Machapisho

Shukran kwa wanaosaidia katika Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Picha
  Viongozi wa Dini ya Kiislam mkoani Kigoma wamepongeza taasisi na watu binafsi wanaojitokeza na kutoa sadaka ya Iftar kwa waislam waliofunga kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Hayo yamejiri wakati Taasisi ya The Islamic Foundation ilipotoa sadaka ya Futari pamoja na chakula cha daku, kwa waislam waliofunga katika Manispaa ya Kigoma Ujiji kama sehemu ya kuimarisha funga zao. Viongozi hao wakiwemo Macho Hamisi Feruz, Sheikh wa Kata ya Gungu katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Sheikh Bazir Ismail, Naibu Amir Mkoa wa Kigoma Jamaat Answer Suna, wamesema hatua hiyo inawatia nguvu waislam kuendelea na funga yao kwa furaha na usalama. Baadhi ya waislam waliopokea zawadi hizo ambazo zinajumuisha mchele, sukari, mafuta na tende, wameishukuru Taasisi ya The Islamic Foundation, na kuiombea izidi kudumu ili iweze kugusa maisha ya watu wengi zaidi katika shughuli zake za kuhudumia jamii.  

Watendaji ongezeni jitiada elimu na hamasa masuala ya Lishe

Picha
  Tumain Munna Afisa Lishe Wilaya ya Kibondo Halima Madenge Mshiriki Mkuu wa wilaya ya Kibondo kanali Mstaafu agrey magwaza amewataka watendaji wa kata kuhakikisha wanasimamia zoezi la wazazi kuchangia chakula mashuleni Hali ambayo itaongeza hamasa ya watoto kuelewa kile wanachojifunza na kuwafanya kuwa na afya bora Ameyasema hayo wakati wa  kujadili taarifa ya Hali ya lishe Kwa watoto katika kipindi Cha robo ya tatu ya October hadi December ambapo amesema Kila mzazi anatakiwa aone umuhimu wa kuchangia chakula kwaajili ya watoto ili waweze kufikia malengo yaliyokusudiwa Aidha  agrey amewataka walimu kutumia maeneo ya yaliyo wazi kwaajili ya kilimo na kuzalisha chakula ambacho kitasaidia kuendelea kuboresha afya za wanafunzi Hali ambayo itasaisaidia pia kupunguza wingi wa michango ya chakula Kutoka Kwa wazazi Fundi Hamisi Mtendaji Kata ya Kitahana na Marushwa Marushwa Mtendaji Kata ya Lugongwe wameahidi kuendelea kufanya utekelezaji hasa katika kuhamasisha na kuelimi...

Mkoani Kigoma,Serikali ya Wadau kuendelea kuboresha huduma zaAfya

Picha
  Serikali kwa kushirikiana na wadau wameendelea kupiga hatua muhimu kuelekea kufikia malengo endelevu ya mwaka 2030 ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kufikia vifo 70 kwa vizazi hai laki moja na vifo vya watoto wachanga kufikia vifo 12 katika vizazi hai elfu moja. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid Chuachua kwenye uzinduzi wa mradi wa Mjamzito na Mtoto Salama utakaotekelezwa na Shirika la Thamini Uhai, ukilenga kuchangia katika juhudi za serikali za kupunguza vifo vya uzazi na watoto wachanga. Amesema hatua hizo ni pamoja na kuboresha na kuimarisha miundombinu pamoja na vifaa tiba kwenye sekta ya afya, na kwamba juhudi zinazofanywa na wadau kama vile Shirika la Thamini Uhai ni muhimu katika kufikia malengo hayo. Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Joachim Masunga, amesema kupitia mradi wa Mjamzito na Mtoto Salama, utaleta tija kubwa kwenye jitihada za kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi. ...

ILEMELA KUENDELEA KUIMARISHA MTANDAO WA BARABARA

Picha
  Moja ya eneo la Barabara zinazojengwa na Tarura Kiwango cha Lami Kagua Nyamhongo Mwanza Stephan Malimi  Bahati Ezekiel Mwananchi Sobe Makonyo Meneja wa Tarura Wilaya ya Ilemela Ujenzi wa Barabara   za Busweru Busenga km 3 na Buswelu Kagua hadi Barabara kuu ya Mwanza Musoma kilomita 9 ni moja ya hatua ambazo zimesaidia kuondoa changamoto ya mawasiliano ya maeneo tofauti   na kurahisha usafiri kwa Wananchi Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza Baadhi ya Wakazi Wakagua, wameeleza kuwa awali wamekuwa wakipata shida kubwa ya kusafirisha wagonjwa kwenda hospitali wakati mwingine vilitokea vifo kwa watumiaji wa vyombo vya Moto kutokana na ubovu wa Barabara Wananchi haoStephan Malimi na Bahati Ezekiel   wameeleza kwa kuipongeza serikali hatua hiyo ya ujenzi wa Barabara kilomita 9 kwa kiwango cha Lami, kwani kwa sasa yapo mawasiliano ya karibu na haraka na maeneo ya Nyamadoke na Nyamhongolo Barabara kuu ya Mwanza Musoma, japo ni eneo dogo lakini siku za nyuma walipata adh...

Wadau wa Elimu kusaidia vifaa kwa Wanafunzi kuongeza chachu ya ujifunzaji

Picha
   Ukosefu wa vifaa muhimu vya shule kama vile madaftari na kalamu umetajwa kuathiri pakubwa maendeleo ya wanafunzi wa shule za msingi katika Kata ya Kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji na kupelekea wengi kushindwa kuendelea na masomo. Hayo yameelezwa na Afisa Elimu Kata ya Kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji Gaston Mwanache, wakati wa hafla ya kutoa zawadi ya vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule za msingi Bushabani na Kibirizi waliofanya vizuri katika masomo yao mwaka uliopita 2025. Amesema ukosefu wa vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule za msingi katika kata hiyo ni changamoto kubwa inayotokana na hali duni za baadhi ya familia na baadhi ya wazazi kutowajibika ipasavyo katika malezi ya watoto wao kwa kuwaacha wakilelewa na bibi zao. Kwa upande mwingine badhi ya   walimu wa shule za msingi Bushabani na Kibirizi wamewapongeza wadau wa elimu wakiwemo Taasisi ya Kigoma Elimu Foundation kwa kutoa zawadi kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo yao, wakieleza hatua...

2,352 Walioacha Masomo Mkoani Kigoma kureshwa Mashuleni

Picha
  Farida Sebalua Afisa Elimu UNICEF Kigoma Simon Siro Mkuu wa Kigoma Kigoma . Mkoa wa Kigoma kupitia mradi wa Elimisha Mtoto umefanikiwa kuwarejesha shuleni watoto 2,352 waliokuwa wameacha shule kupitia mfumo rasmi au nje ya mfumo rasmi. Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, kwenye kikao cha kuendeleza kampeni ya kuhimiza uandikishaji na kuwarejesha watoto walio nje ya shule iliyozinduliwa Desemba   mwaka 2025. Balozi Sirro, amesema kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2026 bado wapo watoto wenye umri wa kati ya miaka 6 na 15 ambao hawajaandikishwa shuleni katika mfumo rasmi au nje ya mfumo rasmi wa shule na kwamba serikali kwa ushirikiano na Shirika la Kuhudumia Watoto Duniani UNICEF na wadau wengine inalenga kuwandikisha watoto wote ambao hawajaandikishwa na kuwarejesha walioacha masomo kutokana na sababu mbali mbali. Kwa upande wake Afisa Elimu kutoka UNICEF, Ofisi ya Kigoma Farida Sebalua, amesema tafiti zinaonyesha kuwa mkoa wa Kigoma unakabiliwa n...

Mabadiliko ya Ongezekola Idadi kubwa ya Wanafunzi 2027, Mikakati iongezeke ujenzi wa Miundo mbinu

Picha
  Mwanza. Kutokana na mabadiliko ya Mitaala ya Elimu katika shule za Msingi na Sekondari hapa nchini, hatua itakayopelekea Wanafunzi wengi kumaliza elimu ya Msingi kuelekea sekondari, serikali imeshauliwa kulitazamaa kwa jicho la pekee suala la ujenzi na uanzishwaji wa shule za sekondari ili kuleta tija Darasa la saba na sita ni makundi yanayotarajiwa kumaliza elimu hiyo huku idadi ya shule na vyumba vya madarasa vikiwa ni vichache hatua inayotajwa kuwa huenda ikakwamisha malengo mahususi Hayo yameelezwa na   Madiwani wa Halmashauri ya Magu Mkoani mwanza walipokuwa wakijadili Bajeti ya Halmashauri hiyo ya 2026/27ambapo   John Ngagaje Diwani Kata ya Shisha   na Jackson   LugwishaKata ya Lutale wanasema   kuwa ni vema pia bajeti hiyo ikajielekeza kunusulu sekta ya elimu   hasa kwenye miundombinu Awali akisoma taarifa ya rasmu ya Bajeti hiyo Afisa Mipango wa Halmashauri ya Magu Mofeni Mwakajonga amesema Bajeti hiyo imetia hatua zote za kisheria na ...