu wa Wilaya ya
Kibondo mwenyekiti wa Kikao cha ushauri Aggrey Magwaza akieleza kuwa
mapendekezo hayo yanapelekwa kwenye vikao vya maamuzi kwa hatua zaidi hivyo
taarifa zitatolewa baada ya maamuzi
Wilaya ya
Kibondo ina jimbo moja la uchaguzi na Halmashauri moja ambapo baadhi ya washiriki wa vikao hivyo Shedrack
Chongera na Ladbod loki Katobahemu wakieleza kuwa hatua hiyo iatasaidia kupunguza adha kubwa
wananchi kutembea umbali mrefu kufuata huduma za kijamii kwenye ofisi za umma
Maoni
Chapisha Maoni