Kakonko;Vijana wanaomaliza mafunzo awali ya kijeshi katika vikosi vya jeshi la kujenga Taifai hapa nchini wametakiwa kuwa na unyenyekevu na nidham na kufuata taratibu na sheria za nchi wakizingatia mafunzo na maelekezo wanayopewa, ili jamii iweze kupata manufaa ya kuwepo kwa jeshi hilo

Mwemezi MuhingoMwananchi







Kakonko;Vijana wanaomaliza mafunzo awali ya kijeshi katika vikosi vya jeshi la kujenga Taifai hapa nchini    wametakiwa kuwa na unyenyekevu na nidham na kufuata taratibu na sheria za nchi wakizingatia mafunzo na maelekezo wanayopewa, ili jamii iweze kupata manufaa ya kuwepo kwa jeshi hilo

Akiwahutubia jana, mamia ya wahitimu wakufunzi , Askali na wananchi wa kawaida wakati wa kufunga mafunzo ya kijeshi kwa vijana mujibu wa sheria Oparation Magufuli Mkuu wa wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma Canol Hosea Ndagala ambae alikuwa mgeni rasmi kikisi 824 Kanembwa amesema kwa kuwa Askali ni Raia daraja la pili hivyo ni lazima kufuata maadili na kinyume chake huyo si Askali

Mkuu wa JKT hapa nchini Brigedia General  Michael Isamuyo  aliyewakilishwa na Luten Canol Joseph P Mahende aliwambia wahitimu hao kuwa ni mambo mengi waliyojinfunza jeshini ambayo hapo awali hawakuyafahamu walipokuwa mashuleni, hivyo ni vema wakayazingatia kwa ajili ya  Faida yao na Taifa kwa ujumla huku Mkuu wa Kikos hicho Luten Canol Amos Molo akieleza kuwa vijana hao wamepata mafuzo katika silabi mbalimbali kulingana na ngazi yao 

Awali Katika lisara yao wahitimu hao, iliyosomwa na Karoline Aweso  walisema kuwa changamoto ambazo wamekabiliana nazo ni ukosefu Gari la kubeba wagonjwa kikosini hapo hali ambayo inasababisha usumbufu pale anapotokea  mgonjwa na kupewa rufaa na kuiomba serikali kukipatia kikosi hicho Gari la kubeba wagonjwa ili kuondoa usumbufu
  
Ibrahim Bewe, ambaye ni mmoja wa wahitimu aliipongeza serikali kwa uwamuzi wake wa kurejesha tena upya jeshi la kujenga Taifa ambalo lilistishwa miaka iliyopita akieleza kuwa JKT kimekuwa ni kitovu muhimu kwa malezi ya Vijana huku akiwataka vijana wenzake wanaopata nafasi kujiunga na  jkt kutozipuuza

Vijana walihitimu mafunzo hayo ya Kijeshi kwa mujibu wa sheria oparation Magufuli, ni wale waliomaliza kidato cha sita mwaka huu na waliobahatika kumaliza katika kikosi cha 824 kj Kanemba JKT ni 11016
Mwisho 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao