Kakonko; Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kulinda mali za umma huku wakitambua kuwa ni kodi za na ni kwa manufaa yao wenyewe hivyo hawana budi kutoa taarifa katika mamlaka husika pale wanapoona kuna dalili za kuhodhiwa au kuhujumiwa kwa mali hizo

Baadhi ya wananchi na wafanyakazi wa halmashauri ta kakonko waliohudhiria utilianaji wa sahihi mkataba ujenzi wa halmashauri hiyo kati yake na kampuni Magaco ya mjini Dodoma
Kakonko; Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kulinda mali za umma huku wakitambua kuwa  ni kodi za na ni kwa manufaa yao wenyewe hivyo hawana budi kutoa taarifa katika mamlaka husika pale wanapoona kuna dalili za kuhodhiwa au kuhujumiwa kwa mali hizo

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma Lusubiro Joel akizungumza wakati wa hafla fupi ya kutiliana saini mkataba wa ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya wilaya hiyo na Mkandarasi Magacon Constraction limited ya Mjini Dodoma juzi, Lusubiro alisema watu wengi ubaki wakilalamika  badala ya kutoa taarifa ili kuzuia uharibifu zaidi huku akiwasisitiza wananchi kutembelea eneo la ujenzi wa osifi hizo na kuhoji pale wasipoelewa mambo juu ya mambo yanayoendelea

‘’Tumeamua katika halmashauri yetu kufanya mambo wazi hale yale yanayotakiwa kuwa wazi kwakuwa tofauti hatua hiyo, kazi au mikataba inapokwenda tofauti na wananchi waposhirikishwa baada ya mapungufu kuonekana ndicho chanzo cha jamii kukata hata kujitoa kushirika katika miradi ya maendeleo tena inayowahusu wao wenye alisema Lusubiro’’

Halmashauri hiyo changa  changa, kwa sasa inatumia majengo ya kuazima kwa ajili ya kuendesha shughuli zake hali ambayo imekuwa haikidhi mahitaji kwakuwa ofisi zingine ziko kwenye makazi ya watu kama alivyoeleza Juma Maganga mwenyekiti wa Halmashauri hiyo huku Mkurugenzi wa Kampuni iliyochukua Kandarasi ya ujenzi huo Philipo Majani akiahidi kumaliza kwa muda uliopangwa

Ujenzi wa ofisi hizo unatarajia kugarimu kiasi cha  shilingi Bilion 2.6 hadi kukamilika na mkataba wa awali unaolenga sehemu ya ofisi hizo unatarajia kugarimu shilingi milion 365.

Mkuu wa wilaya hiyo Canal Hosea Ndagala amemtaka mkadarasi huyo kufanya kazi kwa uadilifu akitambua kuwa fedha hizo ni nyingi na kuwa ni fedha za walipa kodi, huku mmoja wa watumishi wa halmashauri ya kakonko Christopha msafiri akieleza shida wanazokumbana nazo kutoka na uhaba wa vyumba vya kufanyia kazi

Eneo litakalo jengwa ofisi za halmashauri w kakonko 




Philipo Majani mkurugenzi wa kampuni ya Magacon wakipeana mikono na mkurugenzi mtendaji halmashauri ya kakonko Lusubiro Mwakabibi baada ya kusainiana mkataba wa ujensi
Baadhi ya  wananchi waliohudhulia hafla hiyo ambapo mmoja wao  ni Masoud Halfan wamefuhishwa na kitendo cha kushirikishwa katika zoezi la utiaji saini wakieleza kuwa mambo mengi yamekuwa yakiendeshwa kimyakimya hatua ambayo isingewezekana kuingilia kati pale mambo yanapokwenda tofauti kwani wanakuwa hawafahamu kinachoendelea 

Mwisho 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao