Machapisho

Viongozi wa Vijiji na Kata simamien na kutoa elimu umuhimu wa Lishe

Picha
  Kibondo. Viongozi wa Kata na Vijiji wamehaswakuendelea kuhamasisha umuhimu wa Lishe na mpangilio wa matumizi ya vyakula kwa Watoto na watu rika zote ukiwemouchangiaji wa chakula Mashuleni ili kupunguza udumavu na kuinua kiwango cha Elimu Amebainishahayo Afisa Lishe Wilaya ya Kibondo Tumaini Muna wakati wa kujadili ripoti ya utekelezaji afua za Lishe kwa robo yanne 2025/26 ambapo ameeleza kuwa licha ya shule zote kutoa huduma ya Chakula,wapo baadhi ya Wazazi ambao hawachangii chakula kwaajili ya Watoto waojambo ambalo halikubaliki Aidha Munna ameongeza kuwa ili kukabiliana na changamo ya udumavu,ni lazima afua za lishe zisimamiwe kikamilifukuanzia ngazi za familia huku akisistiza viongozi kusimamia kwa Vitendo mafunzo yanayotolewa katika maadhimisho ya siku ya Afya ya Lishe ya Kijiji ‘’Hatuwezi kufikia malengo pasipo kwenda pamoja hivyo hao wazazi ambao hawajitolei katika uchangiaji wa huduma ya chakula wanakwenda kinyume hivyo elimu na usimamizi ni muhimu kwani wanaopata sh...

POLISI KIGOMA WAADHIMISHA WIKI YA POLISI JAMII KWA KUCHANGIA DAMU

Picha
  KIBONDO. Jehi la Polisi Mkoa wa Kigoma katika kuadhimisha wiki ya Polisi jamii, limefanya uafi na kuchangia Damu katika hospitali ya Wilaya ya Kibondoili kusaidia kuokoa maisha ya Watu wanaohitaji huduma hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma SACP Filemoni Makungu akiongea na Waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo, amesemalicha ya kupunguza uhitaji wa Damu katika vituo vya kutolea huduma za Afya,lengo kubwa ni kuonyesha ushiriki wa Jeshi   hilo katika masuala ya Kijamii Aidha Makungu ameongeza kuwa katika Wiki hii,zinafanyika shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na Michezo, Usafiri na kuchangia Damu ili kuokoa maisha ya wahitaji wa Damu Naye Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo Colnely Livin zoezi hilo linaonyesha namna Polisi linavyoshiriki katika utoaji wa huduma ndani ya Jamii Jumla ya Unit 36 za Damu zimepatikana katika zoezi hilo la uchangiaji Damu huku Jeshi hilo likiitaka jamii kuendelea kudumisha amani ambapo Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Col...

SIKU YA HOMA YA INI

Picha
  Kila ifikapo julai 28 kila mwaka Dunia uadhimisha siku ya homa kali ya Ini, lengo ikiwa ni kujenga uelewa kwenye jamii kuhusu tatizo hilo na namna ya kujihami na ili kuepukana na hali hiyo Homa ya Ini ni kuvimba kwa ini. Kitendo cha ini kuvimba ghafla   ndio huitwa Homa kali ya Ini. Sababu zinazofahamika zaidi za ini kuvimba ghafla ni maambukizi ya virusi vya homa ya ini aina A na E na ni katika matukio machache sana virusi vya homa ya Ini B na C. Aina fulani za dawa za matibabu ambazo zina sumu zinaweza pia kusababisha homa Kali ya ini. Mara nyingi inaweza kupona bila hata madhara makubwa au kuhitaji matibabu lakini katika matukio machache huweza kusababisha ini kushindwa kufanya kazi na wakati mwingine kifo. Na hizi ndizo dalili za homa kaliya Ini Bila kujali visababishi, dalili za homa kali ya ini ni pamoja na: -          Kutapika, kuhara au maumivu ya tumbo -          Rangi ya manjano kwenye macho na ngozi. -...

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SGR NA KUZINDUA MELI NNE ZA MIZIGO ZIWA TANGANYIKA

Picha
  Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alan Mvano Mbunge Jimbo la Kakonko Simon Siro Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Makame Mbalawa Waziri wa Uchukuzi Na Emmanueli Matinde,Kigoma Kigoma .Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amwesema serikali imeendelea na jitihada mbali mbali za kuimarisha miundombiu ya usafiri na usafirishaji nchini ikiwemo ujenzi wa Reli ya kisasa, uendelezaji wa bandari na ujenzi wa barabara na viwanja vya ndege. Dkt. Samia amesema hayo leo mkoani Kigoma mara baada ya kuzindua meli nne za mizigo ndani ya Ziwa Tanganyika, na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) Tabora – Kigoma, chenye urefu wa kilomita 506 kitakachojengwa kwa gharama ya Shilingi Trilioni 7.4. Amesema yote hayo yanafanyika kwa lengo la kuifungua nchi kibiashara na kiuwekezaji, kupunguza gharama za usafiri na usafirishaji na kurahisisha biadhaa kuyafikia masoko ya ndani na ya nje ya nchi. Kwa upande wake Waziri wa Uchukuzi P...

UWINDAJI HARAMU WASABABISHA IDADI SOKWE KUPUNGUA GOMBE

Picha
  Na Emmanuel Matinde Kigoma Idadi ya wanyama aina ya Sokwe katika Hifadhi ya Taifa ya Gombe iliyoko mkoani Kigoma, inaelezwa kupungua kwa kasi kutokana na kuwindwa, kuharibu maeneo yao ya asili, pamoja na shughuli za kibinadamu ambazo zinahatarisha maisha yao. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Utafiti wa Sokwe kutoka Taasisi ya JANEGOODALL (JGI), Dr. Deus Mjungu, huku akitoa wito kwa wadau wote kuona umuhimu wa kuwalinda Sokwe ili waweze kuongezeka.   Nchini Tanzania Sokwe, hupatikana katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi lakini kuongezeka kwa idadi ya watu na katika maeneo yaliyo karibu na makazi yao kunatajwa kutishia maisha yao amesema ShedrackKamenya Mhifadhi Mkuu Mstaafu toka Taasisi ya JGI.     Ikumbukwe kuwa wanyama aina ya Sokwe ambao tabia zake hufanana kwa asilimia 98% na binadamu, ni kivutio cha utalii kinachoiingizia serikali fedha za kigeni na kusaidia kukuza uchumi hivyo jamii ina jukumu la kushirikiana na serikali kuhakikisha wa...

MAHUNDI APONGEZA UWAJIBIKAJI KAKONKO ASHAURI WAONGEZE JUHUDI

Picha
  Na Cosmas Makala Kakonko Kakonko . Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi , amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Kakonko, mkoani Kigoma, ambapo alianza kwa kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kakonko. Katika kikao hicho, alipatiwa taarifa ya maendeleo ya Wilaya iliyowasilishwa na mkuu wa wilaya Col. Evance Mallasa ikieleza mafanikio yaliyopatikana pamoja na hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa manufaa ya wananchi. Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Mhe. Mahundi aliupongeza uongozi wa Wilaya ya Kakonko ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya,Col. Mallasa kwa usimamizi mzuri wa shughuli za maendeleo,Pia aliwapongeza Mh. Mbunge Alan Mvano, Katibu Tawala wa Wilaya Maulid Said Mtulia, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndaki Stephano Mhuli, kwa ushirikiano na ufanisi wanaouonyesha katika kusimamia utekelezaji wa mipango ya Serikali, jambo ambalo li...

SIKU YA UJUZI KWA VIJANA

Picha
Monica Mwita Mwanafunzi Veta Mwanza Voronica Gabriel Mkufunzi Veta Mwanza Flaviana Minda Kaimu Mkuu wa Chuo Veta Mwanza     Yapo naneno ya Wahenga yasemayo,Ushindi ni Mwenendo, Mwenendo huo ni Kazi, Kazi ni mawazo, mawazo ni kuelewa na imani, na hivyo kila kitu kinaanzia kwa   binadamu. Kuendana na maneno hayo,mnamo  2014, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilitangaza tarehe ya Julai 15 iwe siku ya Ujuzi wa Vijana Duniani, kuweka mikakati ya kuwaandaa vijana kwa ujuzi unaohitajiwa kuwaajiri na kuwawezesha kupata kazi licha ya kuwawezesha kwa Ujasiriamali.    Siku ya Kimataifa ya Ujuzi kwa Vijana huadhimishwa kila tarehe 15 Julai. Siku hii ilianzishwa na Umoja wa Mataifa ili kuhamasisha na kutambua umuhimu wa kuwapa vijana ujuzi na stadi mbalimbali za kazi ili waweze kujitegemea kimaisha na kuchangia maendeleo. Lengo kubwa ni kukumbusha jamii na serikali kutoa nafasi za mafunzo zitakazowawezesha vijana kupata ujuzi unaohitajika katika soko la ajira, has...