MANISPAA YA ILEMELA YAENDELEZA MPANGO WA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI KWA KUTOA TSH 625 KWA ROBO YA TATU 2026 10% MAKUNDI MAALUM
Watu milioni 800 duniani wanatajwa kuishi katika umaskini uliokithiri na aina nyingi za umaskini zinasababishwa na kuongezeka kwa idadi ya watu wasio na ajira ajenda ya Umoja wa Mataifa ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030, ambayo yameliweka suala la kupambana na umaskini kama lengo kuu kuzishauri nchi zote kuutokomeza umaskini Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, siku ya kupambana na umaskini inaadhimishwa kwa kuzingatia wito uliotolewa miaka 25 iliyopita ya kutambua ujuzi na ujasiri wa familia zinazoishi katika umaskini duniani kote, umuhimu wa kuwafikia Watu maskini na kuwawezesha kiuchumi Tanzania ni moja ya nchi Duniani ambayo inaendelea Mikakati ya kupambana na umasikini kwa kuwawezesha Wananchi kiuchumi ,kutokana na hatua hiyo, Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza imeendeleza mpango huo ambapo katika robo ya tatu 2026 Vikundi 41 Vimepatiwa Mikopo ya 10% amebainisha Kaimu Afisa Maendeleoa Manispaa hiyo Yusuph Okoko wakati wa hafla ya utoaji hudi ...