FPCT NYAWELA WAZINDUA JENGO JIPYA

 Kanisa la Free Pentekote Tanzania FPCT Kibondo Mkoani Kigoma limefanya uzinduzi wa Jengo la Kanisa Jipya katika Mtaa wa Boma Nyawela, ambalo ujenzi wake ulilianza ujenzi wake mwaka 2021 na linatarajia kukamilika mwaka huu 2023

Akizindua Jengo la Kanisa hisa hilo Askofu wa Kanisa la FPCT  Meshak Buhimbi amewapongeza Wahumini wa Kanisa hilo kujitolea Michango yao na kuhakikisha wanafanikisha malengo yao huku akiwataka kuendelea kujitoa kwa kazi zingingine za kijamii na kuwasaidia wahitaji

Akiwa katika Ibada ya  kuadhimisha siku hii ya Pasaka Jamii imehaswa kushirikiana na serikali kupinga Vitendo viovu ili kudumisha Amani ya nchi kama anavyoeleza Askofu kanisa la Free pentekoste Kibondo Meshack Buhini katika Ibada iliyofanyika Kanisa la Nyawela Kibondo ambapo amesema licha ya uwepo wa sheria ipo haja ya Watu kujiepusha na uharifu kwa hiali yakiwemo mapenzi ya jinsia moja 

Aidha meshak amesema licha ya uharibifu mkubwa unaonekana kutokana na mmomonyoko wa maadili ndani ya jamii Wakristo hawatakiwi kukata tamaa bali wawaeleze wenzao yakiwemo malezi bora kwa Watoto wao  na kukataa uovu wa kila aina vikiwemo Vitendo vya Ushoga kwani ni Kinyume cha Maadili na Mila za Afrika na Tanzania

 Nao baadhi ya Vijana ambao ni Wahumini wa Kanisa hilo, Nelson Malaki na Diana Jackson wamesema mmomonyoko wa maadili umekuwa ukichangiwa na baadhi ya wazazi kutokaa na Watoto wao na kuwaelekeza yanayowapasa kutenda badala yake muda wote wako katika masuala ya kutafuta fedha

''Tunaiomba jamii na serikali waendelee kutoa elimu za makuzi kwa Vijana na matumizi mazuri ya mitandao ambayo inatajwa kutumika Vibaya na wazazi watenge muda wa kuzungumza na Watoto wao namna ya kuishi kwa maadilihasa kwa makundi ya Vijana alaisema Diana



Jengo jipya la Kanisa la fpct Nyawela Kibondo Kigoma lililozinduliwa April 9,2023




Nelson Malaki Mhumini

Diana Jackson Mhuumini

Meshack Buhimbi Askofu Kanisa la FPCT KIBONDO

Askofu Buhimbi akikata utepe wakati akizindua Jengo la Kanisa la FPCT Nyawela



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao