KASEKENYA AWATAKA VIJANA ILEJE KUJIKITA KWENYE MICHEZO

 















KASEKENYA AWATAKA VIJANA ILEJE KUJIKITA KWENYE MICHEZO

Naibu Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Ileje, Mhandisi, Godfrey Kasekenya

amewataka vijana Wilayani Ileje, mkoani Songwe kujikita kwenye michezo

na kutumia fursa ya mashindano ya kombe la Kasekenya kuimarisha afya,

ushirikiano na kukuza vipaji.

Akizindua Bonanza la kuhamasisha michezo Wilayani huko, Mbunge

Kasekenya amesema wilaya hiyo imedhamiria kuwekeza kwenye michezo

ili kukuza vipaji vya vijana na kuwawezesha kupata ajira.

"Mashindano haya yatumike kama chachu ya kuhamasishana kufanya kazi

kwa bidii na kukuza vipaji kwani michezo ni ajira, afya na urafiki", amesema

Mhandisi, Kasekenya.

Aidha, Kasekenya amesema kuwa Mashindano hayo pamoja na mambo

mengine yanahamasisha wananchi kujiandikisha kupiga kura, kugombea

na kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa Novemba 27 mwaka huu.

Amefafanua kuwa Bonanza hilo ambalo ni uzinduzi wa Kasekenya Cup

limekutanisha timu za mpira wa miguu wanaume na wanawake, vikundi

vya muziki wa asili, riadha, na uchezaji wa muziki ambapo washindi

wamejizolea zawadi mbalimbali.

Katika soka, timu ya Makaburu ya jimbo la Busokelo, mkoani Mbeya

imeifunga kombaini ya Sange iliyopo wilayani Ileje, mkoani Songwe bao 3

kwa 2 wakati wanawake Lubanda wakishinda kwa penati 3 kwa 2 dhidi ya

Kalembo FC baada ya sare ya bao 2 kwa 2.

Viongozi mbalimbali wa Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa wa Songwe wa

vyama na Serikali wameshiriki Bonanza hilo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu