VIJANA JIAMININI NA MUWE NA MOYO WA KUFANYA KAZI


Meja Generali Hawa Kodi aliyemwakilisha Mkuu wa Majeshi Kikosini Kanembwa

Luteni Kanali Mantange Kombe Kamanda Kikosi 824 Kanembwa

Kanali Evance Malasa Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Mgeni rasmi

Janeth Alex Mmoja wa Wahitimu mafunzo ya awali ya Kijeshi Kanembwa



Kakonko. Vijana wametakiwa kujiamini na kuwa na moyo wa kupenda kufanya kazi na kuwa tayari kulitumikia Taifa ili kuwa na Taifa lenye  ustawi mzuri

 

Akiwahutubia Vijana waliokuwa wanahitimu Mafunzo ya awali ya Kijeshi vijana wa kujitolea katika Jeshi la kujenga Taifa Kikosi cha 824 Kanembwa kilichoko Kakonko Mkoani Kigoma mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi katika Mahafali hayo, Meja Generali Hawa Kodi amesema Vijana ni Taifa la leo na kesho  hivyo wana wajibu wa kujituma na kuheshimu maamuzi yao na kuzingatia Nidhamu

 

Adha ameongeza kuwa Vijana katika kujiunga na Jeshi la kujenga Taifa, walitoka kwenye maeneo mbalimbali hapa nchi na elimu,Makabila,Malezi na uelewa tofauti hivyo Serikali kupitia Jeshi imetumia Garama kubwa kuelimisha na kuwataka kuzingatia yale waliyofundishwa na kuyatendea kazi

 

Luteni Kanali  Mantange Kombe ambaye ni Kamanda Kikosi 824 Kanembwa KJ amesema Vijana hao watika mafunzo licha ya Masuala ya ulinzi ujasiriamali na Stadi za maisha waliweza kujifunza kufanya mambo sahii,sehemu sahihi, kwa wakati sahihi kwani ndiyo Dira ya Mafanikio katika maisha

 

Kutokana na mafunzo waliyoyapata yamewajenga kuwa na uzalendo katika nchi yao, Utii na ukakamavu wa hali ya juu katika kulitumikia Taifa

 

 

Baadhi ya Vijana Janeth Alex na Melensiana Wiliam waliohitimu mafunzo ya awali ya Kijeshi Oparation Miaka 60 ya Jkt 2024 katika shukrani zao, wamesema wametambua Taifa zuri ujengwa na Vijana wenye utii na nidhamu na kuahidi kudumu ndani ya maelekezo hayo siku zote kwa faida yao wenyewe na Jamii nzima ya Tanzania

 

 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kako Kanali Evance Malasa aliyekuwa Mgeni rasmi katika sherehe hizo amewahasa Vijana kutokubali kushawishiwa na kujiunga na makundi yasiyofaa kwani kufanya hivyo ni usaliti 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao