Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2017

Kakonko;Wachimbaji wadogo madini wa Mgodi wa Nyamwilonge wilayani Kakonko Mkoa wa Kigoma wametoa msahada wa mifuko 20 ya Saruji kama mchango wao akatika jamii ili kupunguza changamoto za upatikanaji wa vyumba vya madarsa katika shule ya msingi Kakonko

Picha
Mkuu wa wilaya ya Kakonko mwenye shati la mistari akikabidhiwa mifuko ya saruji na katibu wa wachimbaji wadogo Omary Bakora kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Kakonko Mkuu wa wilaya ya Kakonko mwenye shati la mistari akikabidhiwa mifuko ya saruji na katibu wa wachimbaji wadogo Omary Bakora kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Kakonko Kakonko; Wachimbaji wadogo madini  wa Mgodi wa Nyamwilonge wilayani Kakonko Mkoa wa Kigoma wametoa msahada wa mifuko 20 ya Saruji kama mchango wao  akatika jamii ili kupunguza  changamoto za upatikanaji wa vyumba vya madarsa katika shule ya msingi Kakonko Akikabidhi Sauruji hiyo katibu wa wachimbaji hao,Omary Bakora, amesema kwa kuwa wao ni sehemu ya jamii wameamua kuchangia ili watanzania waweze kupata elimu Bora ila ni baada ya kuona matatizo yanayoikabili sekta elimu juu ya miundo mbinu ya Madarasa na Madawati Akipokea msaada huo wa saruji juzi    alisisitiza msaada huo kuk

Burundi:Kutokana na hali ya usalama kwenye mipaka ya nchi za Burundi na Tanzania kulegalega kwa kushamili vitendo vya uharifu wa kutumia siraha Kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma imekutana na Kamati za ulinzi za mikoa ya Cankuzo, Ruyigi, Kitega nchini Burundi na kuweka mikakati ya kuzuia uharifu huo unaoendelea kugarimu maisha ya watu na mali zao

Burundi : Kutokana na hali ya usalama kwenye mipaka ya nchi za Burundi na Tanzania kulegalega kwa kushamili vitendo vya uharifu wa kutumia siraha Kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma imekutana na Kamati za ulinzi za mikoa ya Cankuzo, Ruyigi, Kitega nchini Burundi na kuweka mikakati  ya kuzuia uharifu huo unaoendelea kugarimu maisha ya watu na mali zao Akiongea katika Kikao hicho kilichofanyika juzi Mkoani Ruyigi Nchini Burundi mkuu wa wilaya ya Kibondo Tanzania, Luis Bura alisema makundi ya uharifu yanayoonekana kuvuka mipaka na kufanya ujambazi kwa kufanya mauwaji yanakuwa ni tishio kwakuwa Watanzania hivi sasa hawafanyi kazi zao kwa amani na kuvitaka vyombo vya ulinzi pande zote kushirikina ‘’Makundi ya waharifu wanao tumia siraha wanaonekana kuvuka mika na kuingia nchini mwetu kuuwa watu sasa mauwaji ya raia wetu sasa basi kinachotakiwa kamati zenu na serikali kwa ujumla kuliangalia kwa umakini mkubwa jambo hili maana ni hatari sana watu wet kwa sasa
Picha
Kibondo; Kutokana na ujio wa wakimbizi toka nchini Burundi na kuongezeka idadi ya watu wanofika kufanyakazi  katika mashirika ya kuhudumia wakimzi wilayani Kibondo mkoani Kigoma imedaiwa kuwa ni chanzo cha ongezeko la maambukizi ya Virus vya ukimwi Inadaiwa  Mabinti wengi wameanza kutoka maeneo ya vijijini na kujikusanya kwenye madangulo kwa ajili ya kujiuza kutokana na msongamano wa watu kuwa wengi na wenye tabia tofauti kwa ajili ya kutafuta pesa  Kutokana na hali hiyo, kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo kilichoketi Juzi,ambao ni Hadija Maulid na Fales Nzobona, wameitaka serikali kupiga marufuku na kusambaratisha maeneo yote yanayojihusisha na biasha ya matendo ya Ngono yakiwemo Madangulo na uvaaji wa mavazi yanayosadikiwa kuchoe hali hiyo kwa wanawake na wasichana '' Inashangaza wasichana kuvaa mavazi ya ajabu na wanatoroka vijijini kuja mjini pia wapo baadhi ya viongozi wa Dini wanao wapotosha wananchi kula vyakula vya aina flani ili wataka

Chama cha walimu CWT wilayani kakonko mkoani kigoma kina idai halimashauri ya wilaya hiyo jumla ya shilingi Milioni 173,442,450 ambazo ni kutokana na uhamisho wa baadhi ya walimu,madai ya likizo, na fedha za kujikimu ambazo hawa kupatiwa kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.

Chama cha walimu CWT wilayani kakonko mkoani kigoma kina idai halimashauri ya wilaya hiyo jumla ya shilingi Milioni 173,442,450 ambazo ni kutokana na uhamisho wa baadhi ya walimu,madai ya likizo, na fedha za kujikimu ambazo hawa kupatiwa kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo. Hayo yalibainishwa  jana na mwenyekiti wa chama cha walimu  wilayani humo Tumaini Daniel alipokuwa akizungumza kupitia kikao cha walimu wa shule za msingi na sekondari walipokutana kwa lengo la kujadili namna bora ya kufanya ili kuendelea kuboresha hali ya ufaulu kwa wanafunzi wa shule zilizopo katika wilaya hiyo. Daniel alisema madai hayo ni ya walimu wa shule za msingi na sekondary na kwamba katika halmashauri hiyo kumekuwa na uhamisho kwa walimu usiozingatia utaratibu hali ambayo inawakatisha tamaa katika ufundishaji ili kuendelea kuinua kiwango cha ufaulukwawanafunzi. Hata baadhi ya walimu Jesca Mpongo na Adrian Gaspal, walisema kuwa wamekuwa wakipigwa tarehe mara wanapofika kuomba waweze kulipwa

Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kujitoa katika kuchangia huduma mbalimbali za kuokoa maisha ya wenzao kwa nyakati ambazo wao wanakuwa hawana uwezo wa kujihudumia kwa namna yoyote ile

Picha
Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kujitoa katika kuchangia huduma mbalimbali za kuokoa maisha ya wenzao kwa nyakati ambazo wao wanakuwa hawana uwezo wa kujihudumia kwa  namna yoyote ile Kutokana na hali hiyo waendesha vikipikipiki ambao ni kundi linalohitaji damu mara baada ya kupata ajali wahamasishwa kuchangia damu kwa hiari  wajitokeza kwa wingi kwa ajili wananchi wenzao na akiba kwao Akiongea jana Katika zoezi la uchangiaji damu lililofanyika mjini Kibondo Mkoani Kigoma kwa kuwahusisha waendesha Pikipiki maarufu Bodaboda mkufunzi wa mafunzo ya udereva toka shirika linalojihusisha na utoaji wa mafunzo hayo la APEC,  Katema Kazwika alisema watu wengi mahospitalin wamekuwa wakipoteza maisha kabla ya wakati kutokana na kukosa huduma ambazo ziko chini ya uwezo wa binadamu Kazwika ambae pia alimwakilisha Mkurugenzi wa shirika hilo Respicius Timanywa, katika kufunga mafunzo ya waendesha pikipiki, alisema kuwa pamoja na kampeni yao ya uhamasishaji wa wateja wao kujitol