Viongozi wa Vijiji na Kata simamien na kutoa elimu umuhimu wa Lishe
Kibondo. Viongozi wa Kata na Vijiji wamehaswakuendelea kuhamasisha umuhimu wa Lishe na mpangilio wa matumizi ya vyakula kwa Watoto na watu rika zote ukiwemouchangiaji wa chakula Mashuleni ili kupunguza udumavu na kuinua kiwango cha Elimu Amebainishahayo Afisa Lishe Wilaya ya Kibondo Tumaini Muna wakati wa kujadili ripoti ya utekelezaji afua za Lishe kwa robo yanne 2025/26 ambapo ameeleza kuwa licha ya shule zote kutoa huduma ya Chakula,wapo baadhi ya Wazazi ambao hawachangii chakula kwaajili ya Watoto waojambo ambalo halikubaliki Aidha Munna ameongeza kuwa ili kukabiliana na changamo ya udumavu,ni lazima afua za lishe zisimamiwe kikamilifukuanzia ngazi za familia huku akisistiza viongozi kusimamia kwa Vitendo mafunzo yanayotolewa katika maadhimisho ya siku ya Afya ya Lishe ya Kijiji ‘’Hatuwezi kufikia malengo pasipo kwenda pamoja hivyo hao wazazi ambao hawajitolei katika uchangiaji wa huduma ya chakula wanakwenda kinyume hivyo elimu na usimamizi ni muhimu kwani wanaopata sh...