Mabadiliko ya Ongezekola Idadi kubwa ya Wanafunzi 2027, Mikakati iongezeke ujenzi wa Miundo mbinu
Mwanza. Kutokana na mabadiliko ya Mitaala ya Elimu katika shule za Msingi na Sekondari hapa nchini, hatua itakayopelekea Wanafunzi wengi kumaliza elimu ya Msingi kuelekea sekondari, serikali imeshauliwa kulitazamaa kwa jicho la pekee suala la ujenzi na uanzishwaji wa shule za sekondari ili kuleta tija Darasa la saba na sita ni makundi yanayotarajiwa kumaliza elimu hiyo huku idadi ya shule na vyumba vya madarasa vikiwa ni vichache hatua inayotajwa kuwa huenda ikakwamisha malengo mahususi Hayo yameelezwa na Madiwani wa Halmashauri ya Magu Mkoani mwanza walipokuwa wakijadili Bajeti ya Halmashauri hiyo ya 2026/27ambapo John Ngagaje Diwani Kata ya Shisha na Jackson LugwishaKata ya Lutale wanasema kuwa ni vema pia bajeti hiyo ikajielekeza kunusulu sekta ya elimu hasa kwenye miundombinu Awali akisoma taarifa ya rasmu ya Bajeti hiyo Afisa Mipango wa Halmashauri ya Magu Mofeni Mwakajonga amesema Bajeti hiyo imetia hatua zote za kisheria na ...