Kibondo;Kwakuwa Serikali ina lengo la kuinua na kuboresha viwango vya elimu hapa nchini kwa kutilia mkazo utengezaji wa Madawati, baadhi ya walimu hasa katika shule za msingi wameomba miundondo mbinu ya majengo nayo ipewe kipaumbele ikiwa ni pamoja na nyumba za walimu ili kuongeza moyo wa ufundishaji

Kibondo;Kwakuwa Serikali ina lengo  la kuinua na kuboresha viwango vya elimu hapa nchini kwa kutilia mkazo utengezaji wa Madawati, baadhi ya walimu hasa katika shule za msingi wameomba miundondo mbinu ya majengo nayo ipewe kipaumbele ikiwa ni pamoja na nyumba za walimu ili kuongeza moyo wa ufundishaji

Baadhi ya walimu wilayani Kakonko Mkoani Kigoma wakiongea na Mwananchi jana mjini kakonko, ambao ni Theopister Balakebura na Prosper Methew walisema hivi sasa zipo changamoto nyingi katika shule hasa upungufu wa madasarasa wanafunzi kuzidi idadi inayotakiwa katika vyumba vya madarasa na walimu kukosa nyumba za kuishi hali inayosababisha ufuatiliaji wa wanafunzi kuwa mdogo

Akitoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo na utekelezaji wake Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kakonko Lusubilo Joel alieleza kuwa mikakati inayofanywa na halmashauri yake kwa sasa licha ya kipato kidogo ni pamoja na kuongeza vyumba vya madarasa   hata madawati yanayopatikana yapate pakuhifadhiwa na  kujenga nyumba za walimu ili kuondoa usumbufu

Katika hatua nyingine halmashauri hiyo imepokea Madawati 200 yenye thamani tsh million 18 yaliyotolewa na shirika lisilo la kiserikali Social Action Trust Fund la Jijini Dar es Salaam ikiwa ni lengo lile lile la kuininua kiwango cha elimu na kuitikia wito wa Rais John Magufuli kama alivyosema Afisa mwandamizi wa shirika hilo Helena Chikamo  ambapo aliwaomba wadau wa elimu kuendelea kujitoa ili kufikia malengo mahususi

Wakitoa shukran juu ya msahada huo wa madawati Juma Maganga mwenyekiti wa halmashauri ya Kakonko na Zainab Mbunda katibu Tawala walisema wanaendelea kutafuta wahisani  kuziba pengo lililobaki kabla Agust 30 2016 , huku afisa elimu Christopher  Bukombe akieleza  upungufu waliokuwa nao hadi sasa ni 1688 na kuitaka jamii kuwa na tabia ya kuwelekeza watoto kutunza mali za umma yakiwemo Madawati  mashuleni

''Kufikia hivi sasa uhaba tuliokuwa nao umeshuka sana tofauti na hapo awali maana tulikuwa na upungufu wa madawati 6000 lakini kufikia muda huda huu tunahitaji madawati 1688 alisema Juma Maganga mwenyekiti halmashauri Kakonko''

Baadhi ya Wajumbe waliudhuria hafla ya kukabhiwa Madawati katika halmashauri ya Kakonko



Wanafunzi wa Shule ya Msingi Maendeleo Kakonko wakiwa Darasani

Madwati yaliyotolewa na shirika la Satf

Juma Maganga mwenyekiti Halmashauri Kakonko

Helena Chikomo Afisa Mwandamizi Satf alipokuwa akikabidhi madawati yaliyotolewa na shirika lake

Lusubiro Joel Mkurugengenzi Mtendaji Kakonko

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao