Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2017

Morogoro;Takwimu zinaonyeshaTanzania bado inakabiliwa na kiwango cha juu cha ukatili wa kijinsia ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, pamoja na vipigo kwa wanawake kutoka kwa waume zao licha ya juhudi mbali mbali za kupinga hatua hiyo na sheria kali kutungwa bado matukio ya aina hii yanazidi kuongezeka.

Picha
Morogoro; Takwimu zinaonyeshaTanzania bado inakabiliwa na kiwango cha juu cha ukatili wa kijinsia ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, pamoja na vipigo kwa wanawake kutoka kwa waume zao licha ya juhudi mbali mbali za kupinga hatua hiyo na sheria kali kutungwa bado matukio ya aina hii yanazidi kuongezeka. Utafiti wa hali ya afya ya uzazi,mtoto na malaria wa mwaka 2015/2016 unaonesha kuwa idadi ya wasichana wanaopata watoto katika umri wa miaka 15-19 imeongezeka mpaka kufikia asilimia 27 mwaka 2015 kutoka asilimia 23 mwaka 2016 Vitendo vya ukatili wa kijinsia hapa nchini vinatajwa kuendelea kuwepo licha ya juhudi nyingi za kupiga vita vitendo hivyo kutiliwa mkazo ikiwa ni pamoja na mashirika mbalimbali na serikalia kwa ujumla hasa kusababishwa na uelewa mdogo katika jamii kufichua vitendo hivyo     Baadhi ya tafiti zinaonyesha kuwa licha kuendelea kuwepo kwa vitendo hivyo, Tanzania bado iko katika nafasi nzuri ya kupiga vita ukatili huo katika bara

Tatizo la ugonjwa wa Malaria linaloonekana kuwa moja ya sabababu za kupunguza nguvu kazi ya Taifa jamii imetakiwa kushirikiana bega kwa bega na serikali ili kuutokomeza ugonjwa huo hasa kwa kuharibu maeneo ya mazalia ya Mbu na katika makazi ya watu

Picha
Mkuu  wa wilaya ya Kibondo Luis Bura akinyunyizia dawa ya kuuwa Vimelea vya Malaria katika Bwawa kufugia samaki katika Kijiji cha Biturana Juma Mnwele mkurugenzi Halmashauri ya Kibondo Raya Chamabali mratibu Kitengo cha Malaria W Kibondo Tatizo la ugonjwa wa Malaria linaloonekana kuwa moja ya sabababu za kupunguza nguvu kazi ya Taifa jamii imetakiwa kushirikiana bega kwa bega na serikali ili kuutokomeza ugonjwa huo hasa kwa kuharibu maeneo ya mazalia ya Mbu na katika makazi ya watu Takwimu za   Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto zinaonyesha hali ya maambukizi na vifo vitokanavyo na ugonjwa wa malaria imepungua kutoka asilimia 90 ya maeneo yenye mbu  hadi kufikia  asilimia 50  ya walioambukizwa  malaria tangu 2000 hadi 2017. Aidha takwimu hizo zimebainisha kuwa, mikoa ya kanda ya ziwa ikiwemo Kagera na Geita  na mikoa ya Nyanda za juu Kusini ambayo ni Mtwara na Lindi ndiyo inayoongoza kwa maambukizi pamoja na idadi ya