Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2016

Katika kuitikia juhudi za serikali za kuboresha huduma za afya na kuokoa maisha ya Watoto na wanawake wajawazito wanaokwenda kujifunguawa katika Zahanati vituo vya afya na hosipitali kote nchini jamii imetakiwa kujitoa kwa hasa na mali hata pale serikali inapokuwa haijafikisha huduma zake

Picha
Katika kuitikia juhudi za serikali za kuboresha huduma za afya na kuokoa maisha ya Watoto na wanawake wajawazito wanaokwenda kujifunguawa   katika Zahanati vituo vya afya na hosipitali kote nchini jamii imetakiwa kujitoa kwa hasa na mali hata pale serikali inapokuwa haijafikisha huduma zake Wito huo umetolewa  wakati wa mkutano wa uchangiaji wa miundo mbinu ya umeme katika zahanati ya Kijiji cha kumhama kata ya Bitare wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma ambapo mwananchi mkazi wa kijiji hicho aliamua kulipia milion moja  baada ya kuona shida wanazozipata wanawake mara wanapofikishwa katika zahanati nyakati za usiku kwa kutumia vibatari na tochi za simu Akipokea msahada huo wa tsh milion moja Diwani wa kata hiyo Julias Kihuna amempongeza mwananchi huyo kwa moyo wa uzalendo na kusema kuwa licha ya kuwa alishachangia pamoja na wananchi wenzake ameamua ajitolee ili tatizo liweze kumalizika na wauguzi pamoja na wanaitaji huduma wasiendelee kupata shida huku muuguzi wa zahanati hio, Lidi

Kutokana nakutoshirikishwa kwa baadhi ya viongozi wa ngazi mbalimbali hapa nchini juu ya maswala yanayohusu maendeleo katika jamii hali hiyo imetajwa kuwa ni njia mojawapo inayosababisha kutofikiwa kwa malengo yanayokuwa yamekusudiwa

Picha
Kutokana nakutoshirikishwa kwa baadhi ya viongozi wa ngazi mbalimbali hapa nchini  juu ya maswala yanayohusu maendeleo   katika jamii hali hiyo imetajwa kuwa ni njia mojawapo inayosababisha kutofikiwa kwa malengo yanayokuwa yamekusudiwa Akizungumza katika ufunguzi wa warsha ya Madiwani iliyoandaliwana mfuko wa maendeleo ya jamii Tasaf, mkuu wa wilaya Kibondo mkoani Kigoma Bi Ruth Msafiri aliyewakilishwa na Kaimu katibu tawala wa wilaya hiyo Bw, Moshi Husein amesema kuwa pasipokuwepo na umoja na ushirikiano katika kutatua kero za wananchi serikali itaendelea kulaumiwa pasipo sababu na hatua za kufikia malengo zitakwama Warsha  hiyo iliandaliwa na tasaf wilaya Kibondo kwa ajili ya   kujenga uelewa juu ya shuguli zinazofanywa na Mfuko huo, juu  ya kunusuru kaya masikini katika maeneo yao ambapo mwanzoni hawakuweza kushiriki kabisana wala kuhusishwa na kazi za mpango huo ambapo Mkufunzi katika warsha hiyo Mhamed  Motomoto, aliwataka madiwani kutoa ushirikiano kwa ajili ya mpango h

Alieyekuwa Askofu wa Dayosisi ya Western Tanganyika Mkoani kigoma Naftali Bikaka, alieyefariki Dunia Mei 3mwaka huu alizikwa jana wilayani Kibondo

Picha
Alieyekuwa Askofu wa Dayosisi ya Western Tanganyika  Mkoani kigoma Naftali Bikaka, alieyefariki Dunia Mei 3mwaka huu alizikwa jana  wilayani Kibondo Akiongoza mamia ya waomboleza ji Askofu Sadock Makaya,  ambaye anaongoza Dayosesi ya  Western Tanganyika kwa sasa,  kwa niaba ya Askofu mkuu wa Kanisa la Anglikana Nchini Dr Jacob Chimeledja, alimtaja Bikaka kuwa wakati wa uhai wake alikuwa mpenda watu na alipenda kuwajenga watu katika maisha ya kujitegemea Aidha Makaya alisema wataendelea kuyaenzi yale aliyoyafanya na kuitaka jamii kuishi kwa kutenda mema kuwasaidia maskini na kumtumania Mungu na kuishi kwa kufuata maadili ya Kiroho ili amani ya Taifa ili izidi Kudumu Kwa upande wake Askofu wa Dayosesi ya KibondoDr Themeo Ndenza, alisema  swala la kuwasaidia watu au kuwatendea mema silazima kuwa kiongozi wa Dini yoyote ila kila mmoja sehemu alipo iwe mahala pa kazi kama ofisini au kwenye Biashara mtu anatakiwa kufanya yanayo ustaili ubinada Hata hivyo baadhi

Watu wanne wametolewa wakiwa hai kutoka kwenye vifusi siku sita baada ya jumba kuporomoka katika mtaa wa Huruma, Nairobi.

Picha
Watu wanne wametolewa wakiwa hai kutoka kwenye vifusi siku sita baada ya jumba kuporomoka katika mtaa wa Huruma, Nairobi. Watu watatu, wanawake wawili na mwanamume, wameokolewa saa chache baada ya mwanamke kutolewa kwenye vifusi na kupelekwa hospitalini. Juhudi za uokoaji bado zinaendelea ingawa kuna wasiwasi kwamba muda wa kupata manusura wakiwa hai unayoyoma Kwa mujibu wa Pius Masai, mkuu wa kitengo cha taifa cha kukabiliana na majanga, idadi ya waliofariki kufikia sasa imefikia 36. Watu 136 wameokolewa wakiwa hai lakini watu 70 kufikia sasa bado hawajulikani walipo. Siku mbili zilizopita, mtoto wa umri wa miezi sita aliokolewa baada ya kukaa kwenye vifusi kwa siku nne. Msichana huyo alitolewa kwenye vifusi mwendo wa saa kumi usiku na kupelekwa hospitalini Alipatikana akiwa amefunikwa kwa blanketi ndani ya ndoo na hakuonekana akiwa na majeraha yoyote. Babake mtoto huyo, Bw Ralson Wasike, akihutubia wanahabari baadaye, alisema bintiye amekuwa na nguvu sana.

Kibondo; Shule za sekondari zilizoko vijijini hapa nchini zinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwaemo ukosefu wa umememe wa uhakika kwa ajili ya kuendeshea maabara licha ya serikali kutilia mkazo ujenzi wa maabara hatua inayoweza kukwamisha ndoto za wanafunzi hasa wa masomo ya sayansiWahitimu wa kidato cha sita Shule ya sekondari wasichana Bon Consilii

Picha
Wahitimu wa kidato cha sita shule ya sekondari wasichana Bon concilii Mabamba Dr Ibrahim Mgeni rasmi Janeroza Mpilirwe mkuu wa shule Bon consilii Kibondo;  Shule za sekondari zilizoko vijijini hapa nchini zinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwaemo ukosefu wa umememe wa uhakika  kwa ajili ya kuendeshea maabara licha ya serikali kutilia mkazo ujenzi wa maabara  hatua inayoweza kukwamisha ndoto za wanafunzi hasa wa masomo ya sayansi Wakizungumza  juzi wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana  Bon consilii iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma katika mahafali ya 12 ya kuhitimu Kidato cha sita ambao ni Isabela Kilongozi na Irene Masabo walisema kuwa ukosefu wa umeme wa uhakika kwa shule zilizoko vijijini  hawapati fulsa nzuri ya kujifunza hasa masomo ya sayansi kwakuwa maabara hizo lazima  zitegeme umeme Aidha  walisema tatizo la uhaba wa walimu wa kudumu  masomo ya sayansi limekuwa likiwahathili hasa pale wanapojikuta kwa mwakammoja wanafundishwa

Kibondo; Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kuungana na kushirikiana katika shuguli za maendeleo kwenye maeneo yao ili kuweza kufikia malengo yanayokusudiwa bila kuiachia serikali peke yake

Kibondo;   Watanzania wametakiwa kujenga tabia ya kuungana na kushirikiana katika shuguli za maendeleo  kwenye maeneo yao ili kuweza kufikia malengo yanayokusudiwa bila kuiachia serikali peke yake Akizungumza jana katika kikao cha  Harambee iliyoandaliwa kwa ajili ya kuchingia madawati ya shule za msingi na sekondari Wilayani Kibondo mkoani Kigoma Bw, Philpo Kayanda Afisa Elimu Watu wazima wa Mkoa huo, aliesema kuwa bila jamii kushirikiana maendeleo hayawezi kupatikana Kayanda aliongeza kuwa watu wengi wamezoea kutoa michango mikubwa kwenye sherehe za harusi na nyinginezo kuliko kusaidia watu wenye matatizo na shughuli za maendeleo hatua ambayo imekuwa ikifanya mambo mengi kuzorota kwa madai kuwa serikali itafanya. Katika harambee hiyo, wananchi, mashirika ya umma Taasisis za serikali waliweza kutoa michango mbalimbali ili kuziba pengo kubwa la upungufu wa madawati 11,150 huku shule za msingi zinahitaji 17,740 na yaliyopo ni 12 elfu tu pungufu 7720 na sekondari yanaitajika