WATUMISHI SITA IDARA YA AFYA MKOANI KIGOMA WAMEKUFA MAJI ZIWA TANGANYIKA
Watu sita ambao ni watumishi wa idara ya afya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wamethibtika kufa, watatu wakiwa bado hawajapatikana wengine tisa wakiokolewa wakiwa hai baada ya boti waliokuwa wanasafiria kuzama katika Ziwa Tanganyika katika Kijiji cha Kalalangabo wilayani humo. Akithibitisha vifo hivyo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Balozi Simon Sirro, amesema tukio hilo limetokea mapema leo Ijumaa Machi 13, 2026 asubuhi, wakati watumishi hao wakisafiri kwenda kijiji cha Kagunga kwa ajili ya kutoa chanjo kabla ya boti yao kupigwa na dhoruba kufuatia upepo mkali na kupinduka. Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kigoma, Mrakibu Msaidizi Michael Maganga, amesema zoezi la kuwatafuta watu watatu watumishi wa idara ya afya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, miongoni mwa waliopinduka na boti katika Ziwa Tanganyika eneo la Kalalangabo bado linaendelea. Aidha Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Kigoma ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Mkuu wa Wilaya hiyo, imepiga ka...