Jeshi kutopendelea pande pinzani Burundi

Jeshi nchini Burundi linasema kuwa litaendelea kuwa na msimamo wa wastani baada ya siku sita za maandamano dhidi ya rais Pierre Nkurunziza.
Waziri wa ulinzi (Pontien Gaciyubwenge) alisema kuwa jeshi ni lazima liheshimu katiba pamoja na makubaliano ya amani yaliyomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Waandamanaji hao wanamlaumu rais kwa kukiuka katiba na makubaliano hayo ya amani kwa kuwania urais kwa muhula wa tatu
Mapema waandamanaji walitangaza kusitisha maandamano kwa siku mbili wakisema kuwa familia zinahitaji muda wa kuwomboleza wale waliouawa kwenye maandamano hayo.
Ongeza kichwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao