Zoezi la kumkataa katibu wa Ccm wilaya Kibondo Kigoma Hamis Kananda limechukua sura mpya Baada ya uongozi wa chama hicho mkoa, kuunda tume kwa ajili ya kuwahobi wajumbe wa Kamati ya siasa ya wilaya juu ya tuhuma zinazosukumiwa kwa katibu wao na kuamuru aachie ngazi

  Zoezi la kumkataa katibu wa Ccm wilaya Kibondo Kigoma Hamis Kananda limechukua sura mpya Baada ya uongozi wa chama hicho mkoa, kuunda tume kwa ajili ya kuwahobi wajumbe wa Kamati ya siasa ya wilaya juu ya tuhuma zinazosukumiwa kwa katibu wao na kuamuru aachie ngazi

Taarifa za ndani za  kikao cha halmashauri ya ccm wilaya kilichofanyika mjini kibondo jumatatu wiki hii,kwa kushirikiana na wajumbe  wa tume hiyo, iliyoongozwa na mwenyekiti wa ccm mkoa wa Kigoma Bw, Aman Kaburu  kwa ajili ya kuchunguza tuhuma zinazomkabili Hamis Kananda, baada ya kuhoji  pande zote mbili,zinaeleza  kuwa katibu huyo alitumia vibaya madaraka yake kwa kukiuka taratibu na kukihujumu chama hicho

Kutokana na jazba walizokuwa nazo wajumbe wa kikao hicho awali viongozi wa ambao ni kalembe Masod, katibu mwenezi Mkoa, walijitahidi kuwatuliza  ili mkutano uweze kwenda kwa amani na utulivu ili lengo linalokusudiwa liweze kupatikana   

Kwa mujibu wa maelezo ya katibu mwenezi  wa ccm wilaya hiyo, Hamisi Tairo,  alipokuwa akihojiwa na  na Gazeti hi, alisema kuwa  Katibu huyo wa Ccm wilaya ya kibondo Bw, Hamis Kananda, anatuhumiwa kuhujumu mali za chama hicho, ikiwemo fedha zaidi shilingi milion 77 milion 10 kwa ajili kujenga wod hospitalini na milion 67 za posho za mabalozi tawi na vijiji

Aidha lisema  kuwa baada ya uongozi mkoa wa kigoma kupitia taratibu zote za vikao na kubaini matatizo yote,  , hivyo kuonekana kuwa katibu kananda  si mwaminifu,  kikao hicho kilitoa maamuzi kuwa katibu huyo Hamas Kananda, kusimama kazi au kuhamishiwa kituo kinginge.   

Baadhi ya wajumbe waliokuwa kwenye kikao hicho cha halmashauri kuu ya ccm wilaya ambao ni Tatu Barakabise na Ayub Mnyiriri, jana  waliutaka uongozi wa juu kutatua migogoro kwani inasababisha watu kioamini chama na baadae kuleta migongano huku wakimtaka katibu huyo kwakuwa amebainika alipe fedha alizopoteza

Kwa upande katibu huyo anayelaumiwa alipouliza juu ya tuhuma hizo zinazozidi kuongezeka amesema kuwa yeye hajaiba pesa yoyo na alishahojiwa na tume hiyo kwenye kamati ya siasa ya wilaya alikuwa anasubiri kukaguliwa kwa mujibu wa taratibu za kifedha, na fedha zote za mabarozi anazotuhumiwa kuiba aliwalipa kwa mujibu wa Taratibu na nakala zipo zinaonyesha wazi

Aliongeza kuwa halmashauri haikutakiwa kujadili  swala hilo bila kuomba zinazoonyesha malipo jinsi yalivyofanyika na kueleza kuwa kamati hiyo niya kisiasa na mgogoro huwo unatengezwa na mtu ili kumchafua kuhusu kuenguliwa kwake amesema yeye bado hajapata barua ya kumsimamisha kazi wala kuhama na ni katibu halali wa ccm Wilaya ya kibondo

Ikumbukwe kuwa mnamo 16 feb mwaka huu kiliitishwa kikao cha halmashauri kuu wa wilaya kwa ajili ya kufanya tathimini ya uchaguzi mkuu uliofanyika 25 octoba 2015  ulivyoenda badala yake kibao kilimgeukia katibu huyo baada ya wajumbe kutaka isijadiliwe agenda yoyote mpaka katibu wa ccm wa wilaya hiyo aleze upotevu wa shiling 10 milion za chama hicho, hali ilizua mtafaluku na kikao kuvunjika na kupelekea uongozi wa mkoa kuingilia kati 

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao