Wahitim Jkt wahaswa kuchangamkia Fursa zinazoibuliwa na serikaliVijana Jkt Mtabila Kikosi 825

 

Wahitim Jkt Kikosi 825 Mtabila wakiwa kwenye Paredi siku ya kufunga mafunzo

 


Patrick Ndwenya Mkuu wa Kikosi 825 Mtabila 

Isack Mwakisu Mkuu wa Wilaya ya Kasulu alipokuwa akiwahubia mamia ya wananchi wakati wa kufunga Mafunzo ya awali ya Kijeshi mujibu wa sheria Mtabila 825




Kasulu.Vijana Nchini wametakiwa kuchangamkia Fursa zinazotolewa na serikali kama Kilimo na Ujasiriamali, ili kukabiliana na changamoto za ajira waweze kujikimu kimaisha

Akiwa  kwenye Hafla ya Kufunga mafunzo ya awali ya Kijeshi Vijana mujibu wa sheria Oparasheni Miaka 60 ya Jkt Kikosi 825 Mtabila, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma Isack Mwakisu amesema Vijana waache kutegemea kazi za maofini bali wafanye kazi mbalimbali kulingana na ujuzi wao

Aidha aliongeza kuwa lipo pia tatizo la upatikanaji wa mitaji lakini wakifuata miongozo na taratibu nzuri wanaweza kupata mikopo kutoka Taasisi mbalimbali za fedha ikiwa ni pamoja na mikopo inayotolewa katika Halmashauri na Majiji hapa nchini

‘’Nawambia nyinyi vijana mkiweza kujitambua na mkawa na bidii kujituma katika shughuli zenu za Mikono mtafanikiwa na nyie mtakaoendelea katika Vyuo mbalimbali mnatakiwa kusoma kwa bidii huku mkitanguliza uzalendo katika nchi yenu’’alisema Mwakisu

Nae Mkuu wa Kikosi 825  Kj Mtabila Patrick Ndwenya amesema Vijana waliopokelewa Kikosini hapo wamejifunza mambo mbalimbali kama Kilimo na ufugaji Nyuki  na kuwataka kutumia ujuzi huo na kuelemisha Vijana wenzao maali popote watakapokuwa

Aliongeza kuwa  Vijana hao katika kipindi cha miezi mitatu walipokuwa kikosini hapo waliaandaa shamba la Mahindi lenye ukubwa wa Hekali 400 na Mizinga ya nyuki 400 baada ya kujifunza masuala ya ufugaji nyuki

Baadhi ya Vijana waliohitimu Kikosini ahapo ambao ni Emmanuel Marwa na Restuta Mwakifuna wamepongeza hatua hiyo ya mafunzo kwani imewajengea uwezo wa kufanya mambo ambayo walikuwa hawayawezi kama kulima na hata kuchangamana na wenzao kwa kushirikiana kulingana na mazingira ya maisha ya familia walikotoka, huku wakiahidi kuwa waadilifu popote watakapokuwa

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao