ONGEZEKO LA IDADI YA WATU NI TATIZO LA KIMATAIFA
Ongezeko la idadi ya watu Duniani, ni tatizo la kimataifa na na linatajwa kusababisha changamoto mbalimbali za Kibinadamu japo uwepo wa Binadamu katika uso wa Dunia ni jambo la muhimu Kwa mujibu wa makadirio ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa kupitia Divisheni ya Idadi ya Watu ya UN (UN DESA Population Division), ni kwamba kufikia mwezi Julai 2025, dunia ilikadiriwa kuwa na zaidi ya watu bilioni 8.1. Nchi zenye Idadikubwa ya Watu Duniani ni ni China na India ambapo katika Nchi ya India kuna Watu wapatao 1,339,180,127 na China ikiwa na Idadi ya Watu 1,409,517,397 huku Bara la Afrika likiwa na Watu billion 1.58 Kila uchao Wanadamu wamekuwa wakiongezeka kwa kasi huku Dunia ikiwa pale pale na mahitaji ya lazima ya kibindamu kama ardhi vikiwa haviongezeki na huduma za Afya, Maji, Chakula na makazi, upatikanaji wake ukiwa ngumu na kuufanya ulimwengu kuwa katika hali ya hatari ya kukumbwa na Majanga ya Kibinadamu Kutok...