Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2016

Vifo vingi vinavyotokea kutokana na ajali za Barabarani vikihusisha waendesha pikpiki ikiwa ni pamoja na kutekwa na kuuwawa vimetajwa kusababishwa na kuosefu elimu ya usalama barabarani kwakuwa biashara hiyo uyahusisha makundi ya vijana ambao wanahuruka mbalimbali iklinganishwa na malikaBaadhi ya waendesha Bodaboda

Picha
Baadhi ya waendesha Bodaboda wakiwa kwenye maandamano mjini Kakonko siku ya kuhitimu mafunzo ya usalama Barabarani Hosea Ndagala Dc Kakonko alipokuwa akiwahutubia waendesha Pikipiki  Waendesha Pikipiki daada ya kuhitimu Mafunzo usalama Barabarani Mkuu wa Wilaya Kakonko Hosea Ndagala akimkabidhi cheti cha Kuhitim Mafunzo ya usalama Barabarani mwendesha Bodaboda Vifo vingi vinavyotokea kutokana na ajali za Barabarani vikihusisha waendesha pikpiki ikiwa ni pamoja na kutekwa na kuuwawa vimetajwa kusababishwa na kuosefu elimu ya usalama barabarani kwakuwa biashara hiyo uyahusisha makundi ya vijana ambao wanahuruka mbalimbali iklinganishwa na malika Hayo yamesemwa na mkurugezi mtendaji wa asasi isiyokuwa ya kiserikali inayojishugulisha na utoaji wa elimu ya ujasiriamali, usalama Barabarani na Polisi Jamii APEC, Resicius Timanywa wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya wandeha Pikipiki wilayani Kakonko Mkoani Kigoma ambapo  amesema watu wengi wamekuwa wakishingw

Kibondo;Kwakuwa Serikali ina lengo la kuinua na kuboresha viwango vya elimu hapa nchini kwa kutilia mkazo utengezaji wa Madawati, baadhi ya walimu hasa katika shule za msingi wameomba miundondo mbinu ya majengo nayo ipewe kipaumbele ikiwa ni pamoja na nyumba za walimu ili kuongeza moyo wa ufundishaji

Picha
Kibondo ;Kwakuwa Serikali ina lengo  la kuinua na kuboresha viwango vya elimu hapa nchini kwa kutilia mkazo utengezaji wa Madawati, baadhi ya walimu hasa katika shule za msingi wameomba miundondo mbinu ya majengo nayo ipewe kipaumbele ikiwa ni pamoja na nyumba za walimu ili kuongeza moyo wa ufundishaji Baadhi ya walimu wilayani Kakonko Mkoani Kigoma wakiongea na Mwananchi jana mjini kakonko, ambao ni Theopister Balakebura na Prosper Methew walisema hivi sasa zipo changamoto nyingi katika shule hasa upungufu wa madasarasa wanafunzi kuzidi idadi inayotakiwa katika vyumba vya madarasa na walimu kukosa nyumba za kuishi hali inayosababisha ufuatiliaji wa wanafunzi kuwa mdogo Akitoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo na utekelezaji wake Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kakonko Lusubilo Joel alieleza kuwa mikakati inayofanywa na halmashauri yake kwa sasa licha ya kipato kidogo ni pamoja na kuongeza vyumba vya madarasa   hata madawati yanayopatikana yapate pakuhifadhiwa na  kujenga nyumba

Kibondo; Halmashauri ya wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma imepokea Magari mawili ya kubeba wagonjwa aina ya Toyota Land Cruiser yaliyotolewa na shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia Watoto Unicef ambapo magari hayo yanalenga kupunguza adha na kuokoa maisha ya wanawake wajawazito na watoto

Picha
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri Wilaya kakonko Lusubilo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari baada ya makabidhiano ya magari ya kubeba wagonjwa yaliyotolewa na Unicef  Magari ya kubeba wagonjwa yaliyotolewa na uncef Fadhil Seleman baada ya kukabidhiwa Magari ya kubeba wagonjwa Kibondo; Halmashauri ya wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma imepokea Magari mawili ya kubeba wagonjwa aina ya Toyota Land Cruiser yaliyotolewa na shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia Watoto Unicef ambapo magari hayo yanalenga kupunguza adha na kuokoa maisha ya wanawake wajawazito na watoto Katika hafla ya makabidhiano  ya magari hayo, iliyofanyika jana mjini Kakonko, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Lusubilo Joel, alisema kuwa kutokana na adha wanazozipata wanawake wajawazito na watoto, shirika hilo la Unicef limetoa magari hayo kwa mkopo ambao utalipwa kwa muda wa miaka mitano na kuitaka idara ya afya ya wilaya hiyo kuyatumia kwa malengo mahususi ili yaweze kuleta tija

Watumiaji wa vyombo vya moto hususa waendesha Pikipiki wametakiwa kuhakikisha wanapata elimu ya usalama Barabarani wafahamu matumizi ya barabara ili waweze kuepuka au kupunguza ajali zisizo za lazima zinazogarimu maisha ya wananchi wengi

Picha
Watumiaji wa vyombo vya moto hususa waendesha Pikipiki wametakiwa kuhakikisha wanapata elimu ya usalama Barabarani  wafahamu matumizi ya  barabara ili waweze kuepuka au kupunguza ajali zisizo za lazima zinazogarimu maisha ya wananchi wengi Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa wilaya ya Kibondo Mkoaani Kigoma, Luis Bura, aliyewakilishwa na katibu tawala wa wilaya hiyo Ayub Sebabili alipo alikwa kama mgeni rasmi wakati wa kufunga mafunzo ya siku saba ya waendesha Pikipiki maalufu kama Bodaboda wapatao 240 hafla iliyofanyika Mjini kibondo Alisema kuwa ajali nyingi zinazotokea kwa waendesha pikipiki wengi ni kwa sababu ya ukosefu wa elimu ya barabarani kutokana na mtu kujifunza kuendesha asubuhi na jioni kuanza kubeba abiria jambo ambalo ni hatari kwa maisha ya watu  kuwani  Mtu huyo anakuwa hajajua namna ya kutumia barabara, na kuwataka waendesha pikipiki  kufuata taratibu za usalama barabarani kwa kuacha kubeba abiria zaidi ya mmoja Awali waendesha Pikipiki  hao katika lisar