Wanavijiji kata ya Mulungu wilaya ya kibondo uenda wakahitaji msahada wa chakula

Wanavijiji kata ya Mulungu uenda wakahitaji msahada chakula


Wakazi wa vijiji vya Kumbanga na Kumuhasha, Kata ya Mulungu Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma uenda wakakumbwa na Baa la njaa mwaka huu baada ya jua kali na kukosa mvua za kutosha katika msimu wa kilimo mwaka jana hali iliyosababisha mazao kuharibika mashambani

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi hao ambao ni Astelia Adriano na Julias Paulo wote wakazi kumbanga mkazi wa Kumbanga  kwa nyakati tofauti kutoka katika vijiji hivyo wakazi wa vijiji hivyo, wamesema kuwa katika msimu wa kilimo wa mwaka jana hawakupata  mvua za kutosha na kuwafanya wakulima  kupata mavuno kidogo ya chakula ambapo wengi wao wanahofia  kutofika kwenye msimu ujao wa kilimo wakiwa na chakula katika familia zao,  tofauti na vipindi vilivyopita maana wamekuwa wakipata Gunia kati ya 40 hadi 50 kwa hekali moja ila msimu huu wengi wao wamepata gunia moja hadi 2 kwa hekali moja

Wamedai kuwa hali hiyo imewahathili hasa wazazi wenye wanafunzi kwani walikuwa wakitegemea mazao  hususa  Mahindi na Maharage kwa ajili ya biashara ili kulipia ada mashuleni.

Hata hivyo  Bi, Keldonia Kayella mkazi wa kijiji cha Kuuhasha  alifafanua  kuwa kwa watu waliokosa kabisa mazao ya chakula kwa kutokupata mahindi na Maharage hivi sasa wanatumia Unga wa Muhogo kwa muda wote na kushindwa kuchangia ipasavyo chakula mashuleni kwani wanatakiwa kupeleka Mahindi na Maharage

Kwa upande wake Afisa mtendaji wa kijiji cha Kumuhasha Bi Joyce  Simon alipoulizwa alikili kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa kingine kilichochangia ni baadhi ya wakulima kuchelewa kuandaa mashamba kwa wakati kwenye mvua za mwanzo


Hata hivyo Bi Joyce aliongeza kuwa kulingana na hali hiyo uongozi wa kijiji unafaya jitihada kutoa elimu ili wananchi waweze kulima mazao yanayovumilia ukame kisha watajaribu kulipeleka swala hilo, katika ngazi ya wilaya kwa msaada zaidi na kuwatakla wananchi kuacha tabia ya kuchoma misitu bila utaratibu kwani hali hiyo uchangia mabadiliko ya hali ya hewa, kuleta jangwa na mvua kukosekana 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao