Mashabiki wa Simba waadhimisha kwa kufanya shughuli za kijamii

 

Vaileti Macha Mwanafunzi shule ya sekondari Kibondo

Frolrntina Thelathini Mwanafunzi

Hija Othman Mwenyekiti wa Simba Tawi la Kibondo alipokuwa akiongea na Waandishi wa habari

Hija Othman Mwenyekiti wa Club ya Simba Tawi la Kibondo alipokuwa akimkabidhi mmoja wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Kibondo



Muhingo Mwemezi Kibondo

Kuelekea Kilele cha maadhimisho siku ya Timu ya Mpira wa Miguu ya Simba Wanachama na Mashabiki wa Timu hiyo Wilayani Kibondo Kigoma,  leo Agost 5,2023 wametoa Msaada wa Taulo za Kike kwa wanafunzi wa shule ya sekkondari ya wasichana Kibondo

Hija Othman ni Mwenyekiti wa Tawi  la Kibondo ameeleza lengo na madhumuni ya kutoa msaada huo kuwa kwa kile wanachokipata ni lazima kirudishwe kwenye Jamii

Aidha amesema kuwa kuwa Watoto wa Kike hasa walioko mashuleni wamekuwa wakikumbwa na changamoto ya kupata  vifaa vya  kujistili wakati wa hedhi hatua ambayo upelekea kuathirika kisaikolojia ka  kushusha kiwango cha ujifunzaji

Licha ya utoaji wa Msaada ya Taulo za Kike Wapenzi,Mashabiki wa Timu Simba walifanya usafi katika Kituo cha Afya cha Kibondo Mjini na kupanda Miti kwa ajili ya utunzaji wa Mazingira  na siku ya Jumapili Agosti 6,2023 watashiriki katika  zoezi la uchangiaji Damu litakalofanyika katika Jumba la maendeleo Kibondo Mjini ambapo ndiyo siku ya Kilele cha Tamasha la Siku ya Simba

Nao baadhi ya Wanafunzi waliopatiwa msaada huo ambao ni Frolentina Thelathini na Vaileti Macha wametoa shukrani kwa   wanachama wa Club hiyo ya Simba wamesema Msaada huo wa Taulo za Kike zitapunguza changamoto za kukosa vifaa hivyo na kueleza kuwa wanapokuwa wamekosa mahitaji hayo uathirika kwa kutojifunza ipasavyo pia msaada huo utasaidia kupunguza changamoto zinazowakabili

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao