DC MISUNGWI AHIMIZA WAZAZI NA WALEZI KUANDIKISHA WATOTO MASHULENI KWA WAKATI

 DC MISUNGWI AHIMIZA WAZAZI NA WALEZI KUANDIKISHA WATOTO MASHULENI KWA WAKATI



Johari Samizi Mkuu wa Wilaya ya Misungwi

Mary Mussa Mwalimu Shule ya Msingi Misungwi


                                                      

Klaud Richard Mkazi wa Misungwi


Pamoja na Wilaya
ya Misungwi Mkoani Mwanza kuendelea kufanya vizuri katika uandikishaji wa Wanafunzi Elimu awali na Msingi, bado hamasa inahitajika  kutolewa kufia malengo yanayokusudiwa

Matarajio ya mwaka 2026 kwa Elimu awalini ilikuwa ni  kuandikisha Watoto 13219  na walioandikishwa hadi sasa ni  6403 huku dara la Kwanza  wanatarajia kuandikisha Wanafunzi  14551 na mpaka sasa Watoto 9082 wamekwisha kuandikishwa wakati zoezi likiendelea 

Akiongea Ofisini na Waandishi wa Habari  Kwake Mkuu wa Wilaya Misungwi Johari Samizi ameeeleza  uandikishaji wanafunzi unavyoendelea na maelekezo yote yametolewa kwa Viongozi wa Vitongoji Vijiji na Kata, kuwaelimisha Wananchi na mchakato huo unaendelea vizuri

Samizi ameendelea kuwahamasisha Wazazi na Walezi kupeleka watoto wao waandikishwe kwa wakati kabla shule hazijafunguliwa ili  kuepuka usumbufu na kuhakikisha wanafunzi 7019 waliochaguliwa kunza kidato cha kwanza mwaka 2026,wanaripoti kwa wakati

‘’Kama inayohamika Wakazi wa eneo letu hili wanajishugulisha na ufugaji na Kilimo hatua ambayo upelekea baadhi ya Wazazi kuwatumia Watoto wanaotakiwa kuwa mashuleni kufanya shughuli  hivyo nawahimiza  kila mmoja kuhakikisha Mtoyo wake anapata Elimu’’ ameeleza Johari Samizi Mkuu wa Wilaya ya Misungwi

Klaud Richard na Bakari Husein ni baadhi ya Wazazi na walezi Wakazi wa Misungwi wameeleza kuwa  wamejipana kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni wjibu wao kama wazazi  huku mmoja wa walimu wa shule ya Msingi Misungwi Maria Mussa akieleza katika shule yake zoezi la uandikishaji linaendelea vizuri japo shule bado hazijafunguliwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

40 CHADEMA KIBONDO WAJIONDOA