"UJENZI WA MELI MPYA NA CHELEZO KIGOMA KUFUNGUA SOKO LA BIASHARA KIMATAIFA" WAZIRI MBARAWA
"UJENZI WA MELI MPYA NA CHELEZO KIGOMA KUFUNGUA SOKO LA BIASHARA KIMATAIFA" WAZIRI MBARAWA Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema uwekezaji wa kampuni ya kizawa ya Dar es Salaam Merchant Group katika ujenzi wa chelezo na meli mpya mkoani Kigoma utaongeza uwezo wa Tanzania kujenga na kukarabati meli nchini, huku ukifungua fursa za biashara na huduma za ujenzi wa meli kwa nchi zinazozunguka Ziwa Tanganyika, ikiwemo DRC na Zambia Prof. Mbarawa ameyasema hayo baada ya kukagua eneo la Bulombora Mkoani Kigoma linalojengwa chelezo cha kampuni hiyo, akisema Serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kushiriki katika uwekezaji wa miundombinu na huduma za usafiri wa njia ya maji hatua ambayo itaongeza uwezo wa wazawa katika ujenzi na ukarabati wa vyombo vinavyosafiri kwa njia ya maji Amesema kampuni hiyo, iliyoshiriki katika ujenzi na ukarabati wa meli ikiwemo MV Liemba, imeanza maandalizi ya ujenzi wa meli mpya yenye uwezo wa...