Kibondo;Chuo cha Uuguzi kilichoko Wilayani Kibondo mkoani Kigoma kina kabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukosefu wa miundo mbinu ya majengo fedha kwa ajili ya kuendeshea chuo hicho na ukosefu wa watumishi wakutosha hali inayopelekea kuathili ufundishaji







Alfrida Ndungulu mkuu wa chuo
Atashasta Nditiye Mbunge jimbo la Muhambwe

Kibondo;Chuo cha Uuguzi kilichoko Wilayani Kibondo mkoani Kigoma kina kabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukosefu wa miundo mbinu ya majengo fedha kwa ajili ya kuendeshea chuo hicho na ukosefu wa watumishi  wakutosha hali inayopelekea kuathili ufundishaji

Chuo hicho hakina Jengo la Maabara kwa ajili ya kujifunzia kwa vitendo kwa wanafunzi walimu waliopo ni watatu na mahitaji wanatakiwa wapo walimu kumi na tano

Akiongelea swala hilo jana  katika mahafali ya saba  kwa wahitimu ngazi ya cheti mkuu wa chuo hicho Alfreda Ndungulu alisema licha ya walimu kujituma kufanya kazi kwa bidii lakini changamoto hizo zimekuwa zikiwalemea kwa kukosa mahitaji muhimu kama vifaa vya maabara kwa ajili ya kufundishia huku akiiomba serikali kupitia wizara ya Afya maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto kulitazama kwa namna ya pekee

Nao wanafunzi waliokuwa wakihitimu kwenye chuo hicho cha uuguzi ambao ni Adela James na Mary Esau, walisema  ni vema serikali ikaweka mpango wa kuwakopesha wanafunzi  katika sekta ya Afya  kwa ni nayo ni muhimu huku wakieleza hali waliyokuwa wakikumbana nayo wakati wa masomo yao walikuwa wakitegemeaf edha kutoka kwa wazazi ambazo zilikuwa hazikidhi mahitaji   na kulazimika kula mlo mmoja kwa sikua Adela

‘’Jinsi ambavyo mikopo inatolewa na serikali basin a sisi tungewekewa utaratibu wa kupata mikopo kwa tunapata shida sana kwa kutegemea fedha za wazazi ikilinganishwa hata huduma za afya ni muhimu kwani hata masomo yake lazima uwe umetulia ili kupata uelewa mzuri wakati wa masomo bila kuwa mawazo ya Ada na mahitaji mengine alisema Adela

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Atashaster  Nditiye, ambae alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo aliitaka jamii na wazazi wenye wanafunzi kuendelea kuchangia huduma za elimu katika sekta ya Afya  kwani serikali bado inaendelea kulitazama kisera japo  ni muhimu kwani utaratibu wa kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaopata elimu katika Vyuo vya Afya hasa ngazi ya  Cheti haukuwepo ili kuondoa Nkanganyiko kwa sekta zingine  

Laurian Kanaganwa Kaimu Mganga mkuu wa wilaya ya kibondo yeye aliwataka  wahitimu hao kutoridhika na ngazi hiyo walinayo bali wajitahidi kujiendeleza zaidi kwakuwa mambo mengi ya huduma za afya ya Binadamu yanabadilika kila kukicha


Chuo hicho kilichoanzishwa mwaka 1977 kikiwakinatoa mafunzo ya Mtoto kwa wakati huo, kilifungwa mwaka 1998 na kuanzishwa tena mwaka 2008 na kuanza kutoa elimu ya Mafunzo ya Uuguzi ngazi ya Cheti  na kwa mwaka huu wanafunzi walihitimu ni 45 tu 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao