Kakonko;Madiwani wa wanaoongozwa na Chadema katika baraza la halmashauri ya Kakonko Mkoani Kigoma wamempa siku saba Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Juma Maganga kuandika barua ya kijieleza usahihi wa kupitisha rasimu ya Bajeti ya 2017/18 kinyume na taratibu na asipo fanya hivyo watamshitaki mahakamani


Add caption

Dafroza Expelius mmoja wa madiwani Chadema


Juma Maganga mwenyekiti Halmashauri ya Kakonko

Medas Amos katibu kambi ya Chadema Halmashauri ya Wilaya Kakonko
Kakonko;Madiwani wa wanaoongozwa na Chadema katika baraza la halmashauri ya Kakonko Mkoani Kigoma wamempa siku saba Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Juma Maganga kuandika barua ya kijieleza usahihi wa kupitisha  rasimu ya Bajeti ya 2017/18 kinyume na taratibu na asipo fanya hivyo watamshitaki mahakamani

Akiongea na Waandishi wa Habari jana Katibu wa Kambi wa chadema wa madiwani Medas Amosi alisema kuwa mwenyekiti huyo alitumia mabavu kupitisha rasimu hiyo kwa ikama isiyokamilika baada ya madiwani 8 wa chadema kuikataa na kukubaliwa na madiwani 10 wa ccm kukubabali

‘’Kwa kutambua kuwa alienda kinyume na sheria, inayozipa mamlaka na Madaraka serikali za mitaa kifungu cha183 sheria no7,na kifungu cha 97 sheria namba 8 ya mwaka 1982 tunataka mwenyekiti huyo atuleleze kwanini aliamua kkukiuka taratibu  na tumemuandikia barua  asipo jibu na tusiporidhia tutakwenda mahakamani Amosi’’

Aidha Madiwani hao wa chadema waliongeza kuwa utaratibu uliotakiwa kutumika ni Theruthi mbi ya wajumbe ambao ni 12 kwa mujibu wa sheria badala yake waliopitisha rasimu hiyo ni 10 tu na kueleza sababu ya kuikata kuwa ni kutokana na kuingiza kodi ya majengo kabla ya kupa maoni ya wananchi husika

Kwa upande wake Juma Maganga ambae ndiye anaelelemikiwa amesema yeye alipitisha rasmu hiyo kwa ridhaa ya wajumbe walio wengi na anashangaa wenzake wa chadema kuwa na malamamiko ya aina hiyo  Bajeti kwa mujibu wa taratibu ilianzia ngazi za chini kabisa kwa wananchi wakakubali, huku wana wengine wakiwataka viongozi kuachana na marumbano ya siasa katika mambo ya maendeleo

‘’Madiwani wenyewe wanaolalamika ukiwauliza kwa nini wanapinga rasimu hii wanadai inautaratibu kandamizi kwa kutoza kodi ya majengo na ukiwauliza ni chanzo gani mbadala tuweke hawaelezi, na sasa watambue kuwa swala la kodi ya majengo ni maamuzi ya serikali na bado yako kwenye rasimu nna inatakiwa ipite katika ngazi zinazohusika alisema Maganga’’ 

Ikumbukwe kuwa tar 16.jan mwaka huu kilifanyika kikao cha cha baraza la madiwani kwa ajili ya kujadili na kupitisha rasimu ya bajeti  ambapo madiwani wa kambi ya upinzani wanaoongozwa na chadema waliipinga kwa madai haija kidhi vigezo

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao