Bujumbula; Baada ya hali ya amani kurejea nchini Burundi baada ya machafuko yaliyoyakumba baadhi ya maeneo hali iliyopelekea wananchi kuyakimbia makazi yao na utulivu kuweposasa, viongozi wa nchi hiyo wamewataka Raia walioko ukimbizin kurudi na kuendelea na maisha ya kawaida

Moja ya Mtaa katika mji wa Bujumbula Nchini Burundi
wakazi wa Jiji la Bujumbula wakiendelea shuguli zao kama kawaida
Abdalah Hasan ambae ni mkuu wa Mkoa wa Ruyigi amesema hayo wakati kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma Tanzania ilipozulu nchini humo kwa ajili ya kudumisha ujirani mwema kati  ya Burundi na Tanzania

Aidha liongeza kuwa baada ya machafuko ya kisiasa ya mwaka 2015, hadi sasa watu bado wanakimbia kwa madai ya kuwepo machafuko ambayo hivi sasa hayapo na kuwataka kurejea na kuipenda nchi yao kwa kuwa Burundi itajengwa na kulindwa na warundi wenyewe

Nae Luis Bura ambae ni mkuu wa wilaya ya Kibondo  Tanzania, aliiomba serikali ya Burundi kutengeneza mazingira ya kuwarudisha watu wake nchini mwao kwakuwa amani imeshapatikana akidai wanaokimbia hawana sifa za ukimbiazi na wameshazuia kupokea watu wasiyokuwa na sifa za ukimbizi kupokelewa katika kambi zilizoko wilayani kwake

Katika Jiji la Bujumbula linalodaiwa kukubwa sana na machafuko 2015 Gazeti hili lilishuhudia wakazi wake wakiendelea na shuguli mbalimbali za kibiashara na nyinginezo bila wasi wasi na kuzungumza na baadhi yao ambao ni Buchumi Shomali na Ngenda Banka ambapo  walidai hivi sasa hakuna tatizo lolote  wakiwataka ndugu zao kurudi nyumbani  huku wakazi wa mkoa wa Ruyigi unaopakana na Tanzania, Hamida Kharufan na Didas Luzovil wakisema kuwa inadaiwa wenzao wanakimbia njaa tu warudi wafanyekazi wajenge nchi yao

‘’’Sisi hivi sasa nchi nzima ya Burundi tunasafiri usiku kilometa nyingi bila kubugudhiwa na Mtu yeyote kutokana na utulivu uliopo sasa hao wanaoendelea kuitoroka nchi yao wakimbia nini  warudi tujenge nchi yatu ukimbizi si mzuri alisema Ngenda Banka’’

Kiongozi wa Jumhiya ya Vijana wa Chama cha CNDD FDD, nchini humo Niyonashima Desire ambayo imekuwa ikituhumiwa kuwasmbua raia wake na kudai wanawakimbia wao alipoulizwa  kama tuhuma hizo ni za kweli amesema kuwa wao siyo jeshi wala hawatishi watu ila wengi wao walikimbia kwa hofu  na kushawishiwa na wanasiasa  kwakuwa machafuko yalitolea zaidi Bujumbula kwanini wa mikoa mingine waendelee kukimbia

Nchi ya Burundi iliingia katika machafuko baada ya Rais wa nchi hiyo Piere Nkurunziza kutangaza kuwania muhula wa Pili 2015 na kusababisha warundi wengi kukimbilia katika nchia za Uganga, Rwanda na Tanzania

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao