Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2017

Viongozi wa nchi za Afrika Magharibi wamempa Yahya Jammeh fursa ya mwisho kuachia madaraka, huku wanajeshi wa Senegal wakiingia nchini Gambia.

Picha
Habari za kuapishwa kwa Adama Barrow zilipokelewa kwa furaha na shangwe Banjul Adama Barrow baada ya kuapishwa aliwaamuru wanajeshi wa Gambia wasalie kambin Viongozi wa nchi za Afrika Magharibi wamempa Yahya Jammeh fursa ya mwisho kuachia madaraka, huku wanajeshi wa Senegal wakiingia nchini Gambia. Bw Jammeh amepewa hadi saa sita mchana Ijumaa kuachia madaraka la sivyo aondolewe kwa nguvu na wanajeshi wa nchi za Afrika Magharibi wanaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa. Wanajeshi hao wametakiwa kusubiri hadi makataa hayo yamalizike. Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi (Ecowas) inaunga mkono Adama Barrow, ambaye aliapishwa kuwa rais mpya wa Gambia katika ubalozi wa nchini hiyo nchini Senegal. Jammeh aongezewa jina jingine Juhudi za mwisho za kumshawishi Bw Jammeh kuondoka kwa hiari, ambazo zinaongozwa na Rais wa Guinea Alpha Conde, zinatarajiwa kufanyika Ijumaa asubuhi. Mwenyekiti wa tume ya Ecowas, Marcel Alain de Souza, alisema iwapo mkutano huo u

Kakonko;Madiwani wa wanaoongozwa na Chadema katika baraza la halmashauri ya Kakonko Mkoani Kigoma wamempa siku saba Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Juma Maganga kuandika barua ya kijieleza usahihi wa kupitisha rasimu ya Bajeti ya 2017/18 kinyume na taratibu na asipo fanya hivyo watamshitaki mahakamani

Picha
Add caption Dafroza Expelius mmoja wa madiwani Chadema Juma Maganga mwenyekiti Halmashauri ya Kakonko Medas Amos katibu kambi ya Chadema Halmashauri ya Wilaya Kakonko Kakonko; Madiwani wa wanaoongozwa na Chadema katika baraza la halmashauri ya Kakonko Mkoani Kigoma wamempa siku saba Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Juma Maganga kuandika barua ya kijieleza usahihi wa kupitisha  rasimu ya Bajeti ya 2017/18 kinyume na taratibu na asipo fanya hivyo watamshitaki mahakamani Akiongea na Waandishi wa Habari jana Katibu wa Kambi wa chadema wa madiwani Medas Amosi alisema kuwa mwenyekiti huyo alitumia mabavu kupitisha rasimu hiyo kwa ikama isiyokamilika baada ya madiwani 8 wa chadema kuikataa na kukubaliwa na madiwani 10 wa ccm kukubabali ‘’Kwa kutambua kuwa alienda kinyume na sheria, inayozipa mamlaka na Madaraka serikali za mitaa kifungu cha183 sheria no7,na kifungu cha 97 sheria namba 8 ya mwaka 1982 tunataka mwenyekiti huyo atuleleze kwanini aliamua kkuki

Vipaji vingi vya ambavyo upatikana vijijini ikiwa ni michezo mbalimbali havikui kutokana na vikwazo vya kutotembelewa na makundi husika kama vilabu vya mipira na usanii

Picha
Vipaji vingi vya ambavyo  upatikana vijijini ikiwa ni  michezo mbalimbali  havikui kutokana na vikwazo vya kutotembelewa  na makundi husika kama vilabu vya mipira na usanii Katika Bonanza la michezo lililoandaliwa na shirika la maendeleo ya vijana la mkoani Kigoma KIVIDEA, lililoandaliwa na kufanyika katika kata ya Mabamba Wilayani Kibondo mkoani humo, baadhi ya vjana wengi waliohudhulia Bonanza hilo,wameviomba vilabu vya michezo hapa nchini kujenga tabia kufuatilia wachezaji katika timu za vijiji kuliko kujikita  mijini tu Aidha wameelekeza lawama zao kwa vyama vya mipira wilaya  kutofika maeneo ya vijijini angalau kuzisaidia timu zinazoanzishwa hata kwa kutoa maelekezo juu ya uendeshaji wa timu na sheria zamichezo Wamesema kuwa kutokana na Mazingira ya vijijini watu wenye vipaji vya uchezaji kama mipira wa pete miguu na muziki kwa upande wa wasichana na wanawake ina kuwa ni changamoto kwa makundi hayo kutokana mitazamo hasi wanafikiriwa kuwa kufanya hiv

Kibondo;Baadhi ya Wakazi wa Mabamba wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma wameiomba serikali ya Tanzania kustisha utaratibu wa kupokea raia wa nchi ya Burundi wanaoingia hapa nchini kama wakimbiambi kwa kuwa hali ya utulivu na amani nchini mwao imesharejea

Picha
-    Waomba hifadhi toka Burundi wakiwa kwenye kituo cha mapokezi cha Mkalazi Mabamba Luis Bura Mkuu wa wilaya ya Kibondo Everine Thadeo Twesa Thobias Sijabaje Ofisa mwakilishi wizara mambo ya Ndani Kitengo cha wakimbizi         Kibondo; Baadhi ya Wakazi  wa  Mabamba wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma wameiomba serikali ya Tanzania kustisha utaratibu wa kupokea raia wa nchi ya Burundi wanaoingia hapa nchini kama wakimbiambi kwa kuwa hali ya utulivu na amani nchini mwao imesharejea  -             -           Wadai kuhofia makundi makubwa yanayiongia kwa kasi  kuwa ni chanzo cha vitendo vya uharifu vinavyoenda ikiwemo uharifu wa mazingira kwa kukata miti hovyo kwa ajili ya maandalizi ya makazi Makambini -             -           Amos Degratias na Arcado Adam ambao ni wakazi mabamba wakiongea na Gazeti hili jana katika Kijiji cha Nyakasanda kilichoko mpakani mwa nchi ya Burundi na Tanzania    walisema kuwa hivi sasa katika nchiyo ya jirani amani iliyokuwa imet

Kibondo;Idara ya elimu katika Halmashauriya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma inakabiliwa na tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa 138 kwa shule za msingi hali inayopelekea wanafunzi wengi kutembea umbali mrefu wakifuata elimu na kusababisha adha kwao na ufundishaji kuwa mgumu kwa walimu

Picha
Kibondo; Idara ya elimu katika Halmashauriya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma inakabiliwa na tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa 138 kwa shule za msingi hali inayopelekea wanafunzi wengi kutembea umbali mrefu wakifuata elimu na kusababisha adha kwao na ufundishaji kuwa mgumu kwa walimu Vyumba hivyo vya madarasa vinavyohitajika, ni katika shule 24 za wilaya hiyo ambapo vinatarajia kugarimu kiasi cha Tsh bilion 1 na milion 300 huku shule zingine zikikosa vyumba kabisa na miundo mbinu yote kutokidhi mahitaji. Akitoa taarifa yake wa wakati wa uhamasishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa uliofanyika jana katika shule ya Msingi Nyamguruma Mkurugenzi Mtendaji  wa halmashauri hiyo Juma Mnwele alisema kutokana  na hali hiyo wameamua kuanzisha utaratibu wa kushirikiana wananchi katika shughuli za ujenzi  kawenye maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo ili kuwaboreshea walimu na wanfunzi mazingira ya jifunza na kufundishia Katika hafra hiyo ya uzinduzi wa ujenzi wa vyumb