Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2015

Pinda akerwa na ushirikina, dawa za kulevya

Picha
Dar es Salaam.  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amewaomba viongozi wa dini nchini kuitumia mikutano ya mahubiri kutoa elimu kwa waumini wao na wananchi kwa ujumla kuachana na imani za kishirikina za kukata viungo na  kuwaua walemavu wa ngozi (albino ). Pia, amewaomba kutumia mahubiri hayo kutoa elimu juu ya athari za dawa za kulevya kwa waumini wao na Watanzania wote kwa ujumla. Pinda alitoa wito huo jana wakati wa ibada ya uzinduzi wa Kanisa la Moravian Tanzania, Jimbo la Mashariki uliyofanyika kwenye makao makuu ya jimbo hilo, Mbagala Chamazi. Jimbo hilo linajumuisha mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Mtwara na Pwani. Akizungumza mbele ya viongozi hao wa dini kutoka ndani na nje ya nchi, Pinda alisema Tanzania bado inakabiliwa na changamoto kubwa ya matumizi ya dawa za kulevya hasa kwa vijana. “Nchi yetu imekuwa ikitajwa kwamba inatumika kwa kasi katika kusafirisha dawa za kulevya. Ni jana tu tumesikia taarifa katika vyombo vya habari zikitaja kwamba meli moja ya

Jeshi kutopendelea pande pinzani Burundi

Picha
Jeshi nchini Burundi linasema kuwa litaendelea kuwa na msimamo wa wastani baada ya siku sita za maandamano dhidi ya rais Pierre Nkurunziza. Waziri wa ulinzi (Pontien Gaciyubwenge) alisema kuwa jeshi ni lazima liheshimu katiba pamoja na makubaliano ya amani yaliyomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo. Waandamanaji hao wanamlaumu rais kwa kukiuka katiba na makubaliano hayo ya amani kwa kuwania urais kwa muhula wa tatu Mapema waandamanaji walitangaza kusitisha maandamano kwa siku mbili wakisema kuwa familia zinahitaji muda wa kuwomboleza wale waliouawa kwenye maandamano hayo. Ongeza kichwa

Jeshi lawaokoa wasichana 300 Nigeria

Picha
Jeshi nchini Nigeria linasema kuwa limeliokoa kundi la kwanza la takriban wasichana 300 na wanawake waliookolewa kutoka kwa kundi la Boko Haram kwenye kambi moja ya wakimbizi. Watu hao wanaripotiwa kusafiri kwa siku tatu kutoka msitu wa Sambisa ulio kaskazini mashariki mwa nchi. Karibu watu 700 wanaripotiwa kuokolewa wiki hii wakati jeshi linapoendelea na operesheni ya kulitimua boko haram kutoka kwa ngome zao za mwisho. Hatma ya wasichana wengine 200 waliotekwa kutoka mji wa Chibok mwaka mmoja uliopita bado haijulikani. Chanzo cha Habari hii ni Bbc Wasichana na wanawake waliokolewqa katika mikono ya Boko Harama katika msitu wa sambisa

IS yawaua raia 300 wa Yazidi nchini Iraq

Picha
Maafisa nchini Iraq wanasema kuwa wanamgambo wa islamic state wamewaua mamia ya watu wa yazidi waliokuwa wakiwazuilia eneo lililo kaskazini mwa nchi. Makamu wa rais nchini Iraq Osama al-Nujifi ameyalaani mauaji hayo akiyataja kuwa ya kikatili Taarifa zilisema kuwa hadi watu 300 waliuawa kwenye wilaya moja iliyo magharibi mwa mji wa Mosul siku ya ijumaa. Wanamgambo wa islamic state walithibiti maeneo yaliyo kaskazini mwa Iraq kwa karibu mwaka mmoja uliopita ambapo waliwaua na kuwashika mateka maelfu ya watu wa Yazidi wakiwaita makafiri. Raia wa Yazidi

Floyd Mayweather amshinda Pacquiao

Picha
Bondia wa Marekani Floyd Mayweather ameshinda pigano lililosubiri kwa wingi katika miongo kadhaa. Bondia huyo ambaye hajashindwa alimshinda mpinzani wake raia wa Ufilipino Manny Pacquiao kwa wingi wa pointi. Mashabiki wengi waliojaa katika ukumbi wa  MGM Grand Garden Arena mjini Las Vegas walimzoma mara kwa mara Mayweather. Kote duniani wateja millioni 3 walilipa kuliona pigano hilo ambalo ndio pigano lililovutia kitita kikubwa cha fedha katika historia ya ndondi. Tiketi nyingi za pigano hilo ziliuzwa katika bei ya makumi ya maelfu ya dola.

Ukawa wakuna vichwa saa 48

Picha
Dar es Salaam.   Mwenyekiti  mwenza wa Ukawa, Freeman Mbowe akizungumza wakati wa mkutano na waandishi  wa habari, Dar es Salaam jana. Wengine ni wenyeviti wenza,James Mbati,  Profesa Ibrahim Lipumba na  Dk Emmanuel Makaidi. Picha na Said Khamis  Saa 48 zilizotumika kikaoni kutafuta muafaka wa majimbo yenye utata ndani ya umoja wa vyama vya upinzani vilivyo chini ya Ukawa, zimekatika bila mafanikio na  mvutano unaonekana kubakia kwenye majimbo 12 kati ya 239 waliyopanga kugawana. Vyama hivyo vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi vimekubaliana kusimamisha mgombea mmoja kuanzia kiti cha urais hadi udiwani, lakini kazi ya kugawana majimbo imekuwa ikivisumbua na ilitarajiwa kuwa ingemalizika juzi baada ya viongozi kukutana kwa siku mbili kuanzia Jumanne. Lakini habari kutoka ndani ya kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam zinaeleza kuwa wajumbe walishindwa kufikia muafaka kwenye majimbo 12. Hata hivyo, viongozi hao wa vyama hivyo walikataa kutaja majimbo hayo

Raia wapinga mauaji ya washukiwa Garissa

Picha
Wakaazi wa mji wa Garissa nchini Kenya ambapo kulikuwa na shambulizi la kigaidi mwezi uliopita wamevishtumu vikosi vya usalama kwa kuwaua washukiwa wa ugaidi. Wakaazi hao wanasema kuwa baadhi ya raia wametoweka baada ya kukamatwa na maafisa wa usalama. Miili kumi na moja ilipatikana katika kaburi moja la jumla karibu na mji wa kazkazini mashariki wa Mandera mapema wiki hii. Kundi la wapiganaji la Alshabaab lilikiri kutekeleza shambulizi hilo katika chuo kikuu cha Garissa,ambapo liliwaua karibia watu 150. Rais Uhuru Kenyatta amesema kuwa taifa lake linakabiliwa na changaoto nyingi za usalama na kwamba serikali itafanya kila iwezalo ili kuhakikisha kuwa kuna usalama Raia wa Garissa wamewashtumu maafisa wa usalama kwa kuwaua washukiwa wa ugaidi

Waandalizi wa maandamano waonywa Burundi

Picha
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ameonya kuwaadhibu vikali wote wanaopanga maandamano ya raia dhidi yake. Kwenye hotuba aliyowasilisha kupitia kituo cha radio ya serikali, siku ya Leba Dei, Kiongozi huyo amesema serikali itaweka vikwazo vikali dhidi ya wale aliowataja kama waasi. Aidha amesema jopo maalum la mahakama limeundwa kuchunguza maandamano ambayo yameingia siku ya sita sasa. Waandamanaji wanapinga hatua ya Rais huyo kuwania muhula wa tatu. Waandamanaji Nchini Burundi

Maandamano mapya Baltimore Marekani

Picha
Kumetokea maandamano mapya nchini Marekani katika mji wa Baltimore kufuatia kifo cha kijana mweusi Freddie Gray aliyekufa kutokana na majeraha akiwa mikononi mwa polisi. Mamia ya watu wameandamana katika mitaa, wakionyesha ujasiri licha ya hali mbaya ya hewa iliyokuwepo. Matokeo ya mwanzo ya uchunguzi wa polisi wa jinsi kijana wa miaka ishirini na mitano mwenye asili ya weusi alivyouawa bado hayajawekwa hadharani. Mtetezi wa haki za binadamu, Mchungaji Al Sharpton, ameitisha mkutano mjini Baltimore ili kuimarisha uhusiano baina ya polisi na wanajamii. Maandamano Baltimore