Machapisho

WATUMISHI SITA IDARA YA AFYA MKOANI KIGOMA WAMEKUFA MAJI ZIWA TANGANYIKA

Picha
  Watu sita ambao ni watumishi wa idara ya afya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wamethibtika kufa, watatu wakiwa bado hawajapatikana wengine tisa wakiokolewa wakiwa hai baada ya boti waliokuwa wanasafiria kuzama katika Ziwa Tanganyika katika Kijiji cha Kalalangabo wilayani humo. Akithibitisha vifo hivyo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Balozi Simon Sirro, amesema tukio hilo limetokea mapema leo Ijumaa Machi 13, 2026 asubuhi, wakati watumishi hao wakisafiri kwenda kijiji cha Kagunga kwa ajili ya kutoa chanjo kabla ya boti yao kupigwa na dhoruba kufuatia upepo mkali na kupinduka. Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kigoma, Mrakibu Msaidizi Michael Maganga, amesema zoezi la kuwatafuta watu watatu watumishi wa idara ya afya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, miongoni mwa waliopinduka na boti katika Ziwa Tanganyika eneo la Kalalangabo bado linaendelea. Aidha Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Kigoma ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Mkuu wa Wilaya hiyo, imepiga ka...

Magu yapunguza vifo vitokanavyo na uzazi asilimia 70 kwa miaka mitano

Picha
  Mwanza . Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza imefanikiwa kupunguza Vifo vitokanavyo na uzazi   kutoka vifo 112 hadi 42 katika kipindi cha miaka mitano baada ya serikali kuboresha huduma kwa kutoa vifaa na kuongeza miundombinu ya majengo Voronica Gibson Mkazi wa Magu Hellen Chizere Muuguzi mfawidhi Hospitali ya Wilaya ya Magu Raphaem Mhana Mganga Mkuu W ya Magu Raphael Mhana Mganga Mkuu Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza ameeleza kipindi cha2015hadi 2020,   hali ilikuwa hairidhishi ikilinganishwa na takwimu kuanzia 2020 hadi 2025   baada ya kufanyika   maboresho katika sekta ya Afya Hata hivyo Mhana amesema kutokana na maboresho hayo kwa sasa wanatengeza na Miguu bandia ambayo inasaidia Watu wanaopata matatizo mbalimbali zikiwemo ajali ‘’Wagonjwa wenye Matatizo ya Viungo hasa Miguu walemavu wa kuzaliwa na wanaokuwa wamepata ajali katika Wilaya ya Magu na maeneo ya jirani,wamekuwa wakisafiri kwenda mbali kutafuta huduma ya Miguu bandia lakini kwa hivi sasa   baada...

Shukran kwa wanaosaidia katika Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Picha
  Viongozi wa Dini ya Kiislam mkoani Kigoma wamepongeza taasisi na watu binafsi wanaojitokeza na kutoa sadaka ya Iftar kwa waislam waliofunga kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Hayo yamejiri wakati Taasisi ya The Islamic Foundation ilipotoa sadaka ya Futari pamoja na chakula cha daku, kwa waislam waliofunga katika Manispaa ya Kigoma Ujiji kama sehemu ya kuimarisha funga zao. Viongozi hao wakiwemo Macho Hamisi Feruz, Sheikh wa Kata ya Gungu katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Sheikh Bazir Ismail, Naibu Amir Mkoa wa Kigoma Jamaat Answer Suna, wamesema hatua hiyo inawatia nguvu waislam kuendelea na funga yao kwa furaha na usalama. Baadhi ya waislam waliopokea zawadi hizo ambazo zinajumuisha mchele, sukari, mafuta na tende, wameishukuru Taasisi ya The Islamic Foundation, na kuiombea izidi kudumu ili iweze kugusa maisha ya watu wengi zaidi katika shughuli zake za kuhudumia jamii.  

Watendaji ongezeni jitiada elimu na hamasa masuala ya Lishe

Picha
  Tumain Munna Afisa Lishe Wilaya ya Kibondo Halima Madenge Mshiriki Mkuu wa wilaya ya Kibondo kanali Mstaafu agrey magwaza amewataka watendaji wa kata kuhakikisha wanasimamia zoezi la wazazi kuchangia chakula mashuleni Hali ambayo itaongeza hamasa ya watoto kuelewa kile wanachojifunza na kuwafanya kuwa na afya bora Ameyasema hayo wakati wa  kujadili taarifa ya Hali ya lishe Kwa watoto katika kipindi Cha robo ya tatu ya October hadi December ambapo amesema Kila mzazi anatakiwa aone umuhimu wa kuchangia chakula kwaajili ya watoto ili waweze kufikia malengo yaliyokusudiwa Aidha  agrey amewataka walimu kutumia maeneo ya yaliyo wazi kwaajili ya kilimo na kuzalisha chakula ambacho kitasaidia kuendelea kuboresha afya za wanafunzi Hali ambayo itasaisaidia pia kupunguza wingi wa michango ya chakula Kutoka Kwa wazazi Fundi Hamisi Mtendaji Kata ya Kitahana na Marushwa Marushwa Mtendaji Kata ya Lugongwe wameahidi kuendelea kufanya utekelezaji hasa katika kuhamasisha na kuelimi...

Mkoani Kigoma,Serikali ya Wadau kuendelea kuboresha huduma zaAfya

Picha
  Serikali kwa kushirikiana na wadau wameendelea kupiga hatua muhimu kuelekea kufikia malengo endelevu ya mwaka 2030 ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kufikia vifo 70 kwa vizazi hai laki moja na vifo vya watoto wachanga kufikia vifo 12 katika vizazi hai elfu moja. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid Chuachua kwenye uzinduzi wa mradi wa Mjamzito na Mtoto Salama utakaotekelezwa na Shirika la Thamini Uhai, ukilenga kuchangia katika juhudi za serikali za kupunguza vifo vya uzazi na watoto wachanga. Amesema hatua hizo ni pamoja na kuboresha na kuimarisha miundombinu pamoja na vifaa tiba kwenye sekta ya afya, na kwamba juhudi zinazofanywa na wadau kama vile Shirika la Thamini Uhai ni muhimu katika kufikia malengo hayo. Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Joachim Masunga, amesema kupitia mradi wa Mjamzito na Mtoto Salama, utaleta tija kubwa kwenye jitihada za kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi. ...

ILEMELA KUENDELEA KUIMARISHA MTANDAO WA BARABARA

Picha
  Moja ya eneo la Barabara zinazojengwa na Tarura Kiwango cha Lami Kagua Nyamhongo Mwanza Stephan Malimi  Bahati Ezekiel Mwananchi Sobe Makonyo Meneja wa Tarura Wilaya ya Ilemela Ujenzi wa Barabara   za Busweru Busenga km 3 na Buswelu Kagua hadi Barabara kuu ya Mwanza Musoma kilomita 9 ni moja ya hatua ambazo zimesaidia kuondoa changamoto ya mawasiliano ya maeneo tofauti   na kurahisha usafiri kwa Wananchi Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza Baadhi ya Wakazi Wakagua, wameeleza kuwa awali wamekuwa wakipata shida kubwa ya kusafirisha wagonjwa kwenda hospitali wakati mwingine vilitokea vifo kwa watumiaji wa vyombo vya Moto kutokana na ubovu wa Barabara Wananchi haoStephan Malimi na Bahati Ezekiel   wameeleza kwa kuipongeza serikali hatua hiyo ya ujenzi wa Barabara kilomita 9 kwa kiwango cha Lami, kwani kwa sasa yapo mawasiliano ya karibu na haraka na maeneo ya Nyamadoke na Nyamhongolo Barabara kuu ya Mwanza Musoma, japo ni eneo dogo lakini siku za nyuma walipata adh...

Wadau wa Elimu kusaidia vifaa kwa Wanafunzi kuongeza chachu ya ujifunzaji

Picha
   Ukosefu wa vifaa muhimu vya shule kama vile madaftari na kalamu umetajwa kuathiri pakubwa maendeleo ya wanafunzi wa shule za msingi katika Kata ya Kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji na kupelekea wengi kushindwa kuendelea na masomo. Hayo yameelezwa na Afisa Elimu Kata ya Kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji Gaston Mwanache, wakati wa hafla ya kutoa zawadi ya vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule za msingi Bushabani na Kibirizi waliofanya vizuri katika masomo yao mwaka uliopita 2025. Amesema ukosefu wa vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule za msingi katika kata hiyo ni changamoto kubwa inayotokana na hali duni za baadhi ya familia na baadhi ya wazazi kutowajibika ipasavyo katika malezi ya watoto wao kwa kuwaacha wakilelewa na bibi zao. Kwa upande mwingine badhi ya   walimu wa shule za msingi Bushabani na Kibirizi wamewapongeza wadau wa elimu wakiwemo Taasisi ya Kigoma Elimu Foundation kwa kutoa zawadi kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo yao, wakieleza hatua...