Aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilaya ya kibondo Emmanuel Gwegenyeza, amejiuzulu nafasi yake

Aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilaya ya kibondo Emmanuel Gwegenyeza, amejiuzulu nafasi yake

Akiongea na waandishi wa habari katibu wa ccm wilaya ya kibondo Hamisi Kananda amekili kuwepo kwa swala hilo na kudai kuwa ofisi yake imepokea barua ya aliyekuwa mwenyekiti huyo iliyoandikwa sep 14 mwaka huu ikieleza sababu za kujiuzulu kwake kuhama kwa shuguli zake kutoka wilaya ya kibondo na kuzipeleka wilaya ya kakonko

Amesema baada ya kupokea barua hiyo ilipelekwa kwenye kikao cha kamati ya siasa ya wilaya hiyo na kujiridhisha  kisha kukubaliana na ombi hilo kwani anabaki kuwa mwanachama wa kawaida

 

Gwegenyeza ambaye alikuwa mshindi wa pili katika kura za maone kusa nafasi ya ubunge katika jimbo la muhambwe alipoulizwa juu ya kujiuzulu kwake amesema kuwa ameamua mwenyewe baada ya kuona anatumia garama kubwa kusafiri kuja wilaya kibondo akitokea kakonko ambako alihamishia shuguli zake za kibiasha


katibu ccm wilaya ya kibondo
Emmanuel Gwegenyeza aliyekuwa mwenyekiti ccm Wilaya Kibondo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao