Machapisho

UWINDAJI HARAMU WASABABISHA IDADI SOKWE KUPUNGUA GOMBE

Picha
  Na Emmanuel Matinde Kigoma Idadi ya wanyama aina ya Sokwe katika Hifadhi ya Taifa ya Gombe iliyoko mkoani Kigoma, inaelezwa kupungua kwa kasi kutokana na kuwindwa, kuharibu maeneo yao ya asili, pamoja na shughuli za kibinadamu ambazo zinahatarisha maisha yao. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Utafiti wa Sokwe kutoka Taasisi ya JANEGOODALL (JGI), Dr. Deus Mjungu, huku akitoa wito kwa wadau wote kuona umuhimu wa kuwalinda Sokwe ili waweze kuongezeka.   Nchini Tanzania Sokwe, hupatikana katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi lakini kuongezeka kwa idadi ya watu na katika maeneo yaliyo karibu na makazi yao kunatajwa kutishia maisha yao amesema ShedrackKamenya Mhifadhi Mkuu Mstaafu toka Taasisi ya JGI.     Ikumbukwe kuwa wanyama aina ya Sokwe ambao tabia zake hufanana kwa asilimia 98% na binadamu, ni kivutio cha utalii kinachoiingizia serikali fedha za kigeni na kusaidia kukuza uchumi hivyo jamii ina jukumu la kushirikiana na serikali kuhakikisha wa...

MAHUNDI APONGEZA UWAJIBIKAJI KAKONKO ASHAURI WAONGEZE JUHUDI

Picha
  Na Cosmas Makala Kakonko Kakonko . Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi , amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Kakonko, mkoani Kigoma, ambapo alianza kwa kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kakonko. Katika kikao hicho, alipatiwa taarifa ya maendeleo ya Wilaya iliyowasilishwa na mkuu wa wilaya Col. Evance Mallasa ikieleza mafanikio yaliyopatikana pamoja na hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa manufaa ya wananchi. Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Mhe. Mahundi aliupongeza uongozi wa Wilaya ya Kakonko ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya,Col. Mallasa kwa usimamizi mzuri wa shughuli za maendeleo,Pia aliwapongeza Mh. Mbunge Alan Mvano, Katibu Tawala wa Wilaya Maulid Said Mtulia, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndaki Stephano Mhuli, kwa ushirikiano na ufanisi wanaouonyesha katika kusimamia utekelezaji wa mipango ya Serikali, jambo ambalo li...

SIKU YA UJUZI KWA VIJANA

Picha
Monica Mwita Mwanafunzi Veta Mwanza Voronica Gabriel Mkufunzi Veta Mwanza Flaviana Minda Kaimu Mkuu wa Chuo Veta Mwanza     Yapo naneno ya Wahenga yasemayo,Ushindi ni Mwenendo, Mwenendo huo ni Kazi, Kazi ni mawazo, mawazo ni kuelewa na imani, na hivyo kila kitu kinaanzia kwa   binadamu. Kuendana na maneno hayo,mnamo  2014, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilitangaza tarehe ya Julai 15 iwe siku ya Ujuzi wa Vijana Duniani, kuweka mikakati ya kuwaandaa vijana kwa ujuzi unaohitajiwa kuwaajiri na kuwawezesha kupata kazi licha ya kuwawezesha kwa Ujasiriamali.    Siku ya Kimataifa ya Ujuzi kwa Vijana huadhimishwa kila tarehe 15 Julai. Siku hii ilianzishwa na Umoja wa Mataifa ili kuhamasisha na kutambua umuhimu wa kuwapa vijana ujuzi na stadi mbalimbali za kazi ili waweze kujitegemea kimaisha na kuchangia maendeleo. Lengo kubwa ni kukumbusha jamii na serikali kutoa nafasi za mafunzo zitakazowawezesha vijana kupata ujuzi unaohitajika katika soko la ajira, has...

KIBONDO YAENDELEZA UDHIBITI UGONJWA EBOLA

Picha
  DktSimon Omary  Mratibu huduma za Afya Wilaya ya Kibondo Fiboreen Siwale Mratibu wa Maralia Wilaya ya Kibondo Aggrey Magwaza Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Mkuu wa wilaya ya kibondo Mkoani Kigoma, kanali Mstaafu   Agery Magwaza amewaagiza wataalamu wa afya kuendelea kufanya tafiti za kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa maralia kutokana na ugonjwa huo kutodhibitiwa kwa ufasaha na kuendelea kuleta athari kwa jamii Amebainisha   hayo wakati wa kikao Cha kamati ya afya ya msingi ya Wilaya, walipokua wakijadili namna ya kudhibiti ugonjwa huo ambapo amesema maambukizi ya ugonjwa yamekua yakisababisha madhara kwa jamii kutokana na mbu wannasambaza vimelea hivyo vya   malaria kushidwa kudhibitiwa ipasavyo   Aidha katika kikao hicho kilijadili namna ya kukabiliana na ugonjwa wa ebola ndani ya wilaya ya kibondo huku mkuu huyo wa wilaya akwahimiza wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo ikizingatiwa Wilaya hiyo iko mpakani mwa nchi,   Ili usien...

ONGEZEKO LA IDADI YA WATU NI TATIZO LA KIMATAIFA

Picha
  Ongezeko la idadi ya watu Duniani, ni tatizo la kimataifa na na linatajwa kusababisha changamoto mbalimbali za Kibinadamu japo uwepo wa Binadamu katika uso wa Dunia ni jambo la muhimu Kwa mujibu wa makadirio ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa kupitia Divisheni ya Idadi ya Watu ya UN (UN DESA Population Division), ni kwamba   kufikia mwezi Julai 2025, dunia ilikadiriwa kuwa na zaidi ya watu bilioni 8.1. Nchi zenye Idadikubwa   ya Watu Duniani ni   ni China na India   ambapo katika Nchi ya India kuna Watu wapatao 1,339,180,127 na China ikiwa na Idadi ya Watu 1,409,517,397 huku Bara la Afrika likiwa na Watu billion 1.58 Kila uchao Wanadamu wamekuwa wakiongezeka kwa kasi huku Dunia ikiwa pale pale na mahitaji ya lazima   ya kibindamu kama ardhi   vikiwa haviongezeki   na huduma za Afya, Maji, Chakula na makazi,   upatikanaji wake ukiwa ngumu na kuufanya ulimwengu kuwa katika hali ya hatari ya kukumbwa na Majanga ya Kibinadamu Kutok...

BOSI TRA MIAKA 20 JERA

Picha
  Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma imemhukumu kifungo cha miaka ishirini gerezani aliyekuwa Meneja wa TRA Wilaya ya Kibondo, Irving Bagasheki, baada ya kupatikana na hatia katika makosa mawili ya kujihusisha na nyara za serikali kinyume cha sheria. Hukumu hiyo imetolewa Juni 29, 2026 na Hakimu Mkazi Mfawidhi Aristida Tarimo mbele ya jopo la mawakili wa serikali, baada ya ushahidi wa upande wa mashtaka kuthibitisha bila kuacha shaka kwamba Bagasheki alihusika na usafirishaji wa meno ya tembo mawili yenye thamani ya shilingi milioni 52. Mnamo Julai 1, 2024 Bagasheki alikamatwa katika eneo la Kihomoka wilayani Kakonko mkoani Kigoma akiwa ndani ya gari ya serikali lenye namba za usajili STL – 7274 akijaribu kusafirisha meno ya tembo kinyume na sheria za nchi, Baada ya kukamatwa Bagasheki na wenzake watano walifunguliwa kesi namba 4733 ya mwaka 2025 kwa makosa ya kupatikana na nyara za serikali isivyo halali. Katika kosa la kwanza, mshtakiwa amehukumiwa kifungo cha miaka ishirini...

MATUMIZI YA YA TUMBAKU NI HATARI

Picha
  Siraji Abubakari Mkazi wa Ilemela Mwanza Haruna Hashimu Mkazi wa Mwanza       Siku ya Kupinga Matumizi ya Tumbaku Duniani,   huadhimishwa Mei 31 kila mwaka. Siku hii inalenga kuongeza uelewa juu ya hatari za matumizi ya tumbaku, hatua za kudhibiti tumbaku na kufichua mbinu hatari zinazotumiwa na makampuni ya tumbaku.   Nchi Wanachama wa Shirika la Afya Ulimwenguni ziliunda Siku ya Kupinga Matumizi ya Tumbaku Duniani mwaka 1987 ili kueleza janga la tumbaku, vifo vinavyoweza kuzuilika na magonjwa yanayosababishwa na tumbaku.   Kwa maelezo ya Shirika laAfya Duniani, Matumizi ya tumbaku, yana athari mbaya kwa mwili,hudhuru karibu kila kiungo katika mwili, na uvutaji tumbaku, ni moja ya sababu kuu ya vifo vya mapema ambavyo husababishwa na na Magonjwa kama SarataniKifua na na mengine   na wahanga wakubwa ni vijana   Kwa mujibu wa WHO, matumizi ya tumbaku huuwa takribani watu milioni sita kila mwaka. Watu laki sita kati ya hao, hu...