Kibondo;Idadi kubwa ya Wakimbizi wanaohifadhiwa mkoani Kigoma ni moja ya changamoto zinazoukabili mkoa huo ikiwa usalama mdogo kwa baadhi ya wenyeji, uharibifu wa miundo mbinu, na mazingira









Bruno Nkwabi Kaimu Mkuu wa Makazi
James Mwangi ofisa Mazingira UNHCR

Revocatus Nginila Mratibu Redeso
 Kibondo;Idadi kubwa ya Wakimbizi wanaohifadhiwa mkoani  Kigoma ni moja ya changamoto zinazoukabili mkoa huo ikiwa usalama mdogo kwa baadhi ya wenyeji, uharibifu wa miundo mbinu, na mazingira

Wakimbizi hao walioko katika makambi ya Nyarugusu Kasulu, Mtendeli  Kakonko na Nduta  Kibondo, wanakadiliwa kufikia 270 ambapo uharibifu  uko kwa kiwango cha juu huku  uoto wa asili  na vyanzo vya maji vikikauka hali ambayo inatishia kuwepo  kwa mabadiliko ya tabia nchi

Akiongea wiki iliyopita na Wakimbizi wa Kambi ya Nduta iliyoko wilayani Kibondo  kaimu mkuu wa makazi wa kambi hiyo, Bruno Nkwabi amewataka kutunza mazingira na mali asili zote walizozikuta ambazo zinawasaidia hata wao

''Lazima mkumbuke wakati mnaingia kwenye maeneo haya mlikuta kila kitu kiko vizuri na mliweza kufurahia hivyo lazima muendeleze hali mliyoikuta  kwa kutambua kuwa kila kitu  kilitunzwa'' alisema Nkwabi   

Kutokana na wingi wa Wakimbizi hao na maeneo wanayoishi baadhi yao Imana ilakiza Bosco na Janeviva Emmanuel walisema wamekuwa wakilazimika kutafuta nishati ya kupikia na wakiipata kwa shida  kwa kuingia katika maeneo ya wenyeji

Kwa upande wake Mratibu wa shirika linalojihusisha na uhifadhi wa mazingira katika Kambi za Nduta na Mtendeli la Redeso, Revocatus Nganila alisema changamoto iliyopo ni kutokana na serikali kutotenga maeneo maalum ya kupata nishati kama kuni kwa ajili ya matumizi

Aidha Nginila aliongeza kuwa wao shirika lenye dhamana lenye uhifadhi wa mazingira wamekuwa wakijitahidi kuielimisha jamii ya ya wakimbizi juu ya matumizi ya majiko banifu yanayotumia kuni chache na kuwataka kutokata miti mibichi bali iliyokauka ikiwa ni pamoja na kuhifadhi vyanzo vya maji 

 ofisa mazingira wa shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR, James Mwangi akisema ipo haja ya kuweka mikakati maalum  juu ya uhifadhi wa mazingira kwa wakimbizi na Wananchi wenyeji ili kufikia malengo yanayokusudiwa na kunusuru Vizazi vijavyo

,Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao