Machapisho

SIKU YA HOMA YA INI

Picha
  Kila ifikapo julai 28 kila mwaka Dunia uadhimisha siku ya homa kali ya Ini, lengo ikiwa ni kujenga uelewa kwenye jamii kuhusu tatizo hilo na namna ya kujihami na ili kuepukana na hali hiyo Homa ya Ini ni kuvimba kwa ini. Kitendo cha ini kuvimba ghafla   ndio huitwa Homa kali ya Ini. Sababu zinazofahamika zaidi za ini kuvimba ghafla ni maambukizi ya virusi vya homa ya ini aina A na E na ni katika matukio machache sana virusi vya homa ya Ini B na C. Aina fulani za dawa za matibabu ambazo zina sumu zinaweza pia kusababisha homa Kali ya ini. Mara nyingi inaweza kupona bila hata madhara makubwa au kuhitaji matibabu lakini katika matukio machache huweza kusababisha ini kushindwa kufanya kazi na wakati mwingine kifo. Na hizi ndizo dalili za homa kaliya Ini Bila kujali visababishi, dalili za homa kali ya ini ni pamoja na: -          Kutapika, kuhara au maumivu ya tumbo -          Rangi ya manjano kwenye macho na ngozi. -...

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SGR NA KUZINDUA MELI NNE ZA MIZIGO ZIWA TANGANYIKA

Picha
  Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alan Mvano Mbunge Jimbo la Kakonko Simon Siro Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Makame Mbalawa Waziri wa Uchukuzi Na Emmanueli Matinde,Kigoma Kigoma .Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amwesema serikali imeendelea na jitihada mbali mbali za kuimarisha miundombiu ya usafiri na usafirishaji nchini ikiwemo ujenzi wa Reli ya kisasa, uendelezaji wa bandari na ujenzi wa barabara na viwanja vya ndege. Dkt. Samia amesema hayo leo mkoani Kigoma mara baada ya kuzindua meli nne za mizigo ndani ya Ziwa Tanganyika, na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) Tabora – Kigoma, chenye urefu wa kilomita 506 kitakachojengwa kwa gharama ya Shilingi Trilioni 7.4. Amesema yote hayo yanafanyika kwa lengo la kuifungua nchi kibiashara na kiuwekezaji, kupunguza gharama za usafiri na usafirishaji na kurahisisha biadhaa kuyafikia masoko ya ndani na ya nje ya nchi. Kwa upande wake Waziri wa Uchukuzi P...

UWINDAJI HARAMU WASABABISHA IDADI SOKWE KUPUNGUA GOMBE

Picha
  Na Emmanuel Matinde Kigoma Idadi ya wanyama aina ya Sokwe katika Hifadhi ya Taifa ya Gombe iliyoko mkoani Kigoma, inaelezwa kupungua kwa kasi kutokana na kuwindwa, kuharibu maeneo yao ya asili, pamoja na shughuli za kibinadamu ambazo zinahatarisha maisha yao. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Utafiti wa Sokwe kutoka Taasisi ya JANEGOODALL (JGI), Dr. Deus Mjungu, huku akitoa wito kwa wadau wote kuona umuhimu wa kuwalinda Sokwe ili waweze kuongezeka.   Nchini Tanzania Sokwe, hupatikana katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi lakini kuongezeka kwa idadi ya watu na katika maeneo yaliyo karibu na makazi yao kunatajwa kutishia maisha yao amesema ShedrackKamenya Mhifadhi Mkuu Mstaafu toka Taasisi ya JGI.     Ikumbukwe kuwa wanyama aina ya Sokwe ambao tabia zake hufanana kwa asilimia 98% na binadamu, ni kivutio cha utalii kinachoiingizia serikali fedha za kigeni na kusaidia kukuza uchumi hivyo jamii ina jukumu la kushirikiana na serikali kuhakikisha wa...

MAHUNDI APONGEZA UWAJIBIKAJI KAKONKO ASHAURI WAONGEZE JUHUDI

Picha
  Na Cosmas Makala Kakonko Kakonko . Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi , amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Kakonko, mkoani Kigoma, ambapo alianza kwa kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kakonko. Katika kikao hicho, alipatiwa taarifa ya maendeleo ya Wilaya iliyowasilishwa na mkuu wa wilaya Col. Evance Mallasa ikieleza mafanikio yaliyopatikana pamoja na hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa manufaa ya wananchi. Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Mhe. Mahundi aliupongeza uongozi wa Wilaya ya Kakonko ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya,Col. Mallasa kwa usimamizi mzuri wa shughuli za maendeleo,Pia aliwapongeza Mh. Mbunge Alan Mvano, Katibu Tawala wa Wilaya Maulid Said Mtulia, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndaki Stephano Mhuli, kwa ushirikiano na ufanisi wanaouonyesha katika kusimamia utekelezaji wa mipango ya Serikali, jambo ambalo li...

SIKU YA UJUZI KWA VIJANA

Picha
Monica Mwita Mwanafunzi Veta Mwanza Voronica Gabriel Mkufunzi Veta Mwanza Flaviana Minda Kaimu Mkuu wa Chuo Veta Mwanza     Yapo naneno ya Wahenga yasemayo,Ushindi ni Mwenendo, Mwenendo huo ni Kazi, Kazi ni mawazo, mawazo ni kuelewa na imani, na hivyo kila kitu kinaanzia kwa   binadamu. Kuendana na maneno hayo,mnamo  2014, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilitangaza tarehe ya Julai 15 iwe siku ya Ujuzi wa Vijana Duniani, kuweka mikakati ya kuwaandaa vijana kwa ujuzi unaohitajiwa kuwaajiri na kuwawezesha kupata kazi licha ya kuwawezesha kwa Ujasiriamali.    Siku ya Kimataifa ya Ujuzi kwa Vijana huadhimishwa kila tarehe 15 Julai. Siku hii ilianzishwa na Umoja wa Mataifa ili kuhamasisha na kutambua umuhimu wa kuwapa vijana ujuzi na stadi mbalimbali za kazi ili waweze kujitegemea kimaisha na kuchangia maendeleo. Lengo kubwa ni kukumbusha jamii na serikali kutoa nafasi za mafunzo zitakazowawezesha vijana kupata ujuzi unaohitajika katika soko la ajira, has...

KIBONDO YAENDELEZA UDHIBITI UGONJWA EBOLA

Picha
  DktSimon Omary  Mratibu huduma za Afya Wilaya ya Kibondo Fiboreen Siwale Mratibu wa Maralia Wilaya ya Kibondo Aggrey Magwaza Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Mkuu wa wilaya ya kibondo Mkoani Kigoma, kanali Mstaafu   Agery Magwaza amewaagiza wataalamu wa afya kuendelea kufanya tafiti za kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa maralia kutokana na ugonjwa huo kutodhibitiwa kwa ufasaha na kuendelea kuleta athari kwa jamii Amebainisha   hayo wakati wa kikao Cha kamati ya afya ya msingi ya Wilaya, walipokua wakijadili namna ya kudhibiti ugonjwa huo ambapo amesema maambukizi ya ugonjwa yamekua yakisababisha madhara kwa jamii kutokana na mbu wannasambaza vimelea hivyo vya   malaria kushidwa kudhibitiwa ipasavyo   Aidha katika kikao hicho kilijadili namna ya kukabiliana na ugonjwa wa ebola ndani ya wilaya ya kibondo huku mkuu huyo wa wilaya akwahimiza wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo ikizingatiwa Wilaya hiyo iko mpakani mwa nchi,   Ili usien...

ONGEZEKO LA IDADI YA WATU NI TATIZO LA KIMATAIFA

Picha
  Ongezeko la idadi ya watu Duniani, ni tatizo la kimataifa na na linatajwa kusababisha changamoto mbalimbali za Kibinadamu japo uwepo wa Binadamu katika uso wa Dunia ni jambo la muhimu Kwa mujibu wa makadirio ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa kupitia Divisheni ya Idadi ya Watu ya UN (UN DESA Population Division), ni kwamba   kufikia mwezi Julai 2025, dunia ilikadiriwa kuwa na zaidi ya watu bilioni 8.1. Nchi zenye Idadikubwa   ya Watu Duniani ni   ni China na India   ambapo katika Nchi ya India kuna Watu wapatao 1,339,180,127 na China ikiwa na Idadi ya Watu 1,409,517,397 huku Bara la Afrika likiwa na Watu billion 1.58 Kila uchao Wanadamu wamekuwa wakiongezeka kwa kasi huku Dunia ikiwa pale pale na mahitaji ya lazima   ya kibindamu kama ardhi   vikiwa haviongezeki   na huduma za Afya, Maji, Chakula na makazi,   upatikanaji wake ukiwa ngumu na kuufanya ulimwengu kuwa katika hali ya hatari ya kukumbwa na Majanga ya Kibinadamu Kutok...