Mwanaume Furaha John, mkazi wa kijiji cha Kinonko wilaya ya Kakonko mkoani alieyejikata utumbo kwa wembe na kulazwa katika Hospitali ya wilaya Kibondo hali yake imeendelea kuimarika kutokana na na jitihada za madaktari kuendelea kumpa matibabu

Mwanaume Furaha John, mkazi wa kijiji cha Kinonko wilaya ya Kakonko mkoani alieyejikata utumbo kwa wembe na kulazwa katika  Hospitali ya wilaya Kibondo hali  yake imeendelea kuimarika kutokana na na jitihada za madaktari kuendelea kumpa matibabu

Kwa mujibu wa maelezo yake amesema  hali yake ya afya inaendelea vizuri baada kufanyiwa upasuaji na kupata matibabu maana alipofikishwa hospitalini hapo fahamu zake hazikuwa sawa kutokana na maumivu aliyokuwanayo, ila hivi sasa anaendelea vizuri maana anaweza kula,  na kutembea pia.

Hata hivyo amesema  kutokana  na matatizo aliyokutana nayo atalazimika kuachana kunywa  na kufanya biashara ya kutengeneza pombe za kienyeji maana uenda ndo zimemsababishia matatizo na ameamua kumrudia Mungu wake

Hamis Mohamed ambae ni muuguzi katika wod alimolazwa Furaha, anasema hivi sasa mgonjwa huyo anaendelea vizuri tofauti na alivyofikishwa  hospitalini hapo

Kwa upande wake Daktari ambae amekuwa akimtibu, Dr Adam Jonathan, amesema uenda akaruhusiwa muda wowote kwa kuwa hali yake imeanza kuridhisha, katika swala la kitaalam Adam amesema uenda Mtu huyo akapata tatizo la mmeng’enyo wa chakula sababu kazi hiyo ufanywa na utumbo na sasa umepungua baada ya kuondolewa

Kwa upande wake John  Nkonkoili ambaye ni Baba mzazi wa Kijana huyo, na ambaye anamuuguza, katika maelezo yake amesema kuwa yeye  Ndugu na jamaa walishangazwa na uamuzi  aliouchukua ndugu yao wa kuamua kujiua  kwa kijiumiza kiasi hicho, tena kwa kuonyesha ujasili mkubwa na kuongeza kuwa watakaa pamoja ili wajadili na kumpa ushauri ili jambo hilo lisijirudie tena

Awali Mwanaume huyo Feb 29 mwaka huu,katika  kijijini cha Kinonko, wilaya ya kakonko, alijikata Tumbo lake na kisha kuumwaga utumbo wake nje na kuanza kuukata vipande ili ajiue, baada ya kufanya jaribio la kujinyonga kwa kamba kwa madai ya Kudhulumiwa kiasi cha Tsh 35,000/ na mfanyabiashara mwenzake na baada ya kufika nyumbani kwake kunyimwa chakula na mke wake

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao