KIBONDO KUUNDA SHERIA NDOGO KATIKA UCHANGIAJI WA CHAKULA MASHULENI

 






Gabriel Chitupila Kaimu Mkurugenzi Hshauri Kibondo



Jacklin Sospeter Afisa Lishe wilaya ya Kibondo



Baadhi ya washiriki wa Kikao cha Kamati ya Lishe wilayani Kibondo waliokuwa wakitathmin hali ya Lishe wilayani Kibondo




KIBONDO KUUNDA SHERIA NDOGO KATIKA UCHANGIAJI WA CHAKULA MASHULENI

Licha ya hamasa na elimu kuendelea kutolewa kwa jamii juu ya uuchangiaji chakula mashuleni ili wanafunzi wapate chakula cha mchana Wilayani Kibondo Mkoa wa Kigoma, hatua hiyo bado ni kizungumkuti kutokana na baadhi ya wazazi na walezi kushindwa kutoa michango ya chakula na wanafunzi kushinda njaa

Baadhi ya wanafunzi wanapata chakula cha mchana na uji  saa nne kutokana na wazazi wao kuchangia huku wengine wakishinda njaa mashuleni kutokana na wazazi na walezi kushindwa kutoa michango ya chakula

Wanafunzi akiwemo Abdukarim Ramadhani na Jesca Reuben chakula wala uji ambao hawapati wamesema wanakumbana na wakati mgumu mara inapofika nyakati za mchana kutoka na kuhisi njaa ambapo usinzia na kushindwa kusikiliza Mwalimu huku wanaopata chakula wakichekelea na kueleza kuwa kwa sasa ushiriki wao katika masomo ni mzuri

‘’Kwakweli tunapata shida sana tupopata njaa huku wenzetu wakielekea kupata chakula wakati mwingine wenzetu wanakula tukiwa tumewatazama maana tunatoka majumbani asubuhi bila kula chochote na shuleni tunatoka muda umeenda sana majira ya saa kumi jioni’’alisema Jesca mmoja wa Wanafunzi wasiopata chakula shuleni

Kutokana  na hali hiyo serikali Wilayani Kibondo inalenga kuweka sheria ndogo ambazo zitasaidia wazazi ambao hawachangii chakula ili waweze kufanya hivyo kuondoa usumbufu kwa wanafunzi

Akiwa kwenye kikao cha Kamati ya Lishe wilaya Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kibondo Gabriel Chitupila amesema kwa sababu maelekezo yameshatolewa kwa wazazi na walezi na wengi hawajawa tayari kutoa michango na Watoto wanashindaa ni vema utaratibu wa sheria ndogo ukafanyiwa kazi ili kufikia malengo yanayokusudiwa

Kwa upande wake Afisa Lishe wilaya hiyo Jacklin Sospeter amesema Katika shule za Msingi 95  ambazo hazitoi chakula ni na 5 pekee na zile zinazotoa chakula ni wanafunzi wachache wanaopata huduma hiyo

Jacklini ameongeza kuwa licha ya changamoto zilizopo kumekuwepo na mwamko kwa baadhi ya wazazi katika utoaji wa chakula tofauti siku zilizopita kwani ahapo awali licha ya elimu kutolewa wazazi wengi walikuwa wanagoma kabisa ila kwa sasa hali ni tofauti ikilinganishwa na mwaka mmoja uliopita

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao