Watumiaji wa vyombo vya moto hususa waendesha Pikipiki wametakiwa kuhakikisha wanapata elimu ya usalama Barabarani wafahamu matumizi ya barabara ili waweze kuepuka au kupunguza ajali zisizo za lazima zinazogarimu maisha ya wananchi wengi

Watumiaji wa vyombo vya moto hususa waendesha Pikipiki wametakiwa kuhakikisha wanapata elimu ya usalama Barabarani  wafahamu matumizi ya  barabara ili waweze kuepuka au kupunguza ajali zisizo za lazima zinazogarimu maisha ya wananchi wengi

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa wilaya ya Kibondo Mkoaani Kigoma, Luis Bura, aliyewakilishwa na katibu tawala wa wilaya hiyo Ayub Sebabili alipo alikwa kama mgeni rasmi wakati wa kufunga mafunzo ya siku saba ya waendesha Pikipiki maalufu kama Bodaboda wapatao 240 hafla iliyofanyika Mjini kibondo

Alisema kuwa ajali nyingi zinazotokea kwa waendesha pikipiki wengi ni kwa sababu ya ukosefu wa elimu ya barabarani kutokana na mtu kujifunza kuendesha asubuhi na jioni kuanza kubeba abiria jambo ambalo ni hatari kwa maisha ya watu  kuwani  Mtu huyo anakuwa hajajua namna ya kutumia barabara, na kuwataka waendesha pikipiki  kufuata taratibu za usalama barabarani kwa kuacha kubeba abiria zaidi ya mmoja

Awali waendesha Pikipiki  hao katika lisara yao walisema kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja ukosefu wa leseni, baadhi na baadhi ya abiria kukataa kuvaa kofia ngumu kuhofia maambukizi ya magonjwa ya ngozi hali inayopelekea Askali wa usalama barabarani kuwakmata kwa makosa hayo na kuiomba serikali kufanya utaratibu wa mapema ili wanapohitimu mafunzo hayo wapate leseni

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika lisilokuw la kiserikali linalojihusisha na kutoa mafunzo ya ujasiliamali na kuondoa umasikini Apec Repicius Timanywa ambae shirika lake ndilo lililosimamia mafunzo hayo amewambia  waendesha pikipiki hao kuwa kupitia shirika lake leseni zao watafikishiwa katika maeneo yao ili kuondoa usumbufu wa kutumia garama kubwa kufuata leseni

Mkuu wa kitengo cha usalama barabarani Stephan Joka alitumia nafasi hiyo kuwataka Madereva hao kufanya kazi zo kwa kutumia elimu waliyopewa, na kusema kuwa ni vema kuhakikisha wanabadili umiliki wa vyombo hivyo vya moto ili hata inapotokea kikaibiwa iwe laisi kukitafuta tofauti kuliko kuendelea kubaki na umiliki wa mtu mwingine hatua inayosababisha usumbufu linapotokea tatizo    




Respius Timanywa Mkurugenzi Apec alipokuwa akiwahutubia mamia ya waendesha Pikipiki wakati wa ufugaji wa mafunzo  mjini Kibondo mkoani kigoma
Ayubu Sebabili katibu tawala W Kibondo aliyekuwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo Luis Bura katika hafla fupi ya kufunga mafunzo ya waendesha Bodaboda
Baadhi ya wahitimu hao ambao ni Thobias salvatory na Imara Seleman wamepongeza uamuzi wa serikali kupitia shirika la Apec  kuwafikishia mafunzo hao kwenye maeneo yao na kueleza walikuwa wanafanya kazi kwa mazoea pasipo kujua jinsi ya kutumia barabara unapokuwa unaendesha chombo cha moto

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao