SEKTA BINAFSI KUSHIRIKISHWA UENDESHAJI RELI

 


SEKTA BINAFSI KUSHIRIKISHWA UENDESHAJI RELI

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Prof.Godius Kahyrara amesema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu na sheria zinazosimamia usafiri wa reli Nchini ili kuruhusu sekta binafsi kuendesha treni zao katika reli ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) na ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA).

 

Prof. Kahyrara ameyasema hayo jijini Dodoma wakati aliposaini mkataba wa Utendaji kazi kati yake na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC)Masanja Kadogosa na kusisitiza kuwa tija ya maboresho hayo ni pamoja na kukuza patola taifa na urahisi kwenye usafirishaji wa mzigo kutoka eneo moja kwenda jingine.

 

“Shirika la TAZARA na TRC ni miongoni mwa mashirikayanayopewa kipaumbele kwa sasa katika sekta ya Uchukuzi na maeneo yanayotazamwa ni pamoja na uboreshaji wa miundombinu ambayo kwa muda mrefu  haikukarabatiwa” amesema Prof. Kahyrara.

 

Katibu Mkuu Prof.  Kahyrara amesema maboresho yanayofanywa katika sekta ndogo ya reli yataongeza tija katika usafirishaji ikiwemo kupunguza gharama za usafirishaji na hivyo kuruhusu bidhaa kuwafikia walaji kwa kwati na kwa bei nafuu.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TRC Bw. Masanja Kadogosa amesema miradi mbalimbali ya maboresho katika reli ya kati inaendelea kutekelezwa ili kuirudisha katika ubora unaotakiwa.

 

Mkurugenzi Kadogosa ameongeza kuwa kwa reli ya Kisasa ya SGR ujenzi unaendelea na tayari baadhi ya vitendea kazi kwa ajili ya uendeshaji vimeshawasili ikiwemokichwa kimoja cha reli hiyo pamoja na mabehwa ambayo hivi karibuni majaribio yanatarajiwa kuanza.

 

Naye Mkurugenzi wa Tathimini na Ufutiliaji kutoka Wizara ya Uchukuzi Bi. Devota Gabriel amemuhakikishia Katibu Mkuu Prof. Kahyarara kuwa kitengo hichokimewekea mikakati thabiti itakayowezesha wataalam wa Wizara kusimamia kwa karibu miradi iliyopangwa kutekelezwa kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ili kuzingatia thamani na ubora.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao