ALATI MKOA WA KIGOMA WAKAGUA MIRADI KIBONDO
Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania ALATI Mkoa wa Kigoma imeishauri Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma kuboresha mazingira ya ujifunzaji kwa Wanafunzi wa Chuo cha Maafisa Matabibu kinachomilikiwa na Halmashauri hiyo Wametoa ushauri huo Wajumbe wa Jumuiya hiyo wakiwa kwenye ziara ya kutembelea na kukagua Miradi ambapo wameeleza kulingana na uhimu wa sekta ya afya ni vema uboreshajiwa miundombinu katika chuo hicho ufanyike haraka iwezekanavyo Hatua hiyo imekuja baada ya kupokea taarifa ya namna chuo hicho kinavyoendeshwa na kutoa huduma ambapo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibondo Diocles Lutema ameeleza kwakuwa chuo hicho kinamilikiwa na serikali wanafuata miongozo Miradi iliyotembelewa na Jumuiya hiyo ni Ujenzi wa Soko la Kisasa, Chuo cha maafisa Tabibu, Jengo la Ofisi za Halmashauri ya Kibondo na Vibanda vya Biashara, huku baadhi ya ambao ni Lugendo Elias na Anthon Kiteleriwajumbe hao wakipongeza ujenzi wa Miradi hiyo huku nae Mwenyekiti wa H...