Mnyukano Ubunge Muhambwe

Jamal Abdlah Mwenyekiti Ccm Mkoa wa  Kigoma achukua Fomu  kugombea Ubunge Jimbo la Muhambwe
 

Frolence Samizi Mbunge Muhambwe anaetetea Kiti chake  achukua fomu ubunge Muhambwe



Kuelekea uchaguzi Mkuu 2025,Wanachama wa  Chama cha Mapinduzi Ccm Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma wameendelea kujitokeza  kuchukua fomu za kugombea nafasi za Udiwani na Ubunge  kwa ajili ya uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu

 

Baadhi ya wanachama hao mmoja wapo ni Mwenyekitiwa Ccm Mkoa wa Kigoma Jamali Abdalah ambaye  ametia nia ya kugombea nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Muhambwe Kibondo kwa kuchukua Fomu kwenye ofisi za Ccm wilayani Kibondo

 

Frolence Samizi ambaye ni Mbunge anaeteteaKiti chake nae amechukua fom kugombea nafasi hiyo kwa mara nyingine tena huku wakifuatiwa na wanachama wengine Nduhilabusa Mapigano Katibu Jumhiya ya Wazazi Wilaya ya Kasulu,  Geradina Kabululu na wengine

 

Kwaupande wake Katibu wa Ccm Wilaya ya Kibondo Rafael Sumaye amesema hadi kufikia mchana wa leo Jen 30,2025,  waliokuwa wamechukua fom idadi yao ni kumi na moja huku akiwahamasisha wanachama wengine wenye sifa kuwania nafasi za huongozi katika uchaguzi Mkuu  2025

 

Aidha Sumaye ameeleza kuwa bado ofisi yake inaendelea kuwapokea watia Nia mpaka pale muda uliopangwa kuhitimisha zoezi hilo hapo julai 2,2025

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

40 CHADEMA KIBONDO WAJIONDOA