Kakonko;Wakazi wa wilaya ya Kakokonko mkoani kigoma wamemuomba Mkuu wa wa mkoa huo Brigedia General Msitaafu, Emmanuel Maganga kusimamia vema vyombo vya ulinzi na usalama wilayani humo baada ya kuingiwa na hofu kutokana na matukio ya mauwaji ambayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara

Mwemezi Muhingo, Mwananchi

Add caption
 Mkuu wa mkoa wa kigoma Brigedia General mstaafu akiongea na wananchi wa kakonko
Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedi General a Mstaafu Emmanuel Maganga wa tatu kutoka kulia  akiwa amekaa kwenye madawati baada ya kukabidhiwa toka kwa meneja wa NMB kanda ya magharibi mjini Kakonko
Kakonko;Wakazi wa wilaya ya Kakokonko mkoani kigoma wamemuomba Mkuu wa wa mkoa huo Brigedia General Msitaafu, Emmanuel Maganga kusimamia vema vyombo vya ulinzi na usalama wilayani humo baada ya kuingiwa na hofu kutokana na matukio ya mauwaji ambayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara

Vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikifanyika katika maeneo mengi wilayani humo, watu wananyang’anywa mali zao wanajeruhiwa na wengine kuuwawa kikatili kwa kupigwa risasi na watu ambao wamekuwa hawafahamiki huku vyombo vya ulinzi vikidai vinaendelea na uchunguzi bila kutoa maelezo yanayoeleweka kwa wananchi

Wakiongea jana katika kikao kilicho wahusisha viongozi wadini, madiwani watendaji kata na vijiji na wakuu wa Idara na kamati za ulinzi na usalama wilayani humo, mmoja wa wakazi hao Bw, Ismail Ntoteye alimwambia mkuu wa Mkoa huo kwa watu wamekuwa wakishambuliwa na kunyang’anywa vitu ambavyo wakati mwingine havina hata thamani yoyote kama simu za mkononi za kawaida na pesa ndogondogo

‘’Tunashindwa kuelewa uvamizi huu unaofanyika mapema kabisa uenda unafanywa vikundi vya uharifu kutoka nchi jirani kwa kuwa tuko mpakani na kila tunapo lieleza Jeshi la Polisi utueleza kuwa tunaendelea na uchunguzi na hatujui kama watu hao wanakatwa  na baadae tunasikia watu wengine wamevamiwa hali hii inatusababishia hofu kubwa alisema Ntoteye’’

Kwa upande wake Mkuu huyo wa Mkoa wa Kigoma Brigedia General msitaafu, Emmanuel Maganga alisema kuwa swala hilo atalifanyia kazi lakini kinachotakiwa ni wananchi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi kwani watu wengi hawajitokezi kuoa maelezo hata kama wanmfahamu mwalifu

Aidha Magnga aliwaeleza wajumbe wakikao hicho kuwa waache kutoa visingizio vya kuwa wanaowavamia ni watu wanovuka mipaka kutoka nchi jirani kwa kusema kuwa hata waalifu wanakuwemo miongoni mwao watanzania wenyewe na hawataki kuwafichua  ili wahojiwe na kama watabainika hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya

Pamoja na mambo mengine Mkuu hyo wa mkoa aliwataka viongozi wa vijiji na watendaji wa halmashauri kuhakikisha wanashirikiana na wanachi katika kazi za maendeleo kwa kuacha kuficha mambo ambayo yanaihusu jamii hali inayopelekea manung’uniko mara kunapotokea kukwama kwa shuguli hizo

Maganga alikazia juu ya Pesa zilizoahidiwa na serikali kuwa itatoa tsh milion 50 kila kijiji akiwataka kuhakikisha wanwaelewesha wananchi  wajiunge katika vikundi na hakuna kuzitumia kwa mambo mengine bali ni kwa ajili ya kuinua uchumi wa wananchi huku akisema kuwa maali pengine viongozi wa halmashauri ukiuka taratibu wanazopewa na kuamua kutengeneza vikundi vyao ili waweze kufanya ubadhilifu wa pesa za walengwa. Na kusema atakaebainika atachuliwa hatua za kisheria

Mwisho    

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao