RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SGR NA KUZINDUA MELI NNE ZA MIZIGO ZIWA TANGANYIKA
Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alan Mvano Mbunge Jimbo la Kakonko Simon Siro Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Makame Mbalawa Waziri wa Uchukuzi Na Emmanueli Matinde,Kigoma Kigoma .Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amwesema serikali imeendelea na jitihada mbali mbali za kuimarisha miundombiu ya usafiri na usafirishaji nchini ikiwemo ujenzi wa Reli ya kisasa, uendelezaji wa bandari na ujenzi wa barabara na viwanja vya ndege. Dkt. Samia amesema hayo leo mkoani Kigoma mara baada ya kuzindua meli nne za mizigo ndani ya Ziwa Tanganyika, na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) Tabora – Kigoma, chenye urefu wa kilomita 506 kitakachojengwa kwa gharama ya Shilingi Trilioni 7.4. Amesema yote hayo yanafanyika kwa lengo la kuifungua nchi kibiashara na kiuwekezaji, kupunguza gharama za usafiri na usafirishaji na kurahisisha biadhaa kuyafikia masoko ya ndani na ya nje ya nchi. Kwa upande wake Waziri wa Uchukuzi P...