RUSHWA YANGONO BADO NICHANGAMOTO KWA WANAWAKE NA WASICHA KATIKA MASUALA YA MAENDELEO







Baadhi ya Wanawake walioshiriki maadhimisho siku ya Wanawake Duniani March8,2025









Hidaya Kimpwi Mkazi wa Buhigwe






Aggripina Buyogela Mwenyekiti UWT Mkoa wa Kigoma alipokuwa akitoa salamu kwenye maadhimisho siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma


Aggrey Magwaza Mkuu wa wilaya  ya Kibondo mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Kigoma


 

Muhingo Mwemezi Kigoma

Imeelezwa Wanawake wamekuwa wakikosa haki zao kutokana na kukosa elimu mapambano dhidi ya rusha za ngono hatua ambayo imekuwa ikididimiza ndoto za watu wengi hasa Wasichana na wanawake vitendo ambavyo vimekuwa vikishamili kila uchao

Akiongea kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kimkoa katika Wilaya ya Kibondo mwakilishi wa Mkuu wa Takukuru Mkoa huo Sweetberita Nkoba amesema yapo madhara ambayo yamekuwa yakiwakuta wanawake kutokana na Rushwa ya Ngono ambapo Taasisi yake imekuwa ikitoa elimu kwenye jamii ili iweze kuepukana na na vitendo hivyo na kusisitiza jamii kuacha ukimya

Wakati wa maadhimisho hayo baadhi ya Wazazi ambao ni Rebeca Mudala Mkazi wa Kibondo na Hidaya Kimpwi Mkazi wa Buhigwe wamesema licha ya vitendo hivyo kufanyika kwa siri sana wamesema wanaendelea kutoa elimu kwa watoto wao huku wakiomba vyombo vinavyoa maamuzi kutenda haki pale watu wanapobainika kujihusisha na ukatili

‘’Kumekuwepo na malalamiko mengi ambayo yamekuwa yakielekezwa kwenye mamlaka mbalimbali kuanzia ngazi za vijiji kutotenda haki kwa kuwakingia vifua wakosaji huku wahanga wa ukatili wakiendelea kutesema hivyo vitendo hivyo havikubaliki na ni vema haki iwe inatendeka ili kujenga Imani kwa mamlaka za kutoa maamuzi’’ amesema Hidaya

Hata hivyo Mkoa wa Kigoma katika kutoa elimu ya Kisheria kupitia Kampen ya Sami Legal Aid imeweza kutataua migogoro 920 ilipokelewa na kushugulikiwa 157 ilishughulikiwa papo kwa papo na migogoro793 ilielekezwa katika mamlaka husika ili itatuliwe hapa ameeleza Mkuu wa wilaya ya Kibondo Aggrey Magwaza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye aliyekuwa Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo

Magwaza ameongeza kuwa lengo la Kampeni hiyo ni kujenga uelewa kwa wananchi ili waweze kujitambua na kuwa na matumizi mazuri ya masuala ya sheria na kutambua haki zao hatua ambayo itasaidia kupunguza Migogoro isiyokuwa na sababu kwenye jamii

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu