Machapisho

DC KIGOMA AWATAKA WANANCHI KULINDA MAZINGIRA KWA KUTUMIA NISHATI SAFI

Picha
  FROLENCE  MASUNGA MWAKILISHI ENVOTEC Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid Mohamed Chuachua, ametoa wito kwa wananchi wilayani humo kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, kwenye ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kulinda na kuhifadhi mazingira. Rashid Chuchua Dc Kigoma Dkt. Chuachua ametoa wito huo wakati wa akizindua ugawaji wa majiko sanifu ya kupikia ya gharama nafuu yenye ruzuku ya serikali, kwa wananchi katika kata ya Simbo wilayani Kigoma, ambapo amesema kuwa matumizi ya majiko sanifu ni hatua muhimu ya kubana matumizi na zaidi kulinda na kuhifadhi mazingira, kwa kuwa majiko hayo yanatumia nishati kidogo. Kampuni ya ENVOTEC iliyopewa dhamana ya kuuza majiko hayo kwa bei ya ruzuku kupitia Wakala wa Nishati Vijijini REA, kwa ujumla imegawa majiko 1,404 kwa wilaya ya Kigoma, ambapo mwakilishi wa kampuni hiyo Florence Masunga, amesema wananchi watachangia asilimia 15% tu ya bei huku serikali ikilipia asilimia 85%. . Baadhi ya wananchi waliopata majiko...

KATIKA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO SERIKALI IMETOA GARI LENYE MTAMBO WA KUZIMIA MOTO KATIKA WILAYA YA KIBONDO

Picha
  Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma imepokea gari (mtambo) utakaosaidia katika kukabiliana na majanga ya moto yanapotoke Uzinduzi wa mtambo umefanyika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kibondo ambapo mkuu wa wilaya hiyo Kanali Aggrey Magwaza amesema mtambo huo utasaidia kwa kiasi kikubwa hasa pale zitakapotokea changamoto za ajali za moto Aidha ameagiza uongozi wa halmashauri chini ya mwenyekiti wa halmashauri Bw. Alex Baragomwa kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa zimamoto katika upatikanaji wa maji, mafuta na matengenezo ya mtambo huo ili uendelee kutoa huduma katika hali ya ubora Awali kaimu Kamada wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Kigoma Mrakibu masaidizi Michale Maganga amesema imani yake ni kwamba, kuwepo kw amtambo huo kutawafanya wananchi wa wilaya ya Kibondo wawe salama zaidi dhidi ya majanga ya moto Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibondo Bw. Alex Baragomwa pamoja na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wa wilaya hiyo Bw. Hamisi Tahiro wameomba elimu izidi kutolew...

UKARABATI WA MELI YA MV LIEMBA MKOANI KIGOMA WAFIKIA 64%

Picha
  Dkt Rashid Chuachua Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Serikali ya Tanzania yaendelea kukarabati Meli ya Mv Liemba ambayo imekuwa ikifanya shughuli zake katika Ziwa Tanganyika na zoezi hili linafanyika Mkoani Kigoma [engo ikiwani kuboresha huduma za usafiri wa Majini kwa Wananchi wa Mwambao wa Ziwa Tanganyika na Nchi jirani za Burundi Congo DRC na Tanzania Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, amemshukuru Rais wa JamhurI ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha zaidi ya Shilingi Bilioni 32 kwa ajili ya ukarabati mkubwa wa Meli ya Kihistoria ya Mv.Liemba. Shukrani hizo za Mkuu wa Mkoa Balozi Simon Sirro kwa Rais, zimetolewa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid Chuachua, wakati alipomwakilisha kwenye mapokezi ya Injini mbili zilizofika kwa ajili ya kukamilisha ukarabati mkubwa wa Meli ya Mv.Liemba katika Bandari ya Kigoma. Amesema hatua hiyo inaashiria historia mpya kwa wana Kigoma kwenye sekta ya usafiri na usafirishaji katika Ziwa Tang...

KIBONDO YAENDELEZA KAMPENI KUUNGANISHA WATOTO WANAOISHI MITAANI NA FAAMILIA ZAO NA WENGINE KURUDISHWA MASHULENI

Picha
  Aneth Kolman Mkuu wa Dawati la Jinsia Jeshi la Polis Kibondo Sophia Gwamagobe Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma Lukas Lazaro mwakilishi wa Mkurugenzi Halmashauri ya Kibondo Skola Kachiila Mkazi wa Kibondo Elias Jackson Mkazi wa Kibondo Kuendelea kuwepo Watoto wanaofanya kazi na kuishi mitaani, hali hiyo imetajwa kuchochewa na baadhi ya Wazazi kutumia ukali zaidi katika kuwakanya, migogoro ya familia, umasikini na utukutu wa watoto wenyewe mambo hayo hupelekea kutoroka katika familia na kuishi mitaani Wengi wa Watoto hao wanapoingia Mitaani huanza kufanyabiashara za kuokota na kuuza chupa za plastic na Vyuma chakavu na wengine kazi za majumbani na wanaokosa shughuli hujuhusisha na udokozi hatua ambayo ni hatari kwa maisha yao maana wengi wao ni wanakuwa na umri mdogo Hayo yamebainishwa katika maadhimisho ya Mtoto anaeishi na kufanya kazi mitaani ambapo Afisa ustawi wa jamii wilaya ya Kibondo Kigoma, Sophia Gwamagobe ameeleza kutokana hali hiyo watoto huroka...

MANISPAA YA ILEMELA YAENDELEZA MPANGO WA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI KWA KUTOA TSH 625 KWA ROBO YA TATU 2026 10% MAKUNDI MAALUM

Picha
  Watu milioni 800 duniani wanatajwa kuishi katika umaskini uliokithiri na aina nyingi za umaskini zinasababishwa na kuongezeka kwa idadi ya watu wasio na ajira ajenda ya Umoja wa Mataifa ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030, ambayo yameliweka suala la kupambana na umaskini kama lengo kuu kuzishauri nchi zote kuutokomeza umaskini Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, siku ya kupambana na umaskini inaadhimishwa kwa kuzingatia wito uliotolewa miaka 25 iliyopita ya kutambua ujuzi na ujasiri wa familia zinazoishi katika umaskini duniani kote, umuhimu wa kuwafikia Watu maskini na kuwawezesha kiuchumi Tanzania ni moja ya nchi Duniani ambayo inaendelea Mikakati ya kupambana na umasikini   kwa   kuwawezesha Wananchi kiuchumi ,kutokana na hatua hiyo, Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza imeendeleza mpango huo ambapo katika robo ya tatu 2026 Vikundi 41 Vimepatiwa Mikopo ya 10%   amebainisha Kaimu Afisa Maendeleoa Manispaa hiyo Yusuph Okoko wakati wa hafla ya utoaji hudi ...

WATUMISHI SITA IDARA YA AFYA MKOANI KIGOMA WAMEKUFA MAJI ZIWA TANGANYIKA

Picha
  Watu sita ambao ni watumishi wa idara ya afya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wamethibtika kufa, watatu wakiwa bado hawajapatikana wengine tisa wakiokolewa wakiwa hai baada ya boti waliokuwa wanasafiria kuzama katika Ziwa Tanganyika katika Kijiji cha Kalalangabo wilayani humo. Akithibitisha vifo hivyo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Balozi Simon Sirro, amesema tukio hilo limetokea mapema leo Ijumaa Machi 13, 2026 asubuhi, wakati watumishi hao wakisafiri kwenda kijiji cha Kagunga kwa ajili ya kutoa chanjo kabla ya boti yao kupigwa na dhoruba kufuatia upepo mkali na kupinduka. Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kigoma, Mrakibu Msaidizi Michael Maganga, amesema zoezi la kuwatafuta watu watatu watumishi wa idara ya afya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, miongoni mwa waliopinduka na boti katika Ziwa Tanganyika eneo la Kalalangabo bado linaendelea. Aidha Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Kigoma ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Mkuu wa Wilaya hiyo, imepiga ka...

Magu yapunguza vifo vitokanavyo na uzazi asilimia 70 kwa miaka mitano

Picha
  Mwanza . Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza imefanikiwa kupunguza Vifo vitokanavyo na uzazi   kutoka vifo 112 hadi 42 katika kipindi cha miaka mitano baada ya serikali kuboresha huduma kwa kutoa vifaa na kuongeza miundombinu ya majengo Voronica Gibson Mkazi wa Magu Hellen Chizere Muuguzi mfawidhi Hospitali ya Wilaya ya Magu Raphaem Mhana Mganga Mkuu W ya Magu Raphael Mhana Mganga Mkuu Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza ameeleza kipindi cha2015hadi 2020,   hali ilikuwa hairidhishi ikilinganishwa na takwimu kuanzia 2020 hadi 2025   baada ya kufanyika   maboresho katika sekta ya Afya Hata hivyo Mhana amesema kutokana na maboresho hayo kwa sasa wanatengeza na Miguu bandia ambayo inasaidia Watu wanaopata matatizo mbalimbali zikiwemo ajali ‘’Wagonjwa wenye Matatizo ya Viungo hasa Miguu walemavu wa kuzaliwa na wanaokuwa wamepata ajali katika Wilaya ya Magu na maeneo ya jirani,wamekuwa wakisafiri kwenda mbali kutafuta huduma ya Miguu bandia lakini kwa hivi sasa   baada...