NMB kupunguza changamoto Madawati Shule za Msingi Wilayani KibondoFrolence Samizi Mbunge wa Muhambwe akisa


Frolence Samizi Mbunge wa Muhambwe alipokuwa akiongea na wakazi wa Busunzu


Seka Urio Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi Tabora alipokuwa akitoa salam zake wakati wa hafla ya makabidhiano shule ya Msingi Busunzu B





Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Kanali Agrey Magwaza
 kushoto akikabidhiana Madawati na Meneja wa Benki ya NMB Seka Urio kanda ya ya Magharibi wakiwa katika shule ya Msingi Kibondo

Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Aggrey Magwaza akikabidhiana Madawati ya shule ya Msingi yaliyotolewa Na Benki ya NMB kulia ni Meneja wa Benki hiyo Kanda ya Magharibi Seka Urio


Kibondo. Shule ya Msingi Busunzu B iliyoko Wilayani Kibondo Mkoa wa Kigoma yenye Idadi ya Wanafunzi 2980, inakabiliwa na Changamoto Mbalimbali ikiwa ni pamoja na uhaba wa Madawati hali ambayo imekuwa ikisababisha usumbufu kwa wanafunzi wakati wa ujifunzaji

Shule hiyo ina Madwati 565 na inaupungufu wa Madawati 421 huku uhitaji ni Madawati 985 ambapo wanafunzi wa shule hiyo wameeleza changamoto hiyo ambavyo imekuwa ikiwasbabishia  adha kubwa

 

 Wanafunzi wa shule hiyo Jaclin Jeremia na Kefa Buzingu katika wamesema Dawati moja wamekuwa wakikaa Watu 5 badala ya Watatu huku wengine wakikaa chini  na wengine  kukalia Mawe na Matofali

‘’Tunapata adha kubwa sana wakati wa kujifunza mfano kama sisi  kama sisi Wasichana Nguo zetu zimekuwa zikichafuka sana na kutufanya tujisikie vibaya na miandiko yetu uharika ila alisema Jcklin Mwanafunzi B

 Katika kukabiliana na hali hiyo Benki ya NMB imetoa Madawati 50 yenye thamani ya shilingi million tano ambapo  Meneja wa Benki  hiyo Kanda ya Magharibi  hiyo Seka Urio amesema wanafanya hivyo ili kuunga Mkono serikali juhudi zake za kuboresha elimu

Aidha Seka ameongeza kuwa wamekuwa wakitoa gawio la faida inayopatikana na kuirudisha katika jamii ili kusaidia Nyanja mbalimbali katika utoaji huduma kwa Wananchi ambapo ameeleza kuwa kwa mwaka huu Benki hiyo imeshato sehemu ya faida asilimia 1% ambayo ni sawa na Sh 6 Bilion nchi nzima

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Frolence Samizi amepongeza Mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Viongozi wa Serikali na Benki hiyo ambayo yamelekea kupatikana kwa Madawati hayo ambayo yatapunguza changamoto iliyokuwepo shuleni hapo

Hata hivyo Mbunge huyo aliwataka wanafunzi kutambua Jitada kubwa zinazofanywa na serikali kwa kushirikiana na Wadau akiwataka kusoma kwa bidii huku akiwataka Wadau wengine kama Mashirika na Benki zingine na kutoa michango yao kuboresha miundombinu ya Elimu na Sekta zingine hapa nchini

Akipoke Madawati hayo kutoka Benki ya NMB Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Kanali Aggrey Magwaza amewataka wanafunzi kupenda elimu ili jitiada za serikali na Wadau za kuboresha miundombinu ziweze kuleta tija kwani Elimu ndiyo msingi pekee wa kumkwamua Binadamu katika lindi la umasikini huku akitoa wito kutunza vifaa vinavyotolewa na Wadau ikiwemo serikali ili viweze kutumika kwa muda mrefu

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao