Kibondo;Baadhi ya Wakazi wa Mabamba wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma wameiomba serikali ya Tanzania kustisha utaratibu wa kupokea raia wa nchi ya Burundi wanaoingia hapa nchini kama wakimbiambi kwa kuwa hali ya utulivu na amani nchini mwao imesharejea

-  
Waomba hifadhi toka Burundi wakiwa kwenye kituo cha mapokezi cha Mkalazi Mabamba

Luis Bura Mkuu wa wilaya ya Kibondo

Everine Thadeo Twesa

Thobias Sijabaje Ofisa mwakilishi wizara mambo ya Ndani Kitengo cha wakimbizi

        Kibondo;Baadhi ya Wakazi  wa  Mabamba wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma wameiomba serikali ya Tanzania kustisha utaratibu wa kupokea raia wa nchi ya Burundi wanaoingia hapa nchini kama wakimbiambi kwa kuwa hali ya utulivu na amani nchini mwao imesharejea 
-           
-          Wadai kuhofia makundi makubwa yanayiongia kwa kasi  kuwa ni chanzo cha vitendo vya uharifu vinavyoenda ikiwemo uharifu wa mazingira kwa kukata miti hovyo kwa ajili ya maandalizi ya makazi Makambini
-           
-          Amos Degratias na Arcado Adam ambao ni wakazi mabamba wakiongea na Gazeti hili jana katika Kijiji cha Nyakasanda kilichoko mpakani mwa nchi ya Burundi na Tanzania    walisema kuwa hivi sasa katika nchiyo ya jirani amani iliyokuwa imetoweka kutokana na vurugu za kiasasa imereje hivyo wimbi kubwa linaloendelea kuingia hawana vigezo vya ukimbizi
-           
-          ‘’Kinachotutisha ni watu wengi badala ya kwenda katika vituo vya kupokelea wakimbizi uishia vijijini na wanaoingia katika Makambi ya wakimbizi baadae utoroka na kuanza kurudi nchini mwao bira taratibu na wengi wanakimbia Njaa na hali ngumu ya maisha alisema Amos ‘’
-           
-          Mwananchi liliweza kufika katika kituo cha Kupokelea wakimbizi  kilichoko katika kijiji cha Mkalazi  na kuona hali halisi ilivyo na kuongea na baadhi ya wafanyakazi wa mashirika ya kuhudumia wakimbizi ambao aliulizwa Ofisa mmoja wa shirika la Twesa, aliyejimbulisha kwa jina la Everin Thadeo na kueleza kuwa idadi kubwa ya wakimbizi  wanaingia Tanzania katika siku za magulio jumamos na jumatano
-           
-          Baadhi ya waomba hifadhi ambao  ni Muwenayo Athumani Kimuga Said walipohojiwa juu ya hali ilivyo nchini mwao na kinachowakimbiaza  walisema wanavamiawa nyakati za usiku na kupewa vitisho hali inayopelekea kuyakimbia makazi yao hali hali ngumu ya Maisha
-           
-          ‘’ Tunapowauliza kwanini mnakuja siku za jumatano na jumasi wanatueleza kuwa kwa siku za kawaida wanajeshi wa nchi yetu utuzuia ila kwa siku hizo tunawambia kuwa tunenda masokoni kama kawaida kwa mosoko ya ujirani mwema alisema Thadeo’’
-           
-          Hata hivyo Afisa mwakilishi toka Wiazara ya Mambo ya Ndani Kitengo cha wakimbizi Thobias Sijabaje alikiri kuwepo kwa idadi kubwa ya wakimbizi wanaoingia nchini kuwa kuanzia mwezi desemba mwaka jana hadi sasa wanapokea watu 463 kwa siku moja katika Vituo vya Mkalazi Lumasi na Mgunzu
-           
-          Aidha Thobiasi aliongeza kuwa Tanzani ni moja ya nchi zilizo saini mkata wa umoja wa Mataifa kuhusu waomba hifadhi  nao wanapokea watu wanaosalimiasha roho zao hivyo kutokana na mkataba huo hakuna mtu mwenye mamlaka ya kumrudisha mtu anaekimbia kujisalimisha ila kwa sasa wataendelea kuwapokea huku taratibu za kimataifa zikisubiliwa
-           
-          Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kibondo ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo Luis Bura alisema kuwa  kinachosababisha watu wengi kuingia Tanzani kama wakimbizi wakitoka nchini Burundi ni kwasabu walikia shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa linatarajia kubadilisha utaratibu wa kuwapa chakula badala yake litakuwa linatoa fedha kwa wakimbizi wengi kuhadiwa kupewa hifadhi ulaya na Amerika
-           
-          Bura aliongeza kuwa hivi sasa katika Kambi ya wakimbizi ya Nduta iliyoko wilayani Kibondo inakaribia kujaa kwa kuwa na idadi ya wakimbizi wapatao 90 elf na kusema kuwa italazimika kufungwa watakapofika laki 120,000 kwa kuwa ndiyo uwezo wake baada ya hapo hakuna mkimbizi atakayeruhusiwa kupelekwa kambini humo kwa kuhifadhiwa
-           
-          Raia wengi wa nchi ya Burundi wamekuwa wakiikimbia nchi hiyo kutokana na machafuko ya kisiasa baada ya Rais Nkurunziza  kutangaza kuwania muhula wa tatu kugombea kiti hicho mwaka 20015
-          Mwisho
-           
-            
-           
-           


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao