CHANGAMOTO WANAFUNZI WANAOACHA SHULE

 











Muhingo Mwemezi Kigoma


Kigoma. Licha ya uwepo wa maendeleo ya upatikanaji wa Elimu hapa nchini katika shule za Msingi na sekondari bado   tatizo la Wanafunzi kushindwa kumaliza shule  ni kubwa na linaendelea kutokana na saababu mbalimbali na kupelekea Watoto kukosa haki za Msingi

Changamoto hiyo haina budi kutiliwa mkazo ikiwa ni pamoja na jamii  Wazazi na Walezi kote nchini kuendelea kuhimizwa na kuelimishwa kutambua umuhimu wa Elimu, ambapo makundi ya rika barehe kuanzia miaka 9 hadi 15 ndiyo wahanga wakubwa

Tatizo hilo linachangiwa na sababu mbalimbali kama Umasikini Umbali wa kutoka katika maeneo ya Makazi kwenda kwenye huduma za shule hatua ambayo hupelekea Watoto wengi kukata tamaa  wakati mwingine kukumbwa na Vitendo kikatili mfano Takwimu za mwaka 2022 Mkoa wa Kigoma ulipata nafasi ya 8

Takwimu hizo zinaonyesha  Mkoa huo una Watoto waliokatisha masomo 10,355  wa shule za Msingi na ulikuwa  wa  na 17  kwa kuwa na Idadi ya Wanafunzi 4,231kwa shule za Sekondari

Hali hiyo iliweza kuwaibua Wadau wa Elimu Plan Internation kupitia Mradi Kagis [ Keeping Adolescent Girls in School] kusaidia Makundi ya Wasichana ambao wanaishi katika mazingira magumu na wanatembea mwendo mrefu kwenda shule kwa kuwapatia Baiskeli katika  Halmashauri ya Geita na Geita Mji Mkoani Geita na Kibondo Mkoani Kigoma

Nikodemas  Gacho Mkuu wa Mradi wa Kagis  alipokuwa kwenye Uzinduzi wa utoaji wa Baiskeli kwa Wanafunzi wa shule ya Sekondari Biturana Kibondo Mkoani Kigoma  alisema hadi kukamilika kwa mradi huo wanatarajia kutoa Baiskeli 2200 ambapo mwaka jana zilitolewa Baiskeli 550 Geita, na mwaka huu zilizotolewa ni ni 300 kwa Geita na 259  wilayani Kibondo Mkoani Kigoma

Hata hivyo Nikodemas ameendelea kutoa wito kwa Viongozi wa serikali na Mashirika  kuungana kwa pamoja kukwamu makundi haya ambayo yanakumbwa na masibu mbalimbali hasa wasichana

Afisa Elimu Mkoa wa Kigoma Simon katika shukrani zake Shija akiwataka viongozi kuhamasisja jamii juu ya umuhimu wa elimu na kuwataka wananchi kutambua kuwa Wahisani mara nyingi wana muda maalu wa kuendelea kutoa misaada hivyo ni vema kujipanga namna ya kundeleza Watoto hao, huku  Rasta Bally toka ubalozi wa Canada  akisema wanashirikiana na Tanzania kuboresha Elimu ya Mtoto wa Kike na kuwahasa Wanafunzi hao kupenda elimu kwani ndiyo urithi wao

Asha Isaya na Mariam Lameck ni baadhi ya Wanafunzi wa shule ya sekondari Biturana wameeleza adha wazokutana nazo ktembea mwendo mrefu wanafika shuleni wamechelewa na kuadhibiwa na walimu na wanaporudi majumbani mwao  ushindwa kuendela na shughuli zingine huku Mratibu Elimu Kata ya Biturana  Benard Shibabo akisema kuwanafunzi katika kata yake wanatembea ubali wa kilomita 7 hadi9 na kuongeza kuwa kwa mwaka jana wanafunzi waliacha shule za msingi ni 50 na 30 sekondari

Nae Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Kanali Aggrey Magwaza aliyewakilishwa na Katibu Tarafa ya Kifura, Omary Shekarata ameitaka jamii kuthami Misaada inayotolewa na Wahisani na kueleza Baiskeli hizo zisitumiwe na watu wazima zitunzwe Mwanafunzi anapomaliza elimu yake anarudisha Baiskeli hiyo shule ili watumie wengine

Mradi wa Kagis katika Shirika la Plan Intertion unafadhiliwa na Serkali ya Watu wa Canada  na unalenga kuwafikia wanufaika102,236 ambao wanafunzi ni 96, wasichana 49,336 wavulana 47,162 wenye umri wa miaka 9 hadi 15 katika shule za Msingi 73 na sekondari 17 na  walio nje ya shule  5,900 wasichana na 2, 950 katika Vijiji 118

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao