Wanawake Jitambueni kufanya kazi




 

Wanawake Jitambueni kufanya kwa kujituma kazi


Kibondo.Wanawake wamehaswa kujituma katika kufanya kazi ili kuogeza vipato vya familia na kuboresha malezi ya watoto ili kuepukana na ukatili wa kiuchumi na kijinsia

Wengi wao wametajwa kutumia mitandao na kuiga tamaduni zisizostaili hatua ambayo imekuwa ikiwachelewesha kufikia malengo yao na kusababisha kukata tamaa

Wakiwa katika siku 16 za kupinga ukatili, kwenye hafla  iliyo wahusisha Wanawake wanachama wa Kibondo women Gala cha Mkoani Kigoma Mwalimu wa Masuala ya Kisaikolojia Epsalia Malya amesema wanawake wengi wamekuwa wavivu wa kujishuguli huku wakipendelea kujipamba na kushindwa kufanya kazi

’Aliyeajiriwa afanye kazi kwa weredi kwa kufuata taratibu za kazi Mfanyabiashara nae awe mbunifu kwani umakini na kujali ni moja chanzo cha mafanikio kwa mlengwa na hizo ndizo baraka’’alisema Malya

Nae Sadaka Gandi toka Jijini Dsalaam ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla  ambae pia  ni Mtaalam wa Saikolojia amesema zipochangamoto nyingi zinazikabili jamii hasa wanawake kutokana na kutojitambua ambapo amewataka wanandoa wote kuheshimiana na kuwataka wanaume kutokaa kimya pale wanafanyiwa ukatili

Chama hicho cha wanawake Kibondo kilianzishwamwaka 2023 kwa lengo la kutoa elimu kwa kuyashirikisha makundi ya wajasiriamali, watumishi wa serikali na mashirika ili kufanya shuguli zao kitaalam badala ya mazoea hali ambayo imekuwa ikisababisha wengi wao kutofanikiwa ipasavyo

Mwenyekiti wa Chama hicho Doreen Lyimo amesema tangu kuanzishwa kwake na kuwapa elimu wanawake namna ya kufanya kazi kulingana na mazingira yao ya kazi ikiwa ni pamoja na malezi ya familia na wengi wamenufaika kutokana na elimu ambazo wamekuwa wakipeana kwa kuwashirikisha Wataalam mbalimbali

Rebeca Mdala ni mmoja wa Wanachama wa umoja huo  na ambaye amekuwa akijihusisha na Biashara pamoja na kusaiia Watoto wanaoishi kwenye Mazingira magumu, amesema kutokana na kujengeana uwezo ambao wamekuwa wakiupata kupia kwenye umoja wao amefanikiwa kiutendaji katika shuguli zake kuihudumia jamii

Hafla hiyo sambamba na kufundwa na wataalam wa Saikolojia, kwa pamoja wametoa tuzo kwa Wanawake ambao wamekuwa wakifanya shughuli zao za kuhudumia jamii kwa werdi katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na Afya, Elimu, Ustawi wa Jamii na Wajasiriamali kwa kuwa mfano mzuri

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao