WALIMU ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAOEA ILI KUBORESHA ELIMU

 






WALIMU ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAOEA ILI KUBORESHA ELIMU

Kibondo.Katika kurekebisha upatikanaji wa elimu hapa nchini walimu wamehaswa kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazoea  ili kufikia malengo ya serikali na kuwapatia Watoto ujuzi

Hayo ameyasema na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi upande wa Elimu Charles Msonde alipokuwa akizungumza na Walimu wa shule za Msingi na sekondari wilayani Kibondo Mkoani Kigoma ambapo amesema Mkoa huo uko kiwango cha chini kielimu kutokana na ufundishaji usiozingatia vigezo

Amesema kila mwalimua anatakiwa kujipima utendaji wake wa kazi kwa kuwasaidia wanafunzi na kuwataka kuacha mazoea kazini          

Aidha Msonde ameeleza kusikitishwa kwake juu ya halimu ya elimu ilivyo wanafunzi shule za Msingi wanapanda Madarasa wakiwa hawajui kusoma wala kuandika huku walimu katika shule zinazomilikiwa na serikali wakiona ni mambo ya kaiwada na kuwahasa kuchukua hatua

‘’Wanafunzi katka shule za sekondari kuanzia kidato cha kwanza hadi channe wengi wao wamekuwa wakikwama katika masomo yao kutokana na kushindwa kuelewa lugha ya kujifua ambayo ni Kiigereza ambapo wengi hushindwa kujieleza huku walimu wakikimbizana na kumaliza Mada tu ambazo wanafunzi hawazielewi hivyo nawaomba walimu kuweni makini katika kuboresha elimu’’alisema Msonde

Baadhi ya walimu walioshiriki kikao hicho Jose Paschal anaefundisha shule ya Msingi Kibondo na John Kimasa shule ya Msingi Boma wamekili uwepo wa utendaji usioridhisha na baada ya kupata maelekezo wameahidi kufanya kazi kwa bidii na maarifa

Pamoja na mambo mengine Msonde ameitaka halmashauri ya kibondo kutatua mahitaji ya walimu na kuacha kutumia lugha zisizo rafiki walimu wanapopeleka changamoto zao  ili zitatuliwe ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanamaliza malalamiko yote ya Walimu ili wasikate tamaa



Charles M
sonde Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi Upande wa Elimu alipokuwa akizungumza na Walimu wa shule za Msingi na Sekondari kwenye Ukumbi wa Kibondo shule ya sekondari ya Wasichana


Baadhi ya Walimu walishiriki Kikao na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi Charles Msonde



 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao