WATAALAM WA KILIMO TIMIZENI WAJIBU WENU



























WATAALAM WA KILIMO TIMIZENI WAJIBU WENU


Kibondo. Wataalam wa Kilimo Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wametakiwa kutimiza Wajibu wao kufanya kazi kwa weredi na uadilifu ili kuboresha sekta ya Kilimo

Wakulima wamekuwa wakikatishwa tamaa na mienedo ya baadhi ya Maafisa Ugani maeneo ya Vijijini kutokana na baadhi yao  kutokuwa na kutowafikia Wakulima ili kuwaelekeza  namna ya  kuendesha shughuli za Kilimo na uzalishaji kuwa katika viawango visivyoridhisha

Akifunga mafunzo  kwa Maafisa Ugani  wa Halmashauri za Wilaya za Kasulu na Kibondo Mkuu wa Idara ya Kilimo na Mifugo  Wilaya ya Kibondo Gabriel Chitupila akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Diokles Lutema  jana aliwataka Maafisa Ugani hao kuwasaidia wakulima kwa hali na mali kwani wengi wamekuwa wakikosa ushauri wa kitaalam na kulazimika kuendesha kilimo isivyostaili

Chitupila aliongeza kuwa Mafunzo hayo ya siku tano kwa Maafisa ugani hao kwa ajili ya kuwajengea uwezo Maafisa ugani hivyo wayatumie vema kuwasaidia Wakulima namna kuandaa Mashamba Kupanda , Kuvuna hata kuhifadhi Mazao

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Chama cha Wahitimu wa Chuo Kikuu cha KilimoSokoine Morogoro SUA SUGECO  na kufadhiliwa na shirika la maendeleo la Umoja wa Mtaifa UNDP  kupitia Mpango wa pamoja Mkoani Kigoma

‘’Kutokana na mchango wa UNDP SUGECO  katika Sekta ya Kilimo Wilaya yangu inaahidi kushirikiana na SUGECO na UNDP katika kuhakikisha mafunzo haya yanaleta tija katika maeneo lengwa ya Mradi na maeneo mengine kwa ujumla ikikumbukwa kwa sasa Wananchi wa Kibondo wanategemea Kilimo cha Mhogo kibiashara’’alisema Chitupila

Erick Thomas ambaye ni Mkufunzi kutoka Chama cha Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Kilimo SUGECO alisema wameweza kutoa mafunzo kwa maafisa Ugani 7 kutoka Kibondo na watatu kutoka Kasulu na Waratibu wawili ili kujenga uelewa na ujuzi  ambao watasaidia Wakulima  40 kila mmoja

Aidha amebainisha kuwa wamejifunza namna ya kukausha Mhogo kwa njia ya Teknolojia ya Umeme Jua yaani Solar ambao utasaidia kuandaa bidhaa bora kwa ajili ya ushindani wa Kibiashara kutokana na Mhogo unaokaushwa na jua kukosa ubora

Vile vile mradi huu unahusisha utoaji wa pembejeo bora kwa Wakulima ikiwemo mbegu bora  za Mahindi ya Njano KG 3000 Maharage Kg 1000 Mbegu za Mhogo kwa eneo la Hekali 20 na Mbolea aidha Mradi kupitia watafanya Tathmini ya masoko kwenye Mnyororo wa thamani wa Mahindi,Mhogo na Maharage na kufunga Kaushio linalotumia mwanga wa Jua Solar dryer katika Halmashauri ya Kibondo ili kuwasadia wakulima kuongezea thamani Mazao yao

Nao baadhi ya Washiriki ambao ni Devotha Balenga  na   Mohamed Mambo  wakitoa shukrani zao wameahidi kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu na miongozo ya kazi ili kutoa mwelekea wa masuala ya kilimo kwa wakulima ili kufikia malengo yanayokusudiwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao