Kibondo;Idara ya elimu katika Halmashauriya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma inakabiliwa na tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa 138 kwa shule za msingi hali inayopelekea wanafunzi wengi kutembea umbali mrefu wakifuata elimu na kusababisha adha kwao na ufundishaji kuwa mgumu kwa walimu






Kibondo;Idara ya elimu katika Halmashauriya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma inakabiliwa na tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa 138 kwa shule za msingi hali inayopelekea wanafunzi wengi kutembea umbali mrefu wakifuata elimu na kusababisha adha kwao na ufundishaji kuwa mgumu kwa walimu

Vyumba hivyo vya madarasa vinavyohitajika, ni katika shule 24 za wilaya hiyo ambapo vinatarajia kugarimu kiasi cha Tsh bilion 1 na milion 300 huku shule zingine zikikosa vyumba kabisa na miundo mbinu yote kutokidhi mahitaji.

Akitoa taarifa yake wa wakati wa uhamasishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa uliofanyika jana katika shule ya Msingi Nyamguruma Mkurugenzi Mtendaji  wa halmashauri hiyo Juma Mnwele alisema kutokana  na hali hiyo wameamua kuanzisha utaratibu wa kushirikiana wananchi katika shughuli za ujenzi  kawenye maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo ili kuwaboreshea walimu na wanfunzi mazingira ya jifunza na kufundishia

Katika hafra hiyo ya uzinduzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa mkuu wa wilaya hiyo Luis Bura ambae alikuwa mgeni rasmi alipokuwa akizungumza na wananchi waliohudhulia alitoa wito kwa  jamii na Viongozi  kujenga Tabia ya kujitegemea katika shuguli zao za maenedeleo ili serikali iweze kwaunga mkono katika hatua inayokuwa ikiendelea

Walimu na wanafunzi  ambao ni Zabron Kasato na Tmain Mayi walieleza  usumbufu wanaoupata kutokana na kutembea  umbali mrefu huku   wakiupongeza uongozi wa halmashauri kwa kuliona swala la uhaba wa miundo mbinu mashuleni hasa ukosefu  vyumba vya madarasa na Nyumba za walimu  wakiomba litiliwe mkazo ili kuonyesha mafanikio

Aidha kutokana na serikali kutaka kuboresha elimu na kuondoa malipo mwaka wanafunzi walioandikishwa kuanza darasa la kwanza katika wilaya ya Kibondo 2017 ni asilimia 25 tofauti na mwaka jana kiwango kinachojwa kuwa cha chini ambapo mkuu wa wilaya hiyo amewataka wazazi na walezi kuwapeleka  watoto shule na atakae kiuka atachukuliwa hatua za kisheria

Licha ya maelezo  ya mkuu wa wilaya kuwachukulia hatua wazazi watakao kataa kuwandikisha watoto wenye umri wa kwenda  shule, Baadhi ya Wazazi wamelalamikia Vitendo vya wanaume kukataa kutoa mahitaji kwa wanafunzi na kukataa kuwaandikisha shule na kutelekeza familia zao walieleza Grace Joakim na Ester Bahati

Hata hivyo imetajwa kuwepo na changamoto ya uelewa Mdogo kwa baadhi ya wazazi juu maswala ya elimu kwa kukataa kuwapeleka watoto wao mashuleni wapate elimu, na kushindwa kutoa mahitaji muhimu kwa kisingizio cha uwezo mdogo na kuiomba serikali kuhamasisha jamii  juu hilo

‘’ Wanaosomesha watoto kwamba ni watu wote wenye uwezo wa kiuchumi bali ni uelewa wa wazazi na kuona umuhimu wa kusomesha watoto maana tumeona watu wengine wakiuza mpaka mashamba yao kwa ajili ya kusomesha watoto wao alisema Mwalimu Melina Kayogoma’’

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao