Mkuu wa mkoa wa Kigoma Emmanuel Maganga amewataka watumishi wa Serikali kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazoea pamoja na kutafuta maslahi binafsi pasipo kuihudumia jamii kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa umma hali inayo sababisha malalamiko kwa wananchiMkuu wa mkoa wa Bligedia General Emmanuel Maganga alipokuwa akizungumza na wakazi wa kifura alipotembelea kituo cha afya na kuweka jiwe la msingi katika nyumba ya mganga

Mkuu wa mkoa wa kigoma Emmanuel Maganga akiongea na wakazi wa kifura alioweka jiwe la msingi katika nyumba ya mganga wa kituo cha afya kushoto Ruth Msafiri Mkuu wa wilaya ya kibondo


Mkuu wa mkoa wakigoma Emmanuel Maganga akiweka jiwe la msingi katika nyumba ya mganga kituo cha afya kifura

Mkuu wa mkoa wa Kigoma  Emmanuel Maganga amewataka watumishi wa  Serikali kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazoea pamoja na kutafuta maslahi binafsi pasipo kuihudumia jamii kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa umma hali inayo sababisha malalamiko kwa wananchi

Kauli hiyo ametoa  jana wakati akizungumza na wakuu  wa Idara za halmashauri na serikali kuu mjini kibondo mkoani humo, katika ziara yake ya kujitambulisha baada ya kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa kigoma akisisitiza kuwa,hali hiyo ndiyo inayopelekea kuwepo kwa mianya ya rushwa na ubadhilifu wa mali za serikali

Alisema kuwa wapo watumishi wa serikali wasiyokuwa waadilifu na wasijali kazi zao na kutimiza wajibu wao  kwa kutumia taaluma zao huku wakitafuta faida zao wenyewe bila kujali wananchi vitendo ambavyo havikubali kwani vinasababisha usumbufu usiyokuwa wa lazima  kwa wananchi

‘’Kila mtu akitimiza wajibu wake kwa kufuata taratibu na miongo ya utumishi wa umma hakuna sababu ya wananchi kulailalamikia serikali hadi kuta kufanya maandamano na anayeona hawezi kufuta taratibu za kazi kwa kuwatumikia wananchi ajiondoe mapema kuliko kuendelea kuvuluga alisema Maganga’’ 

Katika ziara hiyo aliweza kutembelea baadhi ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali kwa kuwashirikisha  wananchi ambapo alikagua utengenezaji wa madawati na ukarabati wa vyumba vya madarasa na kujionea hali ngumu ya ukosefu wa vyoo katika shule ya msingi Kumhama na Shunga na kuwataka walimu kutumia vizuri pesa wanazotolewa na serikali


Aidha Mkuu huyo wa mkoa wa kigoma alitembelea kituo cha Afya kifura na kuweka jiwe la msingi katika Ujenzi wa nyumba ya kuishi watumishi wa afya, nakukagua jengo la upasuaji lililokwishaanza kazi  yake na kuwataka wananchi kulinda kutunza mali za umma na kuthamini misaada inayotolewa na mashirika mbalimbali kupitia serikalini   

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao