Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2023

KAMATI YAITAKA TANROADS KUZINGATIA VIPENGELE VYA GHARAMA KWENYE MIRADI

Picha
 KAMATI YAITAKA TANROADS KUZINGATIA VIPENGELE VYA GHARAMA KWENYE MIRADI Na Mwandishi Wetu Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeiagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kuhakikisha wanaingia mikataba ya ujenzi yenye gharama isiyokuwa na nyongeza za fedha. Imesema wakandarasi wengi  wanaoingia mikataba ya ujenzi na Tanroads wanakuja na mfumo wa nyongeza za gharama hali inayoisababishia serikali gharama zisizokuwa na tija. Mwenyekiti wa kamati hiyo, Seleman Kakoso alitoa maagizo hayo jana jijini Dar es Salaam wakati kamati hiyo ilipotembelea na kukagua ujenzi wa miundombinu ya mradi wa Dart awamu ya pili eneo la Mbagala. "Serikali imetoa fedha nyingi katika ujenzi wa mradi huu. Jitihada ni nzuri zimefanyika, tumeridhika na kwa sasa kuna maendeleo. Lakini igeni mfumo wa TRC katika ujenzi wa barabara. Wakandarasi wanakuja na mfumo wa nyongeza za gharama hali inayosababisha miradi kuwa na gharama kubwa," alisema Kakoso. Mbali na kutoa agizo hilo, kamati hiyo iliagiza Ta

MTABILA YAONGEZA UZALISHAJI

Picha
  Kasulu. Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa JKT Mtabila kilichopo Wilayani Kasulu mkoani Kigoma, kimefanikiwa kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo bustani na ufugaji, na kuwezesha vijana wanaopata mafunzo ya Kijeshi kikosini hapo,  kuwa na uwezo wa kujitegemea kutafuta fursa za kujiajili kupitia kilimo.  Katika mahafari ya kuhitimu mafunzo ya Jeshi Oparesheni  Jenerali Venance Mabeyo, Ambapo  baadhi ya vijana Julias Masuna Jesca Jeremia  jana wamesema stadi za maisha wanazofundishwa kikosini humo, zimewawezesha kuongeza uzalishaji wa mazao. ''Nilifika hapa Kikosini 825 nikiwa sifahamu mambo mengi yahusuyo maisha hasa katika masuala ya maendeleo na kujituma hasa katika sekta ya kilimo ila nilipokutana na wataalam wa Kilimo nimeweza kujifunza namna ya kuendesha kilimo kwa njia za kisasa hata matumizi ya mbolea hatua ambayo naamini itanisaidia baadae katika shuguli zangu hivyo naishukuru serikali kwa kunipatia fursa hii''alisema Julias mhitimu Afisa Kilimo katia Kikosi h