Lipumba ziarani Kigoma

Professor Ibrahim Lipumba mwenyekiti Cuf Taifa alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Kibondo mkoani Kigoma katika mkutano wa hadhala
Lipumba ziarani Kigoma

Kwakuwa mwaka huu wa 2015 ni mwaka wa uchaguzi katika nchi ya Tanzania Wananchi wametakiwa kuhakikisha wanajiandikisha kwa wingi katika maene ambayo bado zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura ili waweze kutimiza wajibu wao katika uchaguzi unaotarajia kufanyika October mwaka huu

Hayo aliyabainisha Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi Cuf  Profeser Ibrahim Lipumba  alipokuwa akiongea na Wananchi kwenye mkutano wa hadala uliofanyika jana katika Viwanja vya Community mjini Kibondo 

Lipumba alisema kuwa watanzania wanatakiwa kucha ushabiki usiyokuwa na tija bali wanatakiwa kufanya uamzi wa mabadiliko kwa kuchagua viongozi bora na wenye maadili  na wale watakao weza kulitumikia Taifa hili kwa moyo wa dhati kwani linakabiliwa na changamoto nyingi

Aidha alisema kuwa Tanzania inatajwa kuwa na Raslimali nyingi zinazoweza kuinfanya kuwa Tajiri lakini wananchi wake ni masini kuliko inavyotakiwa kuwa kwa kukabiliwa na changamoto mbalimbali za ukosefu wa Elimu bora Afya , Maji safi  na mambo mahitaji mengi ya msingi huku akieleza kuwa hali hiyo inaweza kuatuliwa na viongozi waadilifu na wenye uchungu na maenedeleo ya nchi hii
 
 Pamoja na hatua nyingine  licha ya chadema kusimamisha mgombea wa ubunge katika jimbo la muhambwe mwenyekiti wa chama cha Cuf taifa professor Ibrahim Lipumba amesisitiza kuwa jimbo lenye mbunge ambaye chama chake kimejiunga na ukawa ataendelea kupeperusha bendelea ya chama husika na vyama vingine vitapaswa kumuunga mkono

Professor Lipumba amebainisha hayo wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya community center kibondo mjini Mkoani Kigoma jana na kwamba vyama vinne vinavyounda ukawa tayari vimekubaliana kuachiana majimbo hivyo hakuna sababu yoyote kuona jimbo lenye mbunge wa ukawa wakijitokeza wagombea wengine kutaka kuvuruga makubaliano

Aidha Professor Lipumba amesema kuwa katika majimbo ambayo yako wazi wagombea kutoka vyama vya ukawa watachukua fomu na kuomba kuteuliwa na atakayepata kura nyingi kati yao atapata nafasi ya kugombea na kuviwakilisha vyama vingine ambapo itabidi aungwe mkono na vyama vilivyosalia


Pamoja na jimbo la muhambwe kuongozwa na mbunge kutoka chama cha NCCR Mageuzi chama ambacho kimo katika umoja wa katiba ya wananchi lakini hivi majuzi chama cha demokrasia na maendeleo chadema kilisimamisha mgombea wa ubunge kinyume na makubaliano yao  

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao