Jeshi lawaokoa wasichana 300 Nigeria

Jeshi nchini Nigeria linasema kuwa limeliokoa kundi la kwanza la takriban wasichana 300 na wanawake waliookolewa kutoka kwa kundi la Boko Haram kwenye kambi moja ya wakimbizi.
Watu hao wanaripotiwa kusafiri kwa siku tatu kutoka msitu wa Sambisa ulio kaskazini mashariki mwa nchi.
Karibu watu 700 wanaripotiwa kuokolewa wiki hii wakati jeshi linapoendelea na operesheni ya kulitimua boko haram kutoka kwa ngome zao za mwisho.
Hatma ya wasichana wengine 200 waliotekwa kutoka mji wa Chibok mwaka mmoja uliopita bado haijulikani.
Chanzo cha Habari hii ni Bbc
Wasichana na wanawake waliokolewqa katika mikono ya Boko Harama katika msitu wa sambisa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao