Maafisa wa jeshi la ulinzi wa rais wamehusika katika shambulio dhidi ya makao makuu ya chama cha upinzani, watu wawili waliojeruhiwa wameambia BBC.

Add caption
Maafisa wa jeshi la ulinzi wa rais wamehusika katika shambulio dhidi ya makao makuu ya chama cha upinzani, watu wawili waliojeruhiwa wameambia BBC.
Makao makuu ya vyama vitatu vya upinzani katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo yaliteketezwa moto katika mashambulio ya usiku kwenye mji mkuu Kinshasa.
Kumekuwa na miili ya watu wawili ilioteketezwa moto katika ofisi hizo zilizoharibiwa za muungano mkuu wa upinzani DRC (UDPS).
Msemaji wa jeshi la Congo ameiambia BBC hana la kusema kuhusu shutuma hizo.
Upinzani unasema zaidi ya watu 50 wameuawa Jumatatu wakati wa maandamano kumpinga rais Joseph Kabila.
Serikali inasema idadi ya waliouawa ni watu 17.
Vikosi vya usalama vimeshutumiwa kwa kutumia risasi dhidi ya waandamanaj hao wa amani waliotaka kutolewa tarehe ya uchaguzi wa urais nchini.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Shule ya msingi Nengo ya Walemavu, iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma, inayohudumia wanafunzi walemavu wa mahitaji maalum inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni ukosefu wa maji Vifaa vya kujinfunza na kufundishia na vyombo vya kulia chakula