Kibondo; Serikali ya Uberigiji kupitia shiraka la Maendeleo la nchini humo BTC, kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania imetoa msahada wa Mahema 22 yenya thamani ya shilingi milion miamoja kwa ajili ya wakulima na wafugaji Nyuki wa Mkoa wa kigoma ili kuboresha utendaji kazi wakati wa uvunaji wa mazao ya nyuki


Mwemezi Muhingo Mwananchi




Kibondo; Serikali ya Uberigiji kupitia shiraka la Maendeleo la nchini humo BTC,  kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania imetoa msahada wa Mahema 22 yenya thamani ya shilingi milion miamoja kwa ajili ya wakulima na wafugaji Nyuki wa Mkoa wa kigoma ili kuboresha utendaji kazi wakati wa uvunaji wa mazao ya nyuki

Akiongea katika hafla fupi ya kukabidhi mahema hayo, kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa kigoma Kaimu katibu Tawala wa mkoa huo anaehusika na ushauri wa uchumi Robinson Mwanjala ambae alikuwa mgeni rasmi,  ameipongeza serikali ya uberigiji  wakati wa kukabidhi msahada huo na  amewataka wafugaji nyuki kuhakikisha wanayatumia ipasavyo na kwa malengo yanayo kusudiwa ili kazi yao iweze kuwa na tija

Mwanjala aliwataka wafugaji hao na wakulima kuhakikisha wanatumia vizuri elimu waliopewa katika kuvuna mazao ya Nyuki kwa kuzingatia usalama wa chakula kwa watumiaji ambapo vikundi 7 vya ushirika katika wilaya za kakonko KibondoUvinza, Kasulu na Buhigwe vilinufaika na msahada huo

''Kumewepo na na Tabia za baadhi ya watanzania kutokujali misahada inayotolewa na wahisani kwa kuharibu hata miundo mbinu wanayopewa hali inayopelekea watu hao kukata tamaa  ya kutaka kuendelea kusaidia, hivyo tunzeni mahema haya kwani ni faida kwenu wenyewe alisema mwanjala  .

Hata hivyo Afisa mazingira wa wilaya kibondo Mohamed Semdoe katika taarifa yake alisema kuwa wafugaji nyuki na wakulima katika maeneo mengi ya mkoa wa kigoma wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo kutokuwepo na kwamipango ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji na mapori pamoja taasisi nyingi za kifedha kutotoa mikopo kwa wafugaji kwa madai hawana sifa za kukopesheka hali inayopekelea uzalishaji dumi  kwa wakulima na wafugaji

Kwa upande wake Mwakilishi mkazi shirika la maendeleo la  Uberigiji  BTC Thomi Smith, ameishukuru serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na utalii hapa nchini kwa kuruhusu wafuga nyuki   kufanyaka zi zao katika mapori ya hifadhi ya wanyama na kongeza kuwa mahema hayo yatapunguza usumbufu kwa walengwa na kupata mazao yenye viwango vinavyokubalika

Nao baadhi ya wafugaji ambao ni Abubakali Chiizerona Paulina Meshack,  walisema hapo awali walikuwa wakifanya shughuli zao kwa usumbufu  mkubwa  mara wanapokwenda kuvuna asali maporini ambapo wamekuwa wakikosa sehemu ya kutunzia bidhaa zao  wakilala chini ya miti huku wakipoteza mizigo yao na wakikabiliwa na hatari ya kushambuliwa na wanyama wakali na baada ya kupewa mahema hayo yatasaidia kutunzia  mazao ya nyuki na kuweka bidha hizo katika hali ya usalama wakisubiri kusafirisha majumbani mwao

Seif Salum ambae ni mratibu wa kitengo cha nyuki katika halmashauri ya wilaya kibondo shirika la BTC alisema kuwa wafugaji nyuki wengi katika mkoa wa kigoma wamekuwa wakipata shida kubwa wanapokwenda kuvuna asali na kukosa jinsi ya kuhifadhi hali ambayo ingepelekea kupatikana kwa mazao ya nyuki yasiyokuwa viawango vinavyokubalika na baadae kushuka bei katika masoko hivyo mahema hayoyatasaidia kuzuia asali kujaa maji na hema moja wanaweza kulala watu 30

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao