Morogoro;Takwimu zinaonyeshaTanzania bado inakabiliwa na kiwango cha juu cha ukatili wa kijinsia ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, pamoja na vipigo kwa wanawake kutoka kwa waume zao licha ya juhudi mbali mbali za kupinga hatua hiyo na sheria kali kutungwa bado matukio ya aina hii yanazidi kuongezeka.









Morogoro;Takwimu zinaonyeshaTanzania bado inakabiliwa na kiwango cha juu cha ukatili wa kijinsia ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, pamoja na vipigo kwa wanawake kutoka kwa waume zao licha ya juhudi mbali mbali za kupinga hatua hiyo na sheria kali kutungwa bado matukio ya aina hii yanazidi kuongezeka.

Utafiti wa hali ya afya ya uzazi,mtoto na malaria wa mwaka 2015/2016 unaonesha kuwa idadi ya wasichana wanaopata watoto katika umri wa miaka 15-19 imeongezeka mpaka kufikia asilimia 27 mwaka 2015 kutoka asilimia 23 mwaka 2016

Vitendo vya ukatili wa kijinsia hapa nchini vinatajwa kuendelea kuwepo licha ya juhudi nyingi za kupiga vita vitendo hivyo kutiliwa mkazo ikiwa ni pamoja na mashirika mbalimbali na serikalia kwa ujumla hasa kusababishwa na uelewa mdogo katika jamii kufichua vitendo hivyo
  
Baadhi ya tafiti zinaonyesha kuwa licha kuendelea kuwepo kwa vitendo hivyo, Tanzania bado iko katika nafasi nzuri ya kupiga vita ukatili huo katika bara la Afrika ikilinganishwa na mataifa mengi ya bara la Afrika. Imeshika nafasi ya 6 zaidi ya mataifa ya Lesotho, Msumbiji,  Togo, Afrika Kusini na Namibia.

Makundi mbalimbali wakiwemo wanahabari wametakiwa kuendelea kutoa elimu katika jamii, kauli hiyo imetolewa na mkufunzi wa maswala ya kijinsia Agnes Kabigi katika mafunzo na waandishi wa habari ya kujenga uelewa juu kupinga ukatitili huo yanayofanyika mjini Morogoro

Kabigi alisema kwa kuwa Wanahabari nao ni sehemu ya jamii inawapasa kupaza seuti za wanyonge ili kufikia malengo yanayokusudiwa kwani hali ukatili huo bado upo na umekuwa ukuripotiwa japo kwa kiwango cha chini huku baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo Ambao ni Seny Emmanuel na Mwajuma Mmanga walisema, ili kufikia malengo ni vema ushirikiano ukawepo kwa makundi husika na sheria ikafuata mkondo

‘’Licha ya kuonekana kuwekwa  wazi badhi ya matukio, bado hali haijawa nzuri kwani vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia viaendelea kushamili katika baadhi ya maeneo hapa nchini na vingi haviripowi kutokana na changamoto mbalimbali zinazoyakabili makundi tofauti ikiwemo ukiwemo ukandamizaji ‘’ alisema Kabigi

Hata hivyo kwa upande wao baadhi wakazi wa Mji wa Morogo ambao ni Frola Poul na Emmanuel Wilson, walisema kuwa mfumo dume mitazamo ya baadhi ya watu na kukwepa majukumu imekuwa nisababu ya wanawake na Wanaume kukosa haki zao

''Wanaonyanyswa si wanawake pekee kama inavyofikiriwa na Watu wengi hata wanaume katika Familia wapo wanaokosa haki za kimsingi nao migawanyo ya majukumu kwa upande wao haijawa sawa kikubwa ni kuelimishana ili kubadili Tabia na mitazamo inayotokana na hulkaka mbalimbali kama malezi, Makabila na Uelewa Mdogo’’ alisema Wilson.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao