Chama cha walimu CWT wilayani kakonko mkoani kigoma kina idai halimashauri ya wilaya hiyo jumla ya shilingi Milioni 173,442,450 ambazo ni kutokana na uhamisho wa baadhi ya walimu,madai ya likizo, na fedha za kujikimu ambazo hawa kupatiwa kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.

Chama cha walimu CWT wilayani kakonko mkoani kigoma kina idai halimashauri ya wilaya hiyo jumla ya shilingi Milioni 173,442,450 ambazo ni kutokana na uhamisho wa baadhi ya walimu,madai ya likizo, na fedha za kujikimu ambazo hawa kupatiwa kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.

Hayo yalibainishwa  jana na mwenyekiti wa chama cha walimu  wilayani humo Tumaini Daniel alipokuwa akizungumza kupitia kikao cha walimu wa shule za msingi na sekondari walipokutana kwa lengo la kujadili namna bora ya kufanya ili kuendelea kuboresha hali ya ufaulu kwa wanafunzi wa shule zilizopo katika wilaya hiyo.

Daniel alisema madai hayo ni ya walimu wa shule za msingi na sekondary na kwamba katika halmashauri hiyo kumekuwa na uhamisho kwa walimu usiozingatia utaratibu hali ambayo inawakatisha tamaa katika ufundishaji ili kuendelea kuinua kiwango cha ufaulukwawanafunzi.

Hata baadhi ya walimu Jesca Mpongo na Adrian Gaspal, walisema kuwa wamekuwa wakipigwa tarehe mara wanapofika kuomba waweze kulipwa stahiki zao bila mafanikio kwa muda mrefu hali waliyitaja kuwa niya kuwavunja moyo ikilinganishwa pia na mazingira magumu ya kazi kwa baadhi yao

‘’Unakuta mtu unahamishwa kutoka eneo moja hadi lingine ujalipwa chochote na unakokwenda ni kugumu mazingira si rafiki ila unaamua kwenda tu kwa kuwa uliomba kazi huku ukifuatiliwa lazima ufanye kazi kwa namna fulani ukisitizwa kuacha malalamiko jamani hata malipo ya kuhamishwa si ni haki kwa mfanya kazi? Alisema Mpongo’’
Kwa upande wake Afisaelimu shule za sekondari Christopha Bukombe akimwakilisha mkurugenzi wa halmashauri hiyo alisema ombi lao atalifikisha ofsi ya mkurugenzi ili kuona namna ya kuweza kufanya ili kutatua changamoto hizo zinazowakabili walimu wa wilaya hiyo.

Kasuku Bilago ambae ni Mbunge wa Jimbo la Buyungu wilayani humo hivi karibuni katika moja ya mikutano yake alisema kuwa yapo malalamiko kwa walimu na watumishi wengine wa halmashauri hiyo kuhamishwa kama adhabu kwa madai ya kisiasa na kusema kuwa ni haki ya mfanyakazi kujiunga na chama chochote anachotaka  na kuwataka  wafanyakazi kuacha kujihusisha na siasa mahala pa kazi kwa kufanya hivyo ni kifume cha taratibu
Mwisho



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao